Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,559
- 41,075
Ukizungumzia rushwa, CCM ndiyo nyumbani kwake.
Ukizungumzia mbinu chafu za kishetani ili kupata vyeo, including ushirikina, kwa CCM ni jambo la kawaida.
Kunyanyasa watu ili mtu apate cheo (ref. majimbo yote ya kupita bila kupingwa), kwa CCM huonekana ni ushujaa.
Wizi, upendeleo, ufisadi ni tabia za kuitambulisha CCM kuliko kitu chochote.
Haya yanayoitambulisha CCM, bila shaka, inaashiria CCM inaishi na shetani. Ndiyo maana ni nadra sana kumwona mtu anayemwabudu na kumwamini Mungu wa kweli, ambaye anasisitiza upendo wa kweli baina ya wanadamu, halafu awe kada wa CCM.
Wanaiba pesa za umma bila ya kuwafikiria watu maskini wanaolipishwa kodi hata kwenye mapato yao duni kabisa (report za CAG huthibitisha jinsi wakubwa wa CCM wanavypiba na kufuja pesa ya umma, na chama chao kikiwabariki maana imekuwa kama itikadi yao).
Hazina ya wananchi, huporwa na CCM ili ikatumike katika kutekeleza uovu wa kwenda kuwahonga wapiga kura wakati wa uchaguzi (Hayati Mkapa alikiri hilo na kujutia kuwezesha uovu huo akiwa Rais na Mwenyekiti wa CCM. Mungu mwenye huruma amjalie msamaha kamili kwa majuto yake siku chache kabla ya kuhitimisha maisha yake ya Duniani).
Kwa sasa, CCM ni alama ya uovu. Jitengeni na muovu ili mpokee baraka.
Ukizungumzia mbinu chafu za kishetani ili kupata vyeo, including ushirikina, kwa CCM ni jambo la kawaida.
Kunyanyasa watu ili mtu apate cheo (ref. majimbo yote ya kupita bila kupingwa), kwa CCM huonekana ni ushujaa.
Wizi, upendeleo, ufisadi ni tabia za kuitambulisha CCM kuliko kitu chochote.
Haya yanayoitambulisha CCM, bila shaka, inaashiria CCM inaishi na shetani. Ndiyo maana ni nadra sana kumwona mtu anayemwabudu na kumwamini Mungu wa kweli, ambaye anasisitiza upendo wa kweli baina ya wanadamu, halafu awe kada wa CCM.
Wanaiba pesa za umma bila ya kuwafikiria watu maskini wanaolipishwa kodi hata kwenye mapato yao duni kabisa (report za CAG huthibitisha jinsi wakubwa wa CCM wanavypiba na kufuja pesa ya umma, na chama chao kikiwabariki maana imekuwa kama itikadi yao).
Hazina ya wananchi, huporwa na CCM ili ikatumike katika kutekeleza uovu wa kwenda kuwahonga wapiga kura wakati wa uchaguzi (Hayati Mkapa alikiri hilo na kujutia kuwezesha uovu huo akiwa Rais na Mwenyekiti wa CCM. Mungu mwenye huruma amjalie msamaha kamili kwa majuto yake siku chache kabla ya kuhitimisha maisha yake ya Duniani).
Kwa sasa, CCM ni alama ya uovu. Jitengeni na muovu ili mpokee baraka.