Rais Magufuli na wageni mashuhuri duniani

Rais Magufuli na wageni mashuhuri duniani

Amejitoa ufahamu,yaani ameona hilo ni jambo kubwa na la ajabu!!


Halafu huyo ndio kichwa hapo Lumumba! Lakini bado anadhani ofisi ya Rais ni ya sizonje na kwamba kila aendae pale basi ana huba na sizonje. Anaona ile ni ofisi binafsi na sio ya umma.

Fikra finyu kama zake mkulu mwenyewe anayesema "kama hunipi mkono na mie sisaini pension yako" akiona kuwa anaposaini kitu ni kama vile ni mali yake ya urithi na sio kazi yake ambayo ndiyo analipwa kwa kuifanya.

Ni hasara sana kuwa na watu wenye fikra za kiwango hiki kwa dunia hii ya sasa.
 
Kwa hali ilivyo nchini inakuwaje unapata hawa wageni ambao wengine wana madaraka kimataifa huku wengine wakiwa ni matajiri wakubwa duniani.

Sisi ‘’tunataka/tunapenda’’ Tanzania iwe ‘’the skunk of the world’’ halafu wewe unatujibu kwa kupokea kwa siku moja hapo Ikulu ugeni wa;

1) Katibu Mkuu wa Nchi za Jumuiya ya Madola, Rt Hon Patricia Scotland QC.

2) Naibu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Inmi Patterson

3) Tajiri namba moja duniani, Bill Gates.

Hivi hawa wageni wako hawajui kuwa Tanzania hakuna ‘’Freedom of Speech’’?

Hivi hawa wageni hawajui kama wewe ni ‘’Dikteta Uchwara’’?

Hivi hawa wageni hawajui kuwa ACACIA imezuiwa kusafirisha ‘’mchanga wake’’ wenye makanikia nje ya nchi na kwa misingi hiyo ''umevunja sheria'' za biashara kitaifa na kimataifa? Kwa nini wanakuja kuwekeza pesa zao kwenye utawala ambao hauheshimi Katiba na Sheria?

Ina maana sisi ''tunaopiga kelele'' hawatusikii au wanasikia na kutuona wajinga?

Kwa nini mnatufanyia ‘’vituko’’ vya aina hii?

Rais Magufuli acha Usanii wa kisiasa!

VIDEO: Katibu Mkuu wa Nchi za Jumuiya ya Madola, Rt Hon Patricia Scotland QC alipokutana na Rais Magufuli Ikulu Dar es Salaam.


VIDEO: Naibu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Inmi Patterson alipokutana na Rais Magufuli Ikulu Dar es Salaam.


VIDEO: Bill Gates alipokutana na Rais Magufuli Ikulu Dar es Salaam.
Mwenzako Lisu leo katupilia mbali makaratasi yote ya MIGA na sasa hivi inasemekana kajifungia ndani analia, pamoja na Mch. Msigwa.
 
Pogba ana mihela huyo ana tembea nayo kwny gari ukiomba anakupa

G.O.M.D
 
Tuanze kuandaa viongozi wa Taifa miaka ijayo!! Tusifanye makosa kama haya tena!!!
 
Mleta hoja kuwa na heshima basi kwa Mhe.Rais.Unamuitaje Dikteta Uchwara?Unaweza kutumia lugha nzuri tu ya kumpinga na tukakuelewa.(People tend to resist changes)
 
msemaji ukweli, kwa kweli wewe ni akili ndogo halafu kwa akili yako ndogo unaanzisha mada ambayo lengo lake hata majinga ya Lumumba yanatilia shaka. Kwa akili hizi si ajabu kesho tukasikia umeteuliwa kuwa mkuu wa mkoa nawe ulete misaada ya miguu bandia baada ya polisi wetu kuwavunja miguu wanaodai uhuru wa mawazo. Kwa wenye akili kubwa zaidi yako hii mada imezidi tu kukuanika ulivyo mtupu kichwani...wahi basi Lumumba upate malipo yako.
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Sikudhani kuwa msemaji ukweli waweza kuwa na akili za kiwango cha chini kiasi hicho. Wewe unadhani ajapo mgeni Tanzania huwa ni mgeni wa mkulu binafsi au nchi? Bill Gates kaja Tanzania sio kwa sababu Magu ni Rais bali kafuatilia miradi ya foundation yake na ilianza siku nyingi kabla hata huyo mtu wako hajawa na ndoto ya kuwa siku moja watu watakosea na kumpa heshima hiyo.
Hao wengine ni program za kazi zinazowaleta bila kujali ni nani yupo hapo, hata Amin alikuwa anapokea wageni ofisini kwake waliokuwa wanaenda kwa program za kikazi. Maelezo yako labda ungesema safari kama ile ya Raila kule kwake na kulala siku tatu ndiyo hayo maswali ungeuliza. Pale katembelewa yeye binafsi na sio nchi, Leo hii hata yeye angekuwa yuko Likizo huko kwao bado Bill Gates angeonana na Mama Samia.
Acha kupotosha watu kwa ushabiki maandazi
Nadhani nawe umegundua,kuna watu wanamatatizo binafsi sasa wanataka kutulisha sumu ili tukae boti moja,ni mambo ya ajabu mno...Labda Raisi angetoka kwenye familia yao ndio asingekua na comment

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hali ilivyo nchini inakuwaje unapata hawa wageni ambao wengine wana madaraka kimataifa huku wengine wakiwa ni matajiri wakubwa duniani.

Sisi ‘’tunataka/tunapenda’’ Tanzania iwe ‘’the skunk of the world’’ halafu wewe unatujibu kwa kupokea kwa siku moja hapo Ikulu ugeni wa watu watatu ambao ni mover and shaker;
1) Katibu Mkuu wa Nchi za Jumuiya ya Madola, Rt Hon Patricia Scotland QC.

2) Naibu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Inmi Patterson

3) Tajiri namba moja duniani, Bill Gates.

Hivi hawa wageni wako hawajui kuwa Tanzania hakuna ‘’Freedom of Speech’’?

Hivi hawa wageni hawajui kama wewe ni ‘’Dikteta Uchwara’’?

Hivi hawa wageni hawajui kuwa ACACIA imezuiwa kusafirisha ‘’mchanga wake’’ wenye makanikia nje ya nchi na kwa misingi hiyo ''umevunja sheria'' za biashara kitaifa na kimataifa? Kwa nini wanakuja kuwekeza pesa zao kwenye utawala ambao hauheshimi Katiba na Sheria?

Ina maana sisi ''tunaopiga kelele'' hawatusikii au wanasikia na kutuona wajinga?

Kwa nini mnatufanyia ‘’vituko’’ vya aina hii?

Rais Magufuli acha Usanii wa kisiasa!

Hata wananchi wa Tanga walipovamia gari yako ili usimame ''tulisema'' ni usanii!

VIDEO: Katibu Mkuu wa Nchi za Jumuiya ya Madola, Rt Hon Patricia Scotland QC alipokutana na Rais Magufuli Ikulu Dar es Salaam.


VIDEO: Naibu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Inmi Patterson alipokutana na Rais Magufuli Ikulu Dar es Salaam.


VIDEO: Bill Gates alipokutana na Rais Magufuli Ikulu Dar es Salaam.

Wewe nawe umekuwa Mzee Tupatupa wa Lumumba wa kuandika kinyume.
 
Matajiri wanaoeleweka wanakaribishwa ikulu ; lakini makanjanja wathubutu kukutwa.......................
 
Back
Top Bottom