‪Rais Magufuli: Viongozi wa dini mnivumilie kwakuwa fedha zitaendelea kupotea hata kanisani...‬

jsenyinah

JF-Expert Member
Jan 25, 2012
249
338
RAIS AWASILI BUKOBA: Rais John Magufuli amewasili mjini Bukoba kuwatembelea wananchi waliopata maafa ya tetemeko la ardhi mwaka jana.

-------

IMG_2167.JPG


Hatimaye Rais John Magufuli amewasili mjini Bukoba na kushiriki misa ya kufungua mwaka mpya 2017 katika Kanisa la Kuu Katoliki mjini Bukoba.

Katika misa hiyo iliyoongozwa na Askofu wa Jimbo la Bukoba, Mhashamu Desderius Rwoma, Dk Magufuli amewataka viongozi wa dini wamvumilie kwa kuwa fedha zitaendelea kupotea hata kanisani.

3.jpg


Amesema zamani zilikuwepo fedha za hovyo hovyo na sasa anachotaka ni kila mtu aendelee kula anachostahili.

Amesema uchumi wa nchi unaendelea kuimarika na Serikali imedhibiti mfumuko wa bei.

Akiwa Kagera, Rais Magufuli atapata fursa ya kuwasalimia wananchi waliopata maafa ya tetemeko la ardhi Septemba mwaka jana.
 
Ila vitu vingine bwana. Au alienda kutambika kwanza!!! Seriously mnaandika kabisa kaenda kuwajulia hali waliokumbwa na tetemeko!! Watanzania nasi tuna maajabu makubwa
 
Rais wetu anaenda kwa ratiba Safari hii ameamua kutembelea wahanga wote kaanzia chato kukikowzuluwa nyumba na mvua ya upepo na sasa yuko bukoba kwa waathirika wa tetemeko na baadae ataenda mpanda kulikoezuliwa nyumba baadae anaweza kwenda kilosa kunakotokea mauaji wakulima na wafugaji!
 
Ila vitu vingine bwana. Au alienda kutambika kwanza!!! Seriously mnaandika kabisa kaenda kuwajulia hali waliokumbwa na tetemeko!! Watanzania nasi tuna maajabu makubwa
Mkuu hapa hata mm nashangaa, mm nadhani anashida zake tu binafsi
 
Back
Top Bottom