chabuso
JF-Expert Member
- Feb 18, 2013
- 6,379
- 5,887
Kwa hali ilivyo nchini inakuwaje unapata hawa wageni ambao wengine wana madaraka kimataifa huku wengine wakiwa ni matajiri wakubwa duniani.
Sisi ‘’tunataka/tunapenda’’ Tanzania iwe ‘’the skunk of the world’’ halafu wewe unatujibu kwa kupokea kwa siku moja hapo Ikulu ugeni wa watu watatu ambao ni mover and shaker;
1) Katibu Mkuu wa Nchi za Jumuiya ya Madola, Rt Hon Patricia Scotland QC.
2) Naibu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Inmi Patterson
3) Tajiri namba moja duniani, Bill Gates.
Hivi hawa wageni wako hawajui kuwa Tanzania hakuna ‘’Freedom of Speech’’?
Hivi hawa wageni hawajui kama wewe ni ‘’Dikteta Uchwara’’?
Hivi hawa wageni hawajui kuwa ACACIA imezuiwa kusafirisha ‘’mchanga wake’’ wenye makanikia nje ya nchi na kwa misingi hiyo ''umevunja sheria'' za biashara kitaifa na kimataifa? Kwa nini wanakuja kuwekeza pesa zao kwenye utawala ambao hauheshimi Katiba na Sheria?
Ina maana sisi ''tunaopiga kelele'' hawatusikii au wanasikia na kutuona wajinga?
Kwa nini mnatufanyia ‘’vituko’’ vya aina hii?
Rais Magufuli acha Usanii wa kisiasa!
Hata wananchi wa Tanga walipovamia gari yako ili usimame ''tulisema'' ni usanii!
VIDEO: Katibu Mkuu wa Nchi za Jumuiya ya Madola, Rt Hon Patricia Scotland QC alipokutana na Rais Magufuli Ikulu Dar es Salaam.
VIDEO: Naibu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Inmi Patterson alipokutana na Rais Magufuli Ikulu Dar es Salaam.
VIDEO: Bill Gates alipokutana na Rais Magufuli Ikulu Dar es Salaam.
Kaka wazungu wako ki maslahi zaidi,hata kama watanzania watauana au watakufa njaa mpaka wamalizike wote, wao hawajali kama wanapata maslahi yao,kumbuka huko America,South Amerika na visiwa vya Caribiean kuna makabila hayapo tena duniani,wazungu wamewaua na kuwamaliza wote waliwasaka kama wanyama....
"Divide and Rule" hayo uliyoyasema wazungu wanayajua na kuyafahamu lakini kila tukitengana ni bora kwao wao,tafakari