Rais Mstaafu Mwinyi Mahakamani Kisutu

TRA fuatilieni tujue kama Mwnyi analipa kodi itokanayo na mapato yake ya pango. Isijekuwa tunamlipa pensheni mtu anayedaiwa kodi.
 
Nimesikia kwenye vyombo vya habari kuwa mzee Mwinyi jana alikuwa mahakamani kutoa ushahidi baada ya kuibiwa zaidi ya 30m ikiwa ni pesa ya malipo ya pango kwenye nyumba zake mbili. Mapato ya namna hii hayakatwi withholding tax? Naomba kuelimishwa nijue kama yanalipiwa nifuatilie kujua kama huyu mzee amekuwa akilipa kodi hiyo.
 
Tunataka TRA waje na kauli je mzee mwinyi analipia kodi haya mapato yanayotokana na nyumba anazopangisha asije akawa anakula bila kunawa huku anakuwa mchungu kudai wakati yeye alipi kodi
 
Haya ndo yale mnayoambiwa kuwa viongozi wetu wana miliki mali lakini wanawatumia watu ili kujificha,
 
mkuu ukiondoa kinga yule mgoni anayependa kuchukua wake za watu kila wiki siatakuwa yupo mahakani kweli atapata muda wa kuwatumikia wanainchi?.

Hilo nalo neno mkuu mkuu!! Hakuna cha nini wala nini. Katiba iweke wazi kabisa maadili yanayotakiwa kwa kiongozi wa nchi na wa majimbo. Tunaamini kuwa uongozi mzuri huanzia kwenye familia. Sasa kama familia hiyo kama ni baba au mama ana kuwa kiongozi ni lazima vetting ya kwanza iwe familia, kama amevurunda familia kwa kufungua suruali au kuvua chupi kwa wingi kiongozi huu hafai. Na hii itaondoa kama si kupunguza ule uongozi au cheo anachopewa mtu kwa kutumia underwear!!! Tanzania hii inakosekana sana na ndiyo maana viongozi wetu wengi waandamizi nyumba ndogo kibao na zinalelewa na kodi za wananchi badala ya kupeleka katika huduma za maendeleo. Ifike wakati tuondokane na tabia hizi chafu za viongozi kuwa na vimada au vidumu.
 
Updates:
Msitakiwa Abdallah Mzombe anayekabiliwa na kesi ya kumuibia Rais wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi Sh.37.44 million, ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa, Rais Mwinyi alimfungulia kesi hiyo ili kukwepa kutimiza ahadi aliyoitoa kwake ya kumjengea nyumba.

Source: Mwananchi, Januari 11, 2013
 
Mzombe aliyaeleza hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi, Gane Dudu wakati akitoa utetezi dhidi ya mashitaka hayo yanayomkabili. Katika kesi hiyo, mshitakiwa Abdallah Mzombe anadaiwa kumwibia Rais huyo wa awamu ya pili, zaidi ya sh 37.44 million baada ya kuaminiwa na kufanywa wakala wa kukusanya kodi za pango la nyumba za Rais Mwinyi


Source: Mwananchi, Januari 11, 2013
 
"ununuzi wa nyumba hizo ulikuwa ni wa siri baina yetu sisi wawili na baada ya kukamilisha ununuzi, walizifanyia matengenezo ya na kuweka wapangaji.

Source: Mwananchi, Januari 11, 2013
 
Mshitakiwa huyo, alitaja miongoni mwa kazi alizokuwa akimfanyia Mwinyi, ikiwamo ya kumtafutia nyumba alizokuwa akitaka kununua eneo la Mikocheni, Msasani na kisha kumkabidhi fedha za kununulia nyumba hizo ambazo zilikuwa ni zaidi ya sh. 300 million.
"vitu vingi vya Mzee Mwinyi tulivifanya kwa siri hata familia yake ilikuwa haijui, nilikuwa na uwezo wa kumuibia feza za ununuzi wa nyumba alipokuwa ananikabidhi lakini sikufanya hivyo". Alidai Mzombe wakati akiendelea kutoa utetezi mahakamani hapo.


Source: Mwananchi, Januari 11, 2013

My take:
Hapo kwenye red/underline pamenishtua wakuu!!!!
 
Samahani kwa kupost vipande lakini nitaweza kuedit baadae:

Mzombe aliyaeleza hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi, Gane Dudu wakati akitoa utetezi dhidi ya mashitaka hayo yanayomkabili. Katika kesi hiyo, mshitakiwa Abdallah Mzombe anadaiwa kumwibia Rais huyo wa awamu ya pili, zaidi ya sh 37.44 million baada ya kuaminiwa na kufanywa wakala wa kukusanya kodi za pango la nyumba za Rais Mwinyi
"ununuzi wa nyumba hizo ulikuwa ni wa siri baina yetu sisi wawili na baada ya kukamilisha ununuzi, walizifanyia matengenezo ya na kuweka wapangaji.
Mshitakiwa huyo, alitaja miongoni mwa kazi alizokuwa akimfanyia Mwinyi, ikiwamo ya kumtafutia nyumba alizokuwa akitaka kununua eneo la Mikocheni, Msasani na kisha kumkabidhi fedha za kununulia nyumba hizo ambazo zilikuwa ni zaidi ya sh. 300 million.
"vitu vingi vya Mzee Mwinyi tulivifanya kwa siri hata familia yake ilikuwa haijui, nilikuwa na uwezo wa kumuibia feza za ununuzi wa nyumba alipokuwa ananikabidhi lakini sikufanya hivyo". Alidai Mzombe wakati akiendelea kutoa utetezi mahakamani hapo.

Source: Mwananchi, Januari 11, 2013

My take:
Hapo kwenye red/underline pamenishtua wakuu!!!!
 
scan copy ya habari yenyewe
mwananchi.jpg
 
Hawa viongozi wetu ambao tumewapa ridhaa ya kutuongoza, ina maana hayo ndo tuliowatuma kwenda kutufanyia? Huyu si ndie alikuwa anajiita MTUKUFU RAIS enzi zake? Ndio maana wanakuwa wakali pale wanapoona WAPINZANI wanapoelekea kuchukua nchi. Kasungura ndo maana hakakui na hakatakua kamwe ndani ya ccm. Ona sasa mambo ya kufanya vitu kwa siri, sasa mambo yote hadharani. Aibu yako mzee Mwinyi.
 
Anatakiwa ajibu hoja kwa nini amemuibia 37Mil sio kutaja biashara zoote walizowahi kufanya,inawezekana huko nyuma alikuwa mwaminifu na sasa amebadilika baada kushikwa masikio na wajanja!
 
Back
Top Bottom