Twilumba
Platinum Member
- Dec 5, 2010
- 13,468
- 16,168
Mama najua unapitapita kwenye mitandao ya kijamii direct au indirect.
Kwa siku hizi 18 ulizokaa kwenye hicho kiti kwa kweli umeleta nuru kwenye sura za watanzania walio wengi ukiacha wale Kenge walio kwenye msafara wa Mamba.
Pamoja na kauli nzuri za matumaini mpya nadhani Mama hujatamka chochote kuhusu Bunge letu kuoneshwa LIVE kama hapo awali ikiwa ni kwa lengo la wananchi kufuatilia mijadala mbalimbali inayoendeshwa na muhimili huo muhimu.
Nikuombe Mama hebu tamka waziwazi kuwa sasa Bunge lioneshwe LIVE katika session zake kama ilivyokuwa awali. Jambo hilo litakuwa kimekata kiu kavu na sugu waliyonayo watanzania walio wengi.
Najua wapo baadhi ya uliowaamini hasa wale uliowarithi kutoka utawala uliopita ambao kwa hakika bado wanashindwa kwenda na tune zako na hivyo kuonesha kukumwamisha kwa makusudi, mfano ni Dr. Abbas ambaye amenukuliwa na vyombo vya habari kuwa eti umesema vyombo ulivyoamuru vifunguliwe ni online TV peke yake.
Hii ni dharau kwa Mamlaka na kutaka kukugombanisha na wananchi wako, Mama mkanye aache mara moja. Afanye vile umemweleza bila kuanza kuleta ujuaji mwingine na urasimu usio na msingi.
Kila mtu amesikia LIVE umesema vyombo vya habari vifunguliwe lkn vifuate sheria, kanuni na taratibu, Dkt. Abbas anaanza ku-itemize kwamba ni Online TV pekee ndo ume?ungumzia, jamani ametoa wapi ujasiri wa kuiamulia mamlaka yako?
Mkanye mapema huyu Abbas ili utakaporuhusu kuonesha Bunge LIVE asitokee mwingine aseme Bunge lioneshwe specifically session fulani.
Kazi iendelee!!!
Kwa siku hizi 18 ulizokaa kwenye hicho kiti kwa kweli umeleta nuru kwenye sura za watanzania walio wengi ukiacha wale Kenge walio kwenye msafara wa Mamba.
Pamoja na kauli nzuri za matumaini mpya nadhani Mama hujatamka chochote kuhusu Bunge letu kuoneshwa LIVE kama hapo awali ikiwa ni kwa lengo la wananchi kufuatilia mijadala mbalimbali inayoendeshwa na muhimili huo muhimu.
Nikuombe Mama hebu tamka waziwazi kuwa sasa Bunge lioneshwe LIVE katika session zake kama ilivyokuwa awali. Jambo hilo litakuwa kimekata kiu kavu na sugu waliyonayo watanzania walio wengi.
Najua wapo baadhi ya uliowaamini hasa wale uliowarithi kutoka utawala uliopita ambao kwa hakika bado wanashindwa kwenda na tune zako na hivyo kuonesha kukumwamisha kwa makusudi, mfano ni Dr. Abbas ambaye amenukuliwa na vyombo vya habari kuwa eti umesema vyombo ulivyoamuru vifunguliwe ni online TV peke yake.
Hii ni dharau kwa Mamlaka na kutaka kukugombanisha na wananchi wako, Mama mkanye aache mara moja. Afanye vile umemweleza bila kuanza kuleta ujuaji mwingine na urasimu usio na msingi.
Kila mtu amesikia LIVE umesema vyombo vya habari vifunguliwe lkn vifuate sheria, kanuni na taratibu, Dkt. Abbas anaanza ku-itemize kwamba ni Online TV pekee ndo ume?ungumzia, jamani ametoa wapi ujasiri wa kuiamulia mamlaka yako?
Mkanye mapema huyu Abbas ili utakaporuhusu kuonesha Bunge LIVE asitokee mwingine aseme Bunge lioneshwe specifically session fulani.
Kazi iendelee!!!