Sir robby
JF-Expert Member
- Jun 22, 2022
- 2,400
- 4,073
Najua mpo chawa wa rais Samia na chawa wa rais Magufuli lakini, Rais Samia anaijua siasa kuliko rais Magufuli kwa kiwango kikubwa. Moja ya uthibitisho huo ni:-
1.Kuamua kufanya maridhiano na chama kikubwa cha upinzani chenye wafuasi wengi ambacho ni CHADEMA jambo ambalo rais Magufuli aliamini adui mkubwa na hatari kwa utawala wake ni CHADEMA hivyo kufanya nao maridhiano sio sahihi licha ya kuambiwa na kuombwa na mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe wakiwa Mwanza.
Mwanasiasa anayejua siasa na anayetaka kutawala kwa amani lazima ahakikishe ugomvi na adui yake unaepukika na hilo ndilo alilolifanya rais Samia
Rais Magufuli aliongeza chuki kwa CHADEMA kwa kuvuruga chaguzi
Kununua wabunge na madiwani wa CHADEMA akiamini ataiua CHADEMA ili atawale bila upinzani
Kuzuia mikutano ya hadhara akiamini CHADEMA hawataongea na wananchi kuwakamata viongozi wanachama na wafuasi wa CHADEMA na kuwabambikizia kesi na hata kuwafunga.
Leo rais Samia kupitia DPP wake anaziondoa kesi za kugushi na watuhumiwa wanatolewa magerezani
Rais Samia katimiza hitaji ya kikatiba kuruhusu mikutano ya vyama
Hakika rais Samia anajua siasa kuliko rais Magufuli.
Anayepinga apinge kwa hoja sio mihemuko..
1.Kuamua kufanya maridhiano na chama kikubwa cha upinzani chenye wafuasi wengi ambacho ni CHADEMA jambo ambalo rais Magufuli aliamini adui mkubwa na hatari kwa utawala wake ni CHADEMA hivyo kufanya nao maridhiano sio sahihi licha ya kuambiwa na kuombwa na mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe wakiwa Mwanza.
Mwanasiasa anayejua siasa na anayetaka kutawala kwa amani lazima ahakikishe ugomvi na adui yake unaepukika na hilo ndilo alilolifanya rais Samia
Rais Magufuli aliongeza chuki kwa CHADEMA kwa kuvuruga chaguzi
Kununua wabunge na madiwani wa CHADEMA akiamini ataiua CHADEMA ili atawale bila upinzani
Kuzuia mikutano ya hadhara akiamini CHADEMA hawataongea na wananchi kuwakamata viongozi wanachama na wafuasi wa CHADEMA na kuwabambikizia kesi na hata kuwafunga.
Leo rais Samia kupitia DPP wake anaziondoa kesi za kugushi na watuhumiwa wanatolewa magerezani
Rais Samia katimiza hitaji ya kikatiba kuruhusu mikutano ya vyama
Hakika rais Samia anajua siasa kuliko rais Magufuli.
Anayepinga apinge kwa hoja sio mihemuko..