GE2025 Rais Samia ampongeza Rais mteule wa Malawi Prof. Arthur Peter Mutharika

GE2025 Rais Samia ampongeza Rais mteule wa Malawi Prof. Arthur Peter Mutharika

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Wont be the same

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
1,572
Reaction score
2,495
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dkt. Samia Suluhu Hassan amempongeza, Prof. Arthur Peter Mutharika wa Chama cha DPP, Rais Mteule wa Jamhuri ya Malawi, kwa ushindi wake katika uchaguzi mkuu wa Malawi wa mwaka 2025.

Rais Dkt. Samia ametoa pongezi hizo kupitia mtandao wake wa kijamii wa Instagram ambapo pia amempongeza Rais anayemaliza muda wake, Dkt. Lazarus Chakwera wa Chama cha Malawi Congress Party (MCP) na watu wa Malawi, kwa uchaguzi wa amani.

Soma Pia >> UCHAGUZI MKUU MALAWI: Rais wa zamani Peter Mutharika (85), ashinda kwa kishindo kwa kura asilimia 57%

"Kwa niaba ya Serikali na wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, natoa pongezi zangu za dhati kwa Mheshimiwa Profesa Arthur Peter Mutharika, Rais Mteule wa Jamhuri ya Malawi, kwa ushindi wake katika uchaguzi Mkuu wa Malawi wa mwaka 2025...ninampongeza Mheshimiwa Rais Dk. Lazarus Chakwera, Chama cha Malawi Congress Party (MCP) na watu wa Malawi, kwa uchaguzi wa amani"-Rais Dk Samia Suluhu
 

Mapito ya Safari ya Peter Mutharika kwenye taaluma na maisha ya kukazimishwa kwenda uhamishoni Tanzania


Maisha ya Awali na Elimu


Peter Mutharika alisomea sheria katika vyuo vikuu vya juu. Alipata shahada yake ya kwanza ya sheria kutoka Chuo Kikuu Cha London mwaka 1965.

Baadaye, alipata Shahada za Uzamili ya Sheria (LL.M.) na Udaktari wa Sayansi ya Sheria (JSD) kutoka Chuo Kikuu cha Yale mwaka 1966 na 1969.

Baada ya masomo ya sheria ya juu, alikuwa mkimbizi na kuishi nchini Tanzania, Arthur Peter Mutharika alipata cheti cha uwakili kitaaluma nchini Tanzania mwaka 1971.


Akiwa profesa, Mutharika alifundisha sheria katika vyuo vikuu kadhaa ulimwenguni. Hizi ni pamoja na UDSM Chuo Kikuu cha Dar es Salaam nchini Tanzania, Chuo Kikuu cha Haile Selassie nchini Ethiopia, na chuo kikuu cha Rutgerscha Marekani. Pia alifundisha kwa miaka 37 katika Chuo Kikuu cha Washington huko Marekani.

Kujitosa kwenye Siasa za Malawi​


Peter Mutharika alimsaidia kaka yake, Bingu wa Mutharika, wakati wa kampeni zake za kuchaguliwa tena kuwa rais mwaka 2009. Peter Mutharika kisha aliingia katika siasa za Malawi yeye mwenyewe. Alipata kuwa Waziri serikalini na aliendelea kumshauri Rais kuhusu masuala muhimu hadi kifo cha kaka yake mwaka 2012.
 
Baada ya masomo ya sheria ya juu, alikuwa mkimbizi na kuishi nchini Tanzania

Soma kuhusu udikteta wa utawala Ngwazi Dr.Kamuzu Banda rais wa maisha ulivyopelekea raia wa Malawi kukimbilia au kulazimishwa kwenda uhamishoni

 
Anampongeza aliyeshinda bila magumashi, wapi uliona chama tawala kinashindwa? Ccm ijiandae vema kisaikolojia uchaguzi utakaofuata baada ya huu kuondoka madarakani. Iache wananchi wenyewe wajijmulie hatma ya siasa ya nchi yao
 
Soma kuhusu udikteta wa utawala Ngwazi Dr.Kamuzu Banda rais wa maisha ulivyopelekea raia wa Malawi kukimbilia au kulazimishwa kwenda uhamishoni

Siasa za udikteta zilivyomalizwa nchini Malawi :

22 May 2025

Mother and I #4 Masauko Chipembere returns to Tanzania to continue the battle with Kamuzu Banda, 1966...


View: https://m.youtube.com/watch?v=MZU_roqnRTA
Henry Masauko Chipembere returns to Tanzania in 1966 to continue the battle with Kamauzu Banda.

Mai (Mother) Catherine Chipembere gives details on life in Tanzania with Dr. Kamuzu Banda making multiple attempts on Chipembere's life.

Chipembere begins a party in exile with Kanyama Chiume called the Pan African Democratic Party (PDP). Discover the roots of land disputes between Malawi and Tanzania which began in the '60s and continue today Oscar Kambona .... teaching at Kigamboni Ideological College , Kanyama Chiume, Dunduzu Kaluli Chisiza brothers lead invasion into Malawi from Tanzania ... The Malawi Freedom Movement (MAFREMO) was founded in 1977 in Dar es Salaam by Oron Chiewa .. Eduardo Mondlane ...


Dr. Kamuzu Banda
On Nyasa VoiceBox, as discussions about the border dispute between Malawi and Tanzania over Lake Malawi resurface, we reflect on what Ngwazi Dr. Hastings Kamuzu Banda said about the issue. He firmly stated that Lake Malawi belongs entirely to Malawi. He suggested that if the people living along the lakeshore in Tanzania wish to use the lake, Tanzania should cede the Mbeya, Njombe, and Songea (now part of Ruvuma) districts to Malawi instead of claiming half of the lake.

View: https://m.youtube.com/watch?v=lH9g_tEkkRM
 
Historia ndefu ya kudai mabadiliko reforms nchini Malawi, hadi kuwepo uchaguzi huru wa kidemokrasia,

04 June 2024

Mai and I #2 Likoma to Tanzania (Masauko Chipembere's family fleas - Cabinet Crisis )


View: https://m.youtube.com/watch?v=uC9NhiKLiNc
- Catherine Chipembere tells the story of how she fled Malawi fearing for her life as Kamuzu Banda hunted down the Chipemberes.

She made it to Tanzania with the help of Governor and Lady Jones. Henry Masauko Chipembere also fled for America....


PART II the Malawi Cabinet Crisis of 1964
28 April 2024
Mai Catherine Chipembere of Malawi tells the story of how she escaped from Mangochi during the Cabinet Crisis of 1964 with the help of Lady Jones (wife of Governor of Nyasaland) Bishop Arden and his wife Jane...


View: https://m.youtube.com/watch?v=VRt6Il45gno
 
Anampongeza aliyeshinda bila magumashi, wapi uliona chama tawala kinashindwa? Ccm ijiandae vema kisaikolojia uchaguzi utakaofuata baada ya huu kuondoka madarakani. Iache wananchi wenyewe wajijmulie hatma ya siasa ya nchi yao

 
Katika interview hapo juu anadai amefanyiwa Stress Test imeleta majibu moyo wake una afya nzuri kama wa kijana wa miaka 19 (kumi na tisa) na kila siku anafanya mbio za kutembee.
 
Back
Top Bottom