Asante kwa kuliona hili,sasa naomba utuwekee hapa uwiano
wa waislam na wakristo katika serikali ya mapinduzi Zanzibar.
Kwa kuwa serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania ni
muungano wa Tanzania bara na visiwani,binafsi nadhani
rais Magufuli amefanya hesabu ya jumla ya viongozi wote
wa Zanzibar na Tanzania bara akaamua kutafuta uwiano
kwa kufidia namba ya kule Zanzibar ambako hakuna wakristo.
Maana nijuavyo mimi zanzibar hakuna waziri wala mbunge mkristo
hivi ni kweli zanzibar hakuna wakristo?
Ikumbukwe kuwa mambo ya kiuongozi
katika taifa letu la Tanzania yanatakiwa kuongozwa
na katiba ambayo kimsingi inatakiwa iwatendee haki watu
wote wenye dini na wasio na dini
Nakumbuka mtoa mada, wakati tunajadili katiba mpya
ulikuwa bado hujaijua haki,hivyo uliitetea katiba iliyombioni kupitishwa
kuwa katiba ya taifa hili. Nadhani laiti kama wote
tungepigania kupata katiba ya wananchi,mambo ya kutawaliwa
na mkristo au muislam yasingekuwa na nguvu kwani
kiongozi angeongoza nchi kwa kufuata matakwa ya katiba na wala si dini yake.
Tupiganie kupata katiba bora
mambo ya kuongozwa na wenye dini wenzetu
yataishia kutuvuruga.Kama nakudanganya
angalia list ya waliotolewa majipu,wapo wakristo wapo dini nyinginezo
shetani hana dini yeye anamkumba kila aliye tayari kumtumikia.
Tuunganishe nguvu tupate katiba ya wananchi PERIOD!
Hayo mambo mengine ya dini yangu,dini yangu
yatatuletea aibu bure.