Rais Mstaafu Mwinyi Mahakamani Kisutu

Caren

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2010
Posts
278
Reaction score
91
Nimepewa taarifa na shuhuda kuwa Rais Mwinyi amefuata nyanyo za Rais Mkapa kwa kutinga mahakama ya Kisutu kutoa ushahidi.

Kwa mujibu wa mtoa habari Rais Mwinyi bado yuko Kisutu maana motorcade yake bado inaonekana. Aliye karibu ajongee pale na kutujuza. Hii imefanywa kwa siri na haijatangazwa.

Kesi gani siwezi kuisema kwa sasa.

 

Hakuna maana kama hujui kesi inahusu nini. Leta taarifa iliyokamilika.
 
Twasubiri Dec 2015 ifike maana tutsjua mengi na kuwasubiria sana waende kutoa ushahidi au hata kujibu tuhuma zao nyingi sana kwa wakati huo...usimsahau Mamam nae maana yuko active akiwa mwenyewe 'stand alone'sio chini ya kivuli...cha ngao hapana!nae atasimama kama mjasirimali mchumia tumbo
 
Ungefanya utafiti kidogo kabla ya kusema amefuata nyayo za Mkapa. Unajuaje? Labda kaenda kuweka dole gumba hati ya kuuza shamba.......

Mimi nimetimiza wajibu wangu kwa kutoa taarifa. Sidhani kama nilikuwa na jukumu la kufanyia taarifa hiyo utafiti na ndio maana nimeomba mwenye dukuduku aende pale. Kuhusu kufuata nyayo za Mkapa hilo ndio focus yangu maana inacreate precedents (hasa kwa sisi wanasheria). Huko mbele ya safari hakuna rais mstaafu atayeshindwa kuja mahakamni kutoa ushahidi kama hawa wawili wamekuja including mjomba.
 

Taarifa gani umetoa hapa? Nani ana haja ya kujua gari la Mwinyi limepaki wapi? Watu wanataka kujua anafanya nini au anasema nini kinachohusiana na wananchi. Ndio maana ulipaswa kufuatilia habari kamili ili uweke taarifa iliyoshiba
 
Of course hizo no precedents tosha kabisa. Sisi tunamsubiri mjomba atueleze habari ya Richmund at al akiwa ndani ya kibanda cha watuhumiwa
 
Asante mkuu watu wengine wanakimbilia kutoa habari huku hawajui kinachoendelea
Hakuna maana kama hujui kesi inahusu nini. Leta taarifa iliyokamilika.
 
Nani kakwambia atasimama mahakamani?..2015 anahamia kwa Bush na sidhani kama Republican wakishika dola ya USA watamtoa ashitakiwe..Hujui watamlinda
 
Mleta mada, bado mpaka muda huu hujapata taarifa kamili utujuze???
 
Katiba mpya ifute immune kwa Rais!!! Akivurunda tu akiwa madarakani basi akione cha moto. Hii itasaidia kulinda heshima ya nchi pale Rais anapotumia Ikulu kifalme na kujipatia utajiri wa kisiasa na mali!!!!!
 
Waacheni waanza kupata uzoefu na vile vilinge maana soon very soon wataanza kuvikabili.
 
kutoa ushaidi kwenye kesi ya lulu? mbona habari iko nusu nusu
 
Rais Mwinyi alimkabidhi mtu mmoja nyumba zake mbili awe anazitunza na kukusanya kodi. Badala ya ile kodi kuiwasilisha mwa mwenye nyumba, huyo mtu akazitafuna, Ndipo Mwinyi kaenda polisi na polisi wakafungua kaesi ya madai dhidi ya huyo mshtakiwa (note: bado sijalipata jila la mshtakiwa)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…