Rais Magufuli na wageni mashuhuri duniani

Rais Magufuli na wageni mashuhuri duniani

Wanaosema hayo yote ni wapinzani uchwara wa nchi hii.
Itabidi kuwe ma oparesheni ya kuzirudisha akili za wanachadema mahali pake, maana waliozichukua wameziacha bila kuziendeleza.
Duh!

Mkuu hiyo operesheni nina wasi wasi kama itapata go ahead kutoka polisi?
 
Sikudhani kuwa msemaji ukweli waweza kuwa na akili za kiwango cha chini kiasi hicho. Wewe unadhani ajapo mgeni Tanzania huwa ni mgeni wa mkulu binafsi au nchi? Bill Gates kaja Tanzania sio kwa sababu Magu ni Rais bali kafuatilia miradi ya foundation yake na ilianza siku nyingi kabla hata huyo mtu wako hajawa na ndoto ya kuwa siku moja watu watakosea na kumpa heshima hiyo.

Hao wengine ni program za kazi zinazowaleta bila kujali ni nani yupo hapo, hata Amin alikuwa anapokea wageni ofisini kwake waliokuwa wanaenda kwa program za kikazi.

Maelezo yako labda ungesema safari kama ile ya Raila kule kwake na kulala siku tatu ndiyo hayo maswali ungeuliza. Pale katembelewa yeye binafsi na sio nchi, Leo hii hata yeye angekuwa yuko Likizo huko kwao bado Bill Gates angeonana na Mama Samia.
Acha kupotosha watu kwa ushabiki maandazi

Safi kwa elimu ndugu.
 
Moja ya sababu ya Tanzania kuwa masikini ni pamoja na "laana" ya kuwa na "uchafu" badala ya "mtoto" . Mauchafu yanaliangamiza hili Taifa. Ni mpaka pale "mauchafu" yatakapotoweka na kuhakikisha hakuna tena kuletwa "uchafu" ndipo tutakuwa salama. Polee
Nadhani unajenga hoja kwa kutumia dhana na imani ambazo hazina ukweli.

Ukiulizwa useme nani aliyetoa ''laana'' kwa Tanzania, huwezi kumtaja na kama utamtaja utakuwa hauna kidhibiti/kielelezo.
 
Kwa hali ilivyo nchini inakuwaje unapata hawa wageni ambao wengine wana madaraka kimataifa huku wengine wakiwa ni matajiri wakubwa duniani.

Sisi ‘’tunataka/tunapenda’’ Tanzania iwe ‘’the skunk of the world’’ halafu wewe unatujibu kwa kupokea kwa siku moja hapo Ikulu ugeni wa watu watatu ambao ni mover and shaker hapa duniani;

1) Katibu Mkuu wa Nchi za Jumuiya ya Madola, Rt Hon Patricia Scotland QC.

2) Naibu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Inmi Patterson

3) Tajiri namba moja duniani, Bill Gates.

Hivi hawa wageni wako hawajui kuwa Tanzania hakuna ‘’Freedom of Speech’’?

Hivi hawa wageni hawajui kama wewe ni ‘’Dikteta Uchwara’’?

Hivi hawa wageni hawajui kuwa ACACIA imezuiwa kusafirisha ‘’mchanga wake’’ wenye makanikia nje ya nchi na kwa misingi hiyo ''amevunja sheria'' za biashara kitaifa na kimataifa? Kwa nini wanakuja kuwekeza pesa zao kwenye utawala ambao hauheshimi Katiba na Sheria?

Ina maana sisi ''tunaopiga kelele'' hawatusikii au wanasikia na kutuona wajinga?

Kwa nini mnatufanyia ‘’vituko’’ vya aina hii?

Rais Magufuli acha Usanii wa kisiasa!

Hata wananchi wa Tanga walipovamia gari yako ili usimame ''tulisema'' ni usanii!

VIDEO: Katibu Mkuu wa Nchi za Jumuiya ya Madola, Rt Hon Patricia Scotland QC alipokutana na Rais Magufuli Ikulu Dar es Salaam.


VIDEO: Naibu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Inmi Patterson alipokutana na Rais Magufuli Ikulu Dar es Salaam.


VIDEO: Bill Gates alipokutana na Rais Magufuli Ikulu Dar es Salaam.


Unajua kubong'oa mkuu....mnashindana na Mzee Mwanakijiji......unabong'oa mpaka utumbo mwembamba unaonekana? Kha!
 
Hao wote ni wapigania fursa!Hawana haja na mambo yenu ya ndani!

Sent using Jamii Forums mobile app
Niliposikia kuanzia sasa hospital zetu zitatumia mifumo ya computer badala ya makaratasi kwa msaada wa bill get hapo ndipo nikajua business is business zikiisha muda wa matumizi mtakazopewa mjiandae kwenda kununua kwake nyingine kwa bei mara mbili

mzee mzima haishiwi maneno
 
Back
Top Bottom