Abdul Nondo
JF-Expert Member
- Oct 28, 2016
- 515
- 2,874
Uwanja wa Ndege wa sasa wa Bukoba ulivyo ni uwanja hatarishi sana na hii ndege ya @precisionairtz kupata ajali ni ndege ya 4 . Zingine zimewahi pata ajali kwenye mawe kutokana na ufinyu wa uwanja. Huu uwanja rasmi ulijengwa 1940 na serikali ya Uingereza kipindi cha ukoloni wakati wa vita ya pili ya Dunia. Baada ya kupata Uhuru ulikuwa unafanyiwa fanyiwa marekebisho .
Wabunge wa Kagera huko Bukoba waliendelea kupaza sauti zao Mama Seveline Mwijage aliyekuwa Mbunge wa CUF Viti Maalumu Sasa ni mwanachama wa ACT wazalendo na mjumbe wa kamati kuu,Masilingi akiwa Mbunge wa CCM Muleba Kusini, Wilfred Lwakatare akiwa Mbunge wa Chadema Bukoba Mjini na Prof. Annna Tibaijuka wamekuwa wakishinikiza uwanja mwingine kujengwa huo wa Bukoba haufai kwani ni uwanja hatarishi.
Serikali ya awamu ya 4 chini ya kikwete ikaweka suala la uwanja wa ndege wa Omukajunguti katika ilani ya CCM uchaguzi wa 2010.Mwaka 2013 tar 26 Jakaya Kikwete akafanya ziara Bukoba ,akatamka "Ujenzi wa Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kajunguti kuanza rasmi" na kuweka jiwe la msingi. Wakati ule Waziri wa Ujenzi akiwa Harrison Mwakyembe, Mwakyembe akawaambia mamlaka ya viwanja vya ndege (TAA) wafanye haraka kulipa fidia watu wahame uwanja ujengwe.
Uwanja wa Kajunguti design yake ulikuwa ni kama uwanja wa Japani wa Kansai International airport (KIX), ulikuwa pia uhudumie nchi jirani Rwanda, Burundi na Uganda.
Hadi serikali ya Kikwete inatoka madarakani 2015 ilikuwa tayari imeandaa fedha za fidia takribani Bil.9 za awali zilikuwa tayari zipo ,Mkandarasi aliyejenga JKN Airport, Mwanza Airport ndiye alikuwa ajenge uwanja wa ndege wa Omukajunguti, upimaji ulikuwa unaendelea ili Ujenzi uwanze.
Serikali ya awamu ya 5 ilivyoingia madarakani tuu ikapiga STOP Ujenzi wa uwanja wa Omukajunguti,tar 6,Nov 2017,Rais wa awamu ya tano akaamuru fedha zote za fidia TSH Bil.9 ziende kufanya upanuzi wa Uwanja huu wa Bukoba,akisema Ujenzi wa uwanja wa Omukajunguti haukuwa kwenye mpango wake . Hivyo mradi wa Omukajunguti Airport huko Misenyi ukajifia kifo cha Mende
Huu ni wakati sasa Mh. Rais Samia Mwigulu Nchemba kusaidia mradi wa ujenzi wa uwanja wa ndege.
Omukajunguti kuendelea ili kuepusha maafa zaidi.
Wabunge wa Kagera huko Bukoba waliendelea kupaza sauti zao Mama Seveline Mwijage aliyekuwa Mbunge wa CUF Viti Maalumu Sasa ni mwanachama wa ACT wazalendo na mjumbe wa kamati kuu,Masilingi akiwa Mbunge wa CCM Muleba Kusini, Wilfred Lwakatare akiwa Mbunge wa Chadema Bukoba Mjini na Prof. Annna Tibaijuka wamekuwa wakishinikiza uwanja mwingine kujengwa huo wa Bukoba haufai kwani ni uwanja hatarishi.
Serikali ya awamu ya 4 chini ya kikwete ikaweka suala la uwanja wa ndege wa Omukajunguti katika ilani ya CCM uchaguzi wa 2010.Mwaka 2013 tar 26 Jakaya Kikwete akafanya ziara Bukoba ,akatamka "Ujenzi wa Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kajunguti kuanza rasmi" na kuweka jiwe la msingi. Wakati ule Waziri wa Ujenzi akiwa Harrison Mwakyembe, Mwakyembe akawaambia mamlaka ya viwanja vya ndege (TAA) wafanye haraka kulipa fidia watu wahame uwanja ujengwe.
Uwanja wa Kajunguti design yake ulikuwa ni kama uwanja wa Japani wa Kansai International airport (KIX), ulikuwa pia uhudumie nchi jirani Rwanda, Burundi na Uganda.
Hadi serikali ya Kikwete inatoka madarakani 2015 ilikuwa tayari imeandaa fedha za fidia takribani Bil.9 za awali zilikuwa tayari zipo ,Mkandarasi aliyejenga JKN Airport, Mwanza Airport ndiye alikuwa ajenge uwanja wa ndege wa Omukajunguti, upimaji ulikuwa unaendelea ili Ujenzi uwanze.
Serikali ya awamu ya 5 ilivyoingia madarakani tuu ikapiga STOP Ujenzi wa uwanja wa Omukajunguti,tar 6,Nov 2017,Rais wa awamu ya tano akaamuru fedha zote za fidia TSH Bil.9 ziende kufanya upanuzi wa Uwanja huu wa Bukoba,akisema Ujenzi wa uwanja wa Omukajunguti haukuwa kwenye mpango wake . Hivyo mradi wa Omukajunguti Airport huko Misenyi ukajifia kifo cha Mende
Huu ni wakati sasa Mh. Rais Samia Mwigulu Nchemba kusaidia mradi wa ujenzi wa uwanja wa ndege.
Omukajunguti kuendelea ili kuepusha maafa zaidi.