DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo CPA Amos Makalla amesema Mwenyekiti wa chama hicho Rais Samia Suluhu Hassan ameagiza haki kutendeka katika mchakato wa ndani wa chama wa uchujaji wa wagombea.
Akizungumza na wandishi wa habari Julai 03, 2025 katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya CCM Lumumba jijini Dar Es Salaam Makalla amesema “Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kupitia Mwenyekiti wetu wa Chama cha Mapinduzi anaelekeza vikao vyote vitakavyofanya uchujaji na uteuzi viwatendee haki wagombea, tusionee watu, tusitengeneze fitna na majungu, tutende haki, tuteue watu kwa haki, haki ionekane na tusionee mtu.”
Makalla ameongeza kuwa zoezi hilo la uchujaji litaanza rasmia kuanzia kesho Julai 04, 2025 kwa ngazi ya Kata, “Kuanzia kesho tarehe, 04 vikao vya uchujaji vinaanza katika Kata zetu wataanza kukaa kamati za siasa, na kamati za siasa za Mkoa zinatarajiwa kukaa tarehe 09/07 kufanya uteuzi wa mwisho kwa wanaoomba Udiwani. Uwakilishi na Ubunge uteuzi wa mwisho utafanywa na kamati kuu tarehe 19/07 kwa maana ya wagombea watatu watatu.”
Akizungumza na wandishi wa habari Julai 03, 2025 katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya CCM Lumumba jijini Dar Es Salaam Makalla amesema “Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kupitia Mwenyekiti wetu wa Chama cha Mapinduzi anaelekeza vikao vyote vitakavyofanya uchujaji na uteuzi viwatendee haki wagombea, tusionee watu, tusitengeneze fitna na majungu, tutende haki, tuteue watu kwa haki, haki ionekane na tusionee mtu.”
Makalla ameongeza kuwa zoezi hilo la uchujaji litaanza rasmia kuanzia kesho Julai 04, 2025 kwa ngazi ya Kata, “Kuanzia kesho tarehe, 04 vikao vya uchujaji vinaanza katika Kata zetu wataanza kukaa kamati za siasa, na kamati za siasa za Mkoa zinatarajiwa kukaa tarehe 09/07 kufanya uteuzi wa mwisho kwa wanaoomba Udiwani. Uwakilishi na Ubunge uteuzi wa mwisho utafanywa na kamati kuu tarehe 19/07 kwa maana ya wagombea watatu watatu.”