Rais Samia amewafungulia njia wananchi wa Msomera

Rais Samia amewafungulia njia wananchi wa Msomera

Rashda Zunde

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2022
Posts
291
Reaction score
281
Rais Samia Suluhu amewajali sana na kuwathamini wananchi waliohamia Msomera kwa kiasi kikubwa hawakuwahi kufikiria siku moja watakuja kumiliki mashamba makubwa ambayo ni ekari 5, nyumba za kuishi ambazo zina maeneo makubwa ya ekari 2 na nusu na kujengewa miundombinu yote ikiwemo umeme, maji, shule, zahanati na huduma nyingine za kijamii ambazo zipo karibu na makazi yao.

Vitu vyote hivyo hawakuwahi kufikiria katika maisha yao ambapo kwa sasa wana hati miliki ya ardhi wakati Ngorongoro hawakuruhusiwa kujenga nyumba wala kufanya chochote katika eneo la hifadhi.

Rais Samia ana kila sababu ya kupewa pongeze kwa kuweka kuwapa maisha mapya mazuri wananchi hawa, amewafungulia njia amewapa mwanzo mpya na sasa wana maisha mazuri na salama zaidi.
 
Walioleta mifugo kutoka Kenya wachungwe Ngorongoro ,sijui Wana hali gani kwasasa.
 
Hao wamasai kama wangekuwa wanahitaji kujenga nyumba naamini wangeshazijenga miaka mingi iliyopita, hata hizo hati za viwanja nazo kama wangezitaka wangeenda kununua viwanja maeneo mengine wapatiwe hati.
 
Sema serikali mzee. wacha uchawa.
 
Mbona mnawabembeleza hivyo? Wekeni tu mwarabu wenu iko siku tutayavunja makaburi yenu mtueleze ukweli.

Msifikiri mkifa hatutawaadhibu
 
Na wanyantuzu tunaruhusiwa kuhamia huko? Yule laigwani mshenzi alituhamisha ihefu kwa Miguu,
 
Hao wamasai watajua hawajui sasahibi wanabembelezwa hawame..wakimaliza kuhama wnatelekezwa mazima.

#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom