MWATANI
Member
- Feb 14, 2014
- 45
- 44
Wanabodi nawasalimu kwa heshima kubwa.
Jioni ya leo nimetoa maoni yangu kwenye uzi wa Ng'wamapalala, unaosema '' Kwanini wanahabari wazaliiwa wa maeneo ya Kagera huwasumbua watawala nchini'' Kwenye maoni yangu nikasema wapo baadhi ya waandishi wanatoa hoja zao kwa mantiki na mrengo chanya wa kuisaidia serikali na nikatoa mfano wa kumtaja Deogratius Mutungi.
Sasa nimepata na kujua mengi juu ya mwanahabari huyu na hii ni baada ya kulitaja jina lake humu Jukwaani, Licha ya kuandika makala zenye weledi na kujenga utaifa na maendeleo ya nchi kumbe pia ni miongoni mwa vijana wachache waliomshauri JPM kuchukua fomu kugombea urais.
Aidha nimejulishwa kuwa mwaka 2009 alikutana na JPM wakati ameenda kwa ndugu yake Eng. Severine Mugumisa pale Wizara ya miundo mbinu na ndipo alipomuomba JPM kuchukua fomu wakati ukifika na ndivyo ilivyokuwa kwa JPM kuzingatia ushauri wa Deo na wengine wote waliompa ushauri.
Maswali kwako JPM:
1) Je, unamkumbuka mwana habari huyu?
2) Je, unasoma na kupitia makala zake anazoandika kupitia RAI NGUVU YA HOJA?
3) Je, licha ya kukupa ushauri ambao pengine umechangia kuwa kiongozi wa Taifa hili na kuleta mapinduzi chanya kwa Taifa zima, unajua maswahibu gani Deo anapitia hapo TBC?
Nimeambiwa mengi juu ya mwanahabari huyu ambaye licha ya kukushauri lakini bado anaendelea kutangaza mazuri ya Serikali yako na anapokosoa anakosoa kwa hoja kinyume na wana habari wengine.
Ikikupendeza, mkumbuke hata kwa salamu tu maana ni miongoni mwa wanataaluma wanaoinadi Awamu ya Tano kwa nguvu zao zote.
Jioni ya leo nimetoa maoni yangu kwenye uzi wa Ng'wamapalala, unaosema '' Kwanini wanahabari wazaliiwa wa maeneo ya Kagera huwasumbua watawala nchini'' Kwenye maoni yangu nikasema wapo baadhi ya waandishi wanatoa hoja zao kwa mantiki na mrengo chanya wa kuisaidia serikali na nikatoa mfano wa kumtaja Deogratius Mutungi.
Sasa nimepata na kujua mengi juu ya mwanahabari huyu na hii ni baada ya kulitaja jina lake humu Jukwaani, Licha ya kuandika makala zenye weledi na kujenga utaifa na maendeleo ya nchi kumbe pia ni miongoni mwa vijana wachache waliomshauri JPM kuchukua fomu kugombea urais.
Aidha nimejulishwa kuwa mwaka 2009 alikutana na JPM wakati ameenda kwa ndugu yake Eng. Severine Mugumisa pale Wizara ya miundo mbinu na ndipo alipomuomba JPM kuchukua fomu wakati ukifika na ndivyo ilivyokuwa kwa JPM kuzingatia ushauri wa Deo na wengine wote waliompa ushauri.
Maswali kwako JPM:
1) Je, unamkumbuka mwana habari huyu?
2) Je, unasoma na kupitia makala zake anazoandika kupitia RAI NGUVU YA HOJA?
3) Je, licha ya kukupa ushauri ambao pengine umechangia kuwa kiongozi wa Taifa hili na kuleta mapinduzi chanya kwa Taifa zima, unajua maswahibu gani Deo anapitia hapo TBC?
Nimeambiwa mengi juu ya mwanahabari huyu ambaye licha ya kukushauri lakini bado anaendelea kutangaza mazuri ya Serikali yako na anapokosoa anakosoa kwa hoja kinyume na wana habari wengine.
Ikikupendeza, mkumbuke hata kwa salamu tu maana ni miongoni mwa wanataaluma wanaoinadi Awamu ya Tano kwa nguvu zao zote.