Rais Samia ashauriwe vyema uchumi unakufa

Obama alitoka katika familia masikini, hakuwa tajiri wala mfanyabiashara!
 
Kiukweli hali ya nchi inako kwenda sio kuzur,Ijapokuwa tunaona kawaida me nafikiri turudi kumwomba Mungu kwa dini zetu mambo yatakaa sawa,makuhani wa nchi wamejiamini kupita kiasi hata vilio vya wananchi hawavisikii
 
Kwa Magufuli mlisema ameua uchumi, kwa Samia mnasema uchumi unakufa, kwani uchumi unakufa mara ngapi?
Uchumi unaweza kufa hata mara milioni.

Uchumi una tabia ya kufa mara nyingi na kufufuka mara nyingi pia ukifufuliwa.
 
Amerithi ubishi kwa kaka yake hashauriki.
 
Rais anatakiwa awe na washauri wazuri. Unajua serikali haina uwezo wa kuajiri labor force yote hivyo ana wajibu wa kuweka mazingira mazuri kwa sekta binafsi. Sekta binafsi ndio mwajiri mkubwa kokote duniani.
Mkuu uko sahihi ila sioni kiongozi mwenye dhamira ya kuboresha sekta binafsi. Hawa viongozi ni wachoyo,wajivuni,waongo na wanyonyaji.Waache wafaidi tu.
 
Meanwhile wenzetu wanaondoa tozo katika miamala ya kifedha. Sisi ndio kwanza kuongeza kila leo

 
Serikali inakusanya tozo, ili kuongeza vituo vya afya, madarasa na shule mpya. huko kuna kuongezeka kwa ajira za serikali. Kupitia mishahara kutaongeza purchasing power ya waajiriwa wapya, mzunguko wa fedha kwenye maeneo ya waajiriwa. Pia tukumbuke shughuli za ujenzi zitarudisha fedha kwa local contractors watakao jenga vituo vya afya na mashule, vibarua watapata ajira, wafanyabishara wata supply mahitaji ya ujenzi kwa wakandarasi.

Maeneo watakayo ajiriwa watu wapya yatachochea kuongezeka kwa watoa huduma za ziada, na biashara kama mawakala wa fedha, watoa huduma za usafiri, wafanyabiashara wa furniture, electronics watafanya biashara, mabenki yatakopesha wateja wapya watakao ajiriwa. Ni kwamba hautwezi kuona mchango wa tozo ndani ya mwezi mmoja au miwili. Tujifunge mkanda kwa mwaka mmoja tutafanya evaluation ya tozo. Maendeleo yanakuja na maumivu.
 
Kama unashauriwa na failures unaanzaje kuwa na akili na hao failures wewe ndio unaona vipaaanga, ndiomaana wakati mwingine udikteta unahitajika , ita wasomi ita wachumi wakushauri ikifika miezi miwili hakuna mabadiliko piga risasi wote watakaokuja tena watakua na mawazo yenye akili, China hawajaendelea kwa bahati mbaya wanafanya kazi na masihara ni msamiati kule hakuna unakula kitanzi tu, eti PHD nyoooo za Kwiyoo
 
Jamani huyu TULIPIGWA. Hapa tulijua kupotea.
 
Uchumi unaweza kufa hata mara milioni.

Uchumi una tabia ya kufa mara nyingi na kufufuka mara nyingi pia ukifufuliwa.
Kumbe! Magufuli aliua uchumi hadi March 17 alipofariki. Mama akrithi tarehe 17 hiyo hiyo hadi leo takribani miezi 6 tu, haijazidi hapo. Bila shaka huo uchumi uliokuwa umeuliwa na Magufuli ulifufuka kwa sekunde chache sana akaja kuuua Samia tena.
 
Nahisi Kuna kuharibiana!
Halafu anae haribiwa hajagundua
 
Sidhani kama kuna ulazima wa kushauriwa katika hili hapa ni yeye mwenyewe akumbuke malalamiko ya wananchi kuhusu tozo hizi.

Hapa ni common sense tu itumike vinginevyo waacheni watuburuze kwa kodi dhalimu halafu tuwe kama Zimbabwe.
Common sense is not common to all .. Remember that πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…