Ndiyo. Ni demokrasia.
Demokrasia zipo za aina tofauti.
Aina ya demokrasia ya Marekani kwenye kiwango cha serikali ya shirikisho ni demokrasia ya uwakilishi [representative democracy].
Hakuna demokrasia ya moja kwa moja [direct democracy] kwenye uchaguzi wa Rais wa Marekani.
Lakini pia, kwenye nchi nyingi tu za kidemokrasia, kwenye chaguzi zao hususan za viongozi wakuu wa serikali, huwa hakuna demokrasia ya moja kwa moja.
Mfano, Uingereza huwa hawapigi kura kumchagua waziri mkuu wao. India vivyo hivyo. Israel pia.
Hata Afrika Kusini huwa hawampigii kura rais wao moja kwa moja.
Wamarekani, licha ya kwamba wanampigia kura rais wao moja kwa moja, ushindi wake huamuliwa ki majimbo na idadi ya wawakilishi ataopata kutoka majimboni ambao baadaye wawakilishi hao ndo watapiga kura zao za kuuthibitisha ushindi wake.
Hiyo nayo ni demokrasia.