Rais Magufuli na Lissu wakutanishwe

Rais Magufuli na Lissu wakutanishwe

Katika uchambuzi wa kisiasa, nchi imetolewa kutoka ktk udiktekta na kupelekwa ktk ufashisti.

Ufashisti unataka bunge linalotii mamlaka badala ya kuhoji serikali, matajiri wenye viwanda na biashara (National Bourgeoisie) kuunga juhudi, media kuimba na kusifu mamlaka, Miradi mikubwa ya Maendeleo ya Vitu ili watawala kudai hawataki kelele za haki uhuru na demokrasia ili watimize maendeleo ya vitu kwa haraka. Tanzania tayari imetoka ktk udiktekta uchwara na kurushwa ktk ufashisti November 2019 ilianza hatua hiyo na kuhitimishwa October 28 2020.

Hivyo nafasi ya kukutanisha utawala wa kifashisti na wananchi kama Tundu Antipas Lissu, wananchi great-thinkers waliopo Twitter na JamiiForums au katika vyuo vikuu vya wasomi wakutane na watawala walioifikisha nchi ktk utawala wa kifashisti haupo. Maana waumini wa ufashisti huwa hawasikilizi tena sauti mbadala nafasi hiyo ilikuwapo utawala ulipokuwa steji / hatua ya udiktekta-uchwara lakini CCM Mpya na wananchi wasiojua hila ya watawala hawa wamewapaisha madiktekta uchwara kwenda ktk ufashisti wakitumaini mambo yatakuwa mazuri.

Tutegemee kuona kibano zaidi ndani ya CCM Mpya kutafutana uchawi, National Bourgeoisie wenye viwanda / matajiri kukamuliwa zaidi kodi, maadui-maruhani kuibuliwa zaidi ya hawa mabeberu-ruhani, wasaliti-ruhani , wapinzani-ruhani ili utawala uliopo kijaribu kutimiza ahadi walizotoa (ambazo haziwezitimilika) katika hotuba ya Bungeni ktk bunge jipya lililoapishwa November 2020.

Kwa mfano suala la viwanda vya saruji simenti tayari vimeshaanza kusakamwa siyo na wizara ya viwanda bali mkono wa dola kupitia Polisi na wawakilishi wa wateuliwa wa mkuu wa nchi yani wakuu wa mikoa RC. Hizi ni rasharasha maana wenye viwanda hivi watabebeshwa lawama na viwanda vyao kutishiwa kutaifishwa kwa tuhuma za kuhujumu juhudi za mkuu wakati kuna sababu kubwa mfano umeme usiotosha kuendesha viwanda n.k

Pengine miradi mikubwa ya Maendeleo ya Vitu kama SGR Mpya, maDaraja, Stiegler's Gorge ilianzishwa na sementi yote kupelekwa huko kutokana na uzalishaji mdogo wa viwanda vya saruji nchini na sasa taifa limepungukiwa na fedha za kigeni kuagiza saruji hivyo uhaba sasa unaanza kuonekana si tu za fedha za kigeni za korosho bali na uchumi kwa ujumla kuyumbishwa kwa mipango ya kukurupuka.

Bunge jipya la Novemba ambapo wabunge wa CCM Mpya wameteuliwa na mtu mmoja tumeliona limeanza kwa kupiga makofi kila baada ya sentensi chache za Bwana Mkubwa, wateuliwa hawa (hawajachaguliwa na wananchi wala chama cha CCM) hawajiulizi ahadi za miradi mikubwa mipya juu ya anayo tayari ilianzishwa inaweza kumalizika ndani ya mitano mingine au 15 mingine na ndiyo maana waliteuliwa kwa gharama kubwa kwa Taifa kuua demokrasia, uhuru haki ili kisingizio 2025 apewe 15 mingine.
 
Mpasuko gani wewe unaouongelea? Huyo aliyepata kura milioni 2 ndiyo wa kuleta mpasuko ? I mean, chadema imepeta
13% vs > 85% ya CCM, sasa kuna mpasuko gani hapo ? Huo mpasuko upo vichwani mwenu tu labda na akina tundu, ...
Umejaa majigambo mkuu. Watu Million 2 kwako ni takataka?
 
Katika uchambuzi wa kisiasa, nchi imetolewa kutoka ktk udiktekta na kupelekwa ktk ufashisti.

Ufashisti unataka bunge linalotii mamlaka badala ya kuhoji serikali, matajiri wenye viwanda na biashara (National Bourgeoisie) kuunga juhudi, media kuimba na kusifu mamlaka, Miradi mikubwa ya Maendeleo ya Vitu ili watawala kudai hawataki kelele za haki uhuru na demokrasia ili watimize maendeleo ya vitu kwa haraka. Tanzania tayari imeto
Tunayo fursa na sababu ya kuwa taifa Bora kabisaa. Tupendane
 
Hatambui hiyo nafasi na wajibu wake.Anachotambua pekee ni yeye kubaki madarakani kwa 'gharama yoyote'.
Tumuombe aione fursa hiyo. Kwa nafasi yake yeye ndo rate dertimining step kwenye equation za kemia
 
Tumuombe aione fursa hiyo. Kwa nafasi yake yeye ndo rate dertimining step kwenye equation za kemia
Hapo ni kusubiri miujiza itokee mkuu.Tunaposubiri hayo,tupambanie haki katika 'uwanja mwingine'
 
Lissu hatumuhitaji wacha akae hukohuko aende zake..tena mwambie wananchi Wana hasira asiwachokoze kabisa..akomee huko..Hana uwezo wa kushirikiana na Magufuli..mtoto mdogo yulea aendelee kupambana na afya Yake baasi, kiukweli wananchi hawataki kumsikia kabisa Wala kumwona. Sidhani anapendwa anajidanyanya.

Lissu huyu aliyetaka kutuingiza shimoni katika suala la makinikia..loh. Tena asitujaribu, huyu anayeponda kazi zote zilizofanywa na Magufuli leave kutumia Kodi zetu wananchi. Pumbafff kabisa. Haoni jema lolote..yule hafai hata kuwa mwenyekiti wa Kijiji. Labda mwenyekiti wa kitongoji.

Lissu huyu aliyekuwa akimtukana Magu na serikali. Huyuhuyu eti leo sijui Nini maongezi, kwanza Tanzania yetu ina amani na watu wanachapa kazi Kama kawaida. Wameshafunga ukurasa wa siasa. Tuonane 2025
 
Yuko madarakani kwa gharama ya kura za wananchi na sio Wabelgiji!
Kalale,pumzisha tumbo lako lililojaa ugali wa dhuluma ya haki za watanzania.Hutoelewa kamwe vilio vya watanzania.
 
Umejaa majigambo mkuu. Watu Million 2 kwako ni takataka ?

Hawana uwezo wa kuleta mpasuko, kungekuwa na tofauti ya kura kama 10 000 elfu kumi hapo unaweza na ni sawa kuongelea kuhusu mpasuko lkn tofauti ya kura > milioni 10 halafu mnaongelea mpasuko ?
 
Mungu akubariki sana bandiko lako liwafikie wote ulio walenga umeandika maneno adhimu sana na Mungu alitie nguvu
Msimchezee Mungu nyie mafiraunii...maneno adhimu unayajua wewe lakini sio huyo kibaraka wa mabeberu na Amsterdam wake...msifanye wananchi tukaanza kutoa matusi ya nguoni bureeee...he can go to hell Kama mmoja alivyosema
 
Back
Top Bottom