Rais Ramaphosa: Nilipokea vitabu vya Kiswahili, nimejifunza kwa juhudi kubwa. Sasa, kila Jumatatu nazungumza Kiswahili

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,517
Katika kile kinachoonekana kama kueleweka kwa hoja ya Tanzania ya kutumika kwa Kiswahili kama lugha ya nne ya SADC, Rais Cyril Ramaphosa wa Jamhuri ya Afrika ya Kusini amekiri kuwa amepokea vitabu vya Kiswahili, amevisoma na kujifunza vya kutosha na sasa kila Jumatatu anazungumza lugha hiyo.

Akizungumza katika matembezi yake ya eneo la kihistoria la Mazimbu huko Morogoro, Rais Ramaphosa ameonyesha nia ya kukitumia Kiswahili kama lugha rasmi kwa nchi yake na ukanda wote wa SADC. 'Kama unataka kujua kama nazungumza Kiswahili au la, kutana nami siku ya Jumatatu' amesema Rais Ramaphosa.

Katika matembezi hayo, Rais Ramaphosa ameambatana na viongozi mvalimbali wa kiserikali wakiwemo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassimu Majaliwa Majaliwa;Waziri wa Mambo ya Nje Mhe. Prof. P.J.A.M. Kabudi; Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Mhe. Dr. Harrison Mwakyembe na Waziri wa Elimu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako.

Kiujumla, viongozi wa Afrika Kusini na Tanzania wameeleza historia ya kukumbukwa ya eneo hilo la Mazimbu hasa kwenye ukombozi wa Afrika Kusini. Wameahidi kuimarishwa kwa ushirikiano wa kindugu baina ya nchi hizi pendwa mbili huku kukitunzwa historia hiyo ya kuvutia.

Pongezi nyingi kwa viongozi wote wa Serikali yetu ya Tanzania wanaosimamia hoja hii njema ya kuifanya lugha yetu adhimu ya Kiswahili kuwa lugha rasmi katika ukanda wa Kusini kwa Afrika. Siyabonga Tata Ramaphosa!
 
Katika kile kinachoonekana kama kueleweka kwa hoja ya kutumika kwa Kiswahili kama lugha ya nne ya SADC, Rais Cyril Ramaphosa wa Jamhuri ya Afrika ya Kusini amekiri kuwa amepokea vitabu vya Kiswahili, amevisoma na kujifunza vya kutosha na sasa kila Jumatatu anazungumza lugha hiyo.

Akizungumza katika matembezi yake ya eneo la kihistoria la Mazimbu huko Morogoro, Rais Ramaphosa ameonyesha nia ya kukitumia Kiswahili kama lugha rasmi kwa nchi yake na ukanda wote wa SADC. 'Kama unataka kujua kama nazungumza Kiswahili au la, kutana nami siku ya Jumatatu' amesema Rais Ramaphosa.

Katika matembezi hayo, Rais Ramaphosa ameambatana na viongozi mvalimbali wa kiserikali wakiwemo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassimu Majaliwa Majaliwa;Waziri wa Mambo ya Nje Mhe. Prof. P.J.A.M. Kabudi; Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Mhe. Dr. Harrison Mwakyembe na Waziri wa Elimu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako.

Kiujumla, viongozi wa Afrika Kusini na Tanzania wameeleza historia ya kukumbukwa ya eneo hilo la Mazimbu hasa kwenye ukombozi wa Afrika Kusini. Wameahidi kuimarishwa kwa ushirikiano wa kindugu baina ya nchi hizi pendwa mbili huku kukitunzwa historia hiyo ya kuvutia.

Pongezi nyingi kwa viongozi wote wa Serikali yetu ya Tanzania wanaosimamia hoja hii njema ya kuifanya lugha yetu adhimu ya Kiswahili kuwa lugha rasni katika ukanda wa Kusini kwa Afrika. Siyabonga Tata Ramaphosa!
Eventually itakua kama ilivyokuwa kwenye harakati za kuwasaidia wajikomboe kutawaliwa na makaburu!! =====Tulipoteza=====

Hata kwenye kiswahili tunakitumia kuficha kutokujua kwetu lugha zinazotambuliwa na engine zinazoendesha dunia (technology)

Tuendelee kudanganyana na kujifariji.
 
Katika kile kinachoonekana kama kueleweka kwa hoja ya Tanzania ya kutumika kwa Kiswahili kama lugha ya nne ya SADC, Rais Cyril Ramaphosa wa Jamhuri ya Afrika ya Kusini amekiri kuwa amepokea vitabu vya Kiswahili, amevisoma na kujifunza vya kutosha na sasa kila Jumatatu anazungumza lugha hiyo.

Akizungumza katika matembezi yake ya eneo la kihistoria la Mazimbu huko Morogoro, Rais Ramaphosa ameonyesha nia ya kukitumia Kiswahili kama lugha rasmi kwa nchi yake na ukanda wote wa SADC. 'Kama unataka kujua kama nazungumza Kiswahili au la, kutana nami siku ya Jumatatu' amesema Rais Ramaphosa.

Katika matembezi hayo, Rais Ramaphosa ameambatana na viongozi mvalimbali wa kiserikali wakiwemo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassimu Majaliwa Majaliwa;Waziri wa Mambo ya Nje Mhe. Prof. P.J.A.M. Kabudi; Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Mhe. Dr. Harrison Mwakyembe na Waziri wa Elimu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako.

Kiujumla, viongozi wa Afrika Kusini na Tanzania wameeleza historia ya kukumbukwa ya eneo hilo la Mazimbu hasa kwenye ukombozi wa Afrika Kusini. Wameahidi kuimarishwa kwa ushirikiano wa kindugu baina ya nchi hizi pendwa mbili huku kukitunzwa historia hiyo ya kuvutia.

Pongezi nyingi kwa viongozi wote wa Serikali yetu ya Tanzania wanaosimamia hoja hii njema ya kuifanya lugha yetu adhimu ya Kiswahili kuwa lugha rasni katika ukanda wa Kusini kwa Afrika. Siyabonga Tata Ramaphosa!
Sasa Wananchi tunapata faida gani huyu Ramaphosa kuijua lugha ya Kiswahili? Au ndiyo mwanzo wa kutengeneza Fursa ili kupunguza tatizo la ajira nchini kwetu? Au itapunguza umasikini nchini Tanzania ambao unasababisha vifo vinavyoambatana na maumivu makali?
 
Mimi naungana nawewe ndugu Mselwa kupongeza juhudi za tanzania kutilia mkazo wa lugha ya kiswahili kwa nchi za jumuiya ya SADC.

Wasio na ufahamu au uelewa mdogo wanaweza waka kebei lugha yetu hasa watanzania kama kawaida yao kuponda kila kitu.

Ila lazima watanzania wajue, hakuna utanzania bila lugha ya kiswahi. Hakuna umoja, undugu, mshikamano nje ya lugha ya kiswahili.

kiswahili ndio kimetuleta watanzania wote pamoja. Kama waasisi wataifa hili wasinge jua umuhimu wa kuwa na lugha 1 yakutuunganisha kama taifa basi leo kungekua na ukabila, ukanda na utengano.

Embu nenda tanzania nzima kiswahili utakikuta kila maali. Tuache ujinga na kudharau lugha yetu. Kama wenzetu wameona kuna kitu kwenye kiswahili kimelijenga taifa hili na kutulepa 1 kama watanzania. Basi tujivunie lugha yetu.
 
Tunataka Kiswahili kitumike.
Lakini cha ajabu ukienda kuomba KAZI.
Lugha inayotumika ni KIINGEREZA.
na kama haujui hyo lugha kupata KAZI ni ngumu unaonekana kilaza
Hapo mkuu na Mimi ndio naona kama tumelogwa kiingereza kimeisha jeruhi na kinaendelea kujeruhi watu rika mbalimbali badala ya kusahihisha wapi tumekosea ndio kwanza tunaelekeza nguvu kubwa kwenye kiswahili katiba inazitambua lugha hizi kwa usawa mawasiliano ya nje yote kitumike kiingereza na sehemu za kazi ni lugha zote mbili nimemsikiliza waziri wa elimu na hotuba yake huko morogoro mbele ya raisi wa afrika ya kusini japo alikuwa anasoma lakini unaona kabisa acha wajifiche kwenye kiswahili hali ni mbaya.
 
Umeelewa nichoandika?

Mnashabikia kiswahili kwa kuwa kimalkia kinawapiga chenga, kama unabisha sema kwa sauti neno "enterpreneur"
teh...teh...hivyo hivyo! sasa na wewe sema kwa haraka na sauti au mwambie mtoto wako wa darasa la tatu aseme kipikitukikusikitishacho!
 
Petro E. Mselewa ,

..ktk hotuba aliyoitoa Ikulu Raisi Ramaphosa alidokeza kuwa Afrika Kusini ina lugha 11 za taifa ukimjulisha na Kiingereza, hivyo na yeye akamuomba Raisi Magufuli ajifunze lugha 10 za Afrika Kusini.

..kwa statement ile utaona wenzetu wanazichukuliaje juhudi za Tz "kueneza" lugha ya Kiswahili.

..Mwisho, waTz tutakuwa na nafasi nzuri ya kueneza Kiswahili ikiwa tutaongeza juhudi ktk kujifunza lugha za nchi ambazo tunataka wajifunze Kiswahili.
 
Eventually itakua kama ilivyokuwa kwenye harakati za kuwasaidia wajikomboe kutawaliwa na makaburu!! =====Tulipoteza=====

Hata kwenye kiswahili tunakitumia kuficha kutokujua kwetu lugha zinazotambuliwa na engine zinazoendesha dunia (technology)

Tuendelee kudanganyana na kujifariji.
Watakuja ng'ombe wa lumumba kukupa samadi coment yako
 
Petro E. Mselewa ,

..ktk hotuba aliyoitoa Ikulu Raisi Ramaphosa alidokeza kuwa Afrika Kusini ina lugha 11 za taifa ukimjulisha na Kiingereza, hivyo na yeye akamuomba Raisi Magufuli ajifunze lugha 10 za Afrika Kusini.

..kwa statement ile utaona wenzetu wanazichukuliaje juhudi za Tz "kueneza" lugha ya Kiswahili.

..Mwisho, waTz tutakuwa na nafasi nzuri ya kueneza Kiswahili ikiwa tutaongeza juhudi ktk kujifunza lugha za nchi ambazo tunataka wajifunze Kiswahili.
Mkuu Joka kuu,hapa sasa ni kimbembe kumbe nao wanajiuliza mbona Hawa unatusukumia kiswahili ngoja na sisi tuwasukumie kikhosa,kizulu au kiafrikan tuhangaike navyo mambo ya ajabu haya.
 
Sasa Wananchi tunapata faida gani huyu Ramaphosa kuijua lugha ya Kiswahili? Au ndiyo mwanzo wa kutengeneza Fursa ili kupunguza tatizo la ajira nchini kwetu? Au itapunguza umasikini nchini Tanzania ambao unasababisha vifo vinavyoambatana na maumivu makali?
Hata tusipoenda mbali tu kujadili hoja ya faida ya kiswahili.

Huoni fahari kuona mtu anayetoka nchi ya mbali kuongea lugha yako.

Raha saana...kuona binadamu asiye mswahili anajivunia uswahili.

Inamaana tume wa -inspire kila lililoletu kaliona zuri.
 
Hakuna wakati mgumu kama kuwasiliana kwa lugha usiyoijua. Kama hawa maraisi watakubali kiswahili kiingizwe kama moja ya lugha za SADC ni kheri.

Watanzania tunajuana kiingereza kinatupiga chenga. Ni hii sio dhambi wala haina maana kutokukijua kiingereza hatuna akili. Kwangu hii ni faida viongozi wetu wataweza kusema kwa mapana.

Na ikishapitishwa ni shurti wageni wetu wataanza kujifunza taaratibu, na kusema ukweli kiswahili kinakua.
 
Tunataka Kiswahili kitumike.
Lakini cha ajabu ukienda kuomba KAZI.
Lugha inayotumika ni KIINGEREZA.
na kama haujui hyo lugha kupata KAZI ni ngumu unaonekana kilaza
Kutumika kwa kiswahili kwenye shughuli za SADC sidhani kama kutatufanya tusijifunze kiingereza. Mbona kilikuwa hakitumiki na kiingereza kinatupiga chenga.

Tusisahau pia kinatumika AU. Kiswahili ni moja ya lugha rasmi za AU.

Sijajua kwanini watu tumekuwa tunaliongelea hasi hili suala.
 
Back
Top Bottom