My Son drink water
JF-Expert Member
- Nov 30, 2016
- 4,932
- 13,283
Uliwaita watendaji wa Kata Ikulu na kuwapa maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za mitaa, kwamba wakikishe Chama tawala kinapata favor zote za ushindi.
Hivi umeshawaza kuwa maisha hubadilika? Leo wewe ni Rais, kuna siku hutakuwa Rais na hawahawa wapinzani unaowachukia ndio watakuwa wanaongoza nchi huku ukishuhudia kwa macho yako.
Kwa nafasi yako ya ukuu wa nchi watendaji wa Kata hawakuwa na hadhi ya kuonana nawe Ikulu.
Uliamua kuvunja itifaki ili tu CCM ipate ushindi feki.
Vyama mamluki vya upinzani vilivyopandikizwa na System vijifanye eti ni vyama vya upinzani na vinashiriki Uchaguzi, mataifa makubwa yanajua ukweli wote juu ya hiyo ghiliba.
Kila siku unataka tukuombee kwa Mungu ila Mungu hana chuki na wapinzani Kama uliyonayo wewe.
Mungu anawapenda wana CCM wote na wapinzani wote,na ndo huyu huyu Mungu atakuja kuwawezesha waingie Ikulu na kuongoza Tanzania huku wote mkiona.
Kwa akili za kibinadamu haiwezekani, ila kwa Mungu inawezekana.
Hata makaburu wa South Africa hawakuwahi kufikiria kuwa ANC ya weusi itakuja kuchukua Dola huku wakishuhudia.
Tabia ya Mungu huwa ni kukaa na wanyonge na kuwainua juu kutoka mavumbuni.
Badilika mapema uiandae kesho yako siku ukistaafu uwe kimbilio la wote kwa ushauri wa hekima, na siyo watu wakusambae kwa kuacha alama mbaya.
Hivi umeshawaza kuwa maisha hubadilika? Leo wewe ni Rais, kuna siku hutakuwa Rais na hawahawa wapinzani unaowachukia ndio watakuwa wanaongoza nchi huku ukishuhudia kwa macho yako.
Kwa nafasi yako ya ukuu wa nchi watendaji wa Kata hawakuwa na hadhi ya kuonana nawe Ikulu.
Uliamua kuvunja itifaki ili tu CCM ipate ushindi feki.
Vyama mamluki vya upinzani vilivyopandikizwa na System vijifanye eti ni vyama vya upinzani na vinashiriki Uchaguzi, mataifa makubwa yanajua ukweli wote juu ya hiyo ghiliba.
Kila siku unataka tukuombee kwa Mungu ila Mungu hana chuki na wapinzani Kama uliyonayo wewe.
Mungu anawapenda wana CCM wote na wapinzani wote,na ndo huyu huyu Mungu atakuja kuwawezesha waingie Ikulu na kuongoza Tanzania huku wote mkiona.
Kwa akili za kibinadamu haiwezekani, ila kwa Mungu inawezekana.
Hata makaburu wa South Africa hawakuwahi kufikiria kuwa ANC ya weusi itakuja kuchukua Dola huku wakishuhudia.
Tabia ya Mungu huwa ni kukaa na wanyonge na kuwainua juu kutoka mavumbuni.
Badilika mapema uiandae kesho yako siku ukistaafu uwe kimbilio la wote kwa ushauri wa hekima, na siyo watu wakusambae kwa kuacha alama mbaya.