Rais Samia ana uchu wa maendeleo

Rais Samia ana uchu wa maendeleo

Nyabukika

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2022
Posts
1,441
Reaction score
1,049
Leo ni ile siku tuliyokua tunaisubiri kwa hamu kujua matokeo ya sensa kwa maendeleo ya jamii matokeo haya ya sensa yametoka mapema zaidi ukilinganisha na miaka mingine kwasababu ya kutumia mfumo wa kidigitali na uchu wa maendeleo alionao Rais Samia Suluhu.

Rais Samia Suluhu amesema kua Tanzania ina idadi ya watu milioni 61.741. kati yao wanawake ni milioni 31.6 sawa na asilimia 51 na wanaume milioni 30.53 sawa na asilimia 49 ya watu wote amesema kua jiji la Dar es salaam lina idadi kubwa ya watu amabao ni 5,383,728 (8.7% ya Watanzania wote) ikifuatiwa na Mwanza idadi ya watu ni 3,699,872 (6% ya Watanzania wote).

Kutokana na idadi hii ya watu kila mkoa, wilaya vijiji na vitongoji namanisha kila sehemu ya Tanzania itapata maendeleo kulingana na idadi ya watu na Rais Samia Suluhu ameahidi kupeleka maendeleo endelevu kila sehemu ikiwemo huduma za kijamii.
 
Kwa katiba hii kupata maendeleo ayatakayo ni vigumu sana ajiulize wengine walishindwaje kupata maendeleo?
 
Ndoto za mchana au kimpumu cha mchana ni shida
Husababisha tupo na watu wa aina hii
au shida ni nini?
 
Mama kanyaga twende tumecheleweshwa mnooo kama taifa. Piga kazi
Nakuunga mkono. Nani kama mama. Hafokifoki hana wenge lakini mambo yanaenda smoothly as planned.

Utawala huu unatukosha. Kuna utu atuishi kama digidigi.
 
KWA KATIBA HII KUPATA MAENDELEO AYATAKAYO NI VIGUMU SANA AJIULIZE WENGINE WALISHINDWAJE KUPATA MAENDELEO?
Maendeleo ni wewe mwenyewe. Mama kashakuwekea mazingira rafiki. Sasa hhakuna kutishwa tishwa, kuibiwa mke, kuibiwa hela na mali.

Hakuna kitu kizuri kutafuta hela ukiwa na amani na faraja ya moyo na akili. Hata kama uchumi wa dunia unasuasua lakini that peaceof mind .

Mama hadi 2030 na kuendelea hadi achoke

Cc Crimea
 
Maendeleo ni wewe mwenyewe. Mama kashakuwekea mazingira rafiki. Sasa hhakuna kutishwa tishwa, kuibiwa mke, kuibiwa hela na mali. Hakuna kitu kizuri kutafuta hela ukiwa na amani na faraja ya moyo na akili. Hata kama uchumi wa dunia unasuasua lakini that peaceof mind .

Mama hadi 2030 na kuendelea hadi achoke
Hakuna cha Maendeleo ya Nchi labda ya kila Mtu ajitafutie mwenyewe
 
Bado tunao wajinga wapatao milioni ngapi nchini ukiwemo na wewe mleta mada hii jinga!
 
Hakuna cha Maendeleo ya Nchi labda ya kila Mtu ajitafutie mwenyewe
Maendeleo ya nchi kwa ujumla yapo na yataendelea kutekelezwa kama kuendelea na ujenzi wa vituo vya afya, Shule pia miundombinu kulingana na idadi ya watu.

Maendeleo ya mmoja mmoja ni kama kupata mikopo yenye masharti nafuu Rais Samia Suluhu anaendelea kuleta maendeleo endelevu We are so proud of her
 
Maendeleo ni wewe mwenyewe. Mama kashakuwekea mazingira rafiki. Sasa hhakuna kutishwa tishwa, kuibiwa mke, kuibiwa hela na mali. Hakuna kitu kizuri kutafuta hela ukiwa na amani na faraja ya moyo na akili. Hata kama uchumi wa dunia unasuasua lakini that peaceof mind .

Mama hadi 2030 na kuendelea hadi achoke
Exactly umenena vyema Rais Samia Suluhu anakufungulia milango ya maendeleo na sio kukujengea nyumba au kukupa chakula mkononi watu hawaelewi kabisa
 
Nakuunga mkono. Nani kama mama. Hafokifoki hana wenge lakini mambo yanaenda smoothly as planned.

Utawala huu unatukosha. Kuna utu atuishi kama digidigi.
Moja ya kitu wanajivunia ccm, ni takataka aina yako
 
Nakuunga mkono. Nani kama mama. Hafokifoki hana wenge lakini mambo yanaenda smoothly as planned.

Utawala huu unatukosha. Kuna utu atuishi kama digidigi.
Sure Rais Samia Suluhu anaiendesha Tanzania kwa akili sana hana papala na maendeleo tunayaona
 
KWA KATIBA HII KUPATA MAENDELEO AYATAKAYO NI VIGUMU SANA AJIULIZE WENGINE WALISHINDWAJE KUPATA MAENDELEO?
Maendeleo ni lazima mzee maana mpaka sasa toka Rais Samia Suluhu aingie madarakani maendeleo yanaonekana
 
Ndoto za mchana au kimpumu cha mchana ni shida
Husababisha tupo na watu wa aina hii
au shida ni nini?
Shida ni wewe unaejua Rais Samia Suluhu ameleta maendeleo mengi hasa katika sekta zinazokulenga direcy wewe mtanzania na bado unataka kupinga
 
Mama ni mtaaluma kwenye mahesabu. Najua kama siyo kukwamishwa na walamba Asali basi tungekuwa mbali sana

Tusiache kumuombea lakini akiendelea kuamini anachodanganywa basi anguko ni kama jiwe kwenye maji
 
Back
Top Bottom