Nampurukano
JF-Expert Member
- Jul 17, 2015
- 1,845
- 2,266
Tangu Mobutu ameondoka madarakani ni miaka 20 sasa. Wamefanya nini cha maana zaidi ya migogoro ambayo haiishi. Natarajia utaniambia machafuko Zaire yameanzishwa na Wazungu pia maana wao kila mahali wanaanzisha machafuko as if sisi waafrika hatuna akili timamu.Mi namsifu Rais magufuli kumsifia Gaddafi alivyoifanya libya.
Maisha yalikuwa shwari libya. Tupa kule propaganda za wazungu. Mwafrika yoyote mpenda nchi yake angetaman nchi yake iwe kama ilivyo kuwa libya. Full misosi japo wapo jangwani. Nyumba na huduma zingine safi sana. Maisha murua. Utake nini zaid!
Kufanikisha hilo alikuwa anawapenda watu wake na alitaka na kuwa na njia za kunyanyua hali za watu wake. Hakuwa na tamaa na ubinafsi
Huduma za afya na Elimu pia shwari zilikuwa
Wazungu wanatufundsha kuwa jamaa alikuwa mwovu. Badala yake wanaona aibu kumsifia mobutu, kipenzi chao. Naamini Zaire ingekuwa kama libya ya Gaddafi kama si hila za wazungu wakimtumia mobutu.
Maendeleo ya Libya hayajaanza zamani sana. Yameanza kipindi Gaddafi ameishika nchi ile
Naamini tuna vitu kama vya libya, na hivyo tukimpata mtu mwenye akili kama ya Gaddafi lazima tufanikiwe
Tatizo Lita kuwa watu wenye mawazo kama ya kwako. Na wabaya wetu hawatopenda maana wanapendelea watu wa kuwatumia kama mobutu
Watanzania wenzetu wanatushambulia na kutuita tusiojua as if wao ni waLibya.Gadafi hajawahi kuwa roll model ya utawala mzuri si kwa africa tu hata huko Libya kwenyewe, mambo yanayofanyika chini ya carpet kwa viongozi kama hao usipime, of course kuna watu wanafaidika na tawala kama hizo na watazisifia sana. Watu wanashindwa kuelewa kwamba aliyesababisha kutoweka kwa amani Libya ni Gadafi mwenyewe wala hakuna mtu mwingine, hata kufa alijisababishia yeye. Bila udikteta wake Gadafi angeweza kuifanya Libya ikawa nchi ya amani na utulivu daima na yeye akaishi kama Farther of the Nation hata baada ya kutoka madarakani.
Bado hatujafikia huko ila Magufuli ndiyo anataka tuelekee hukoUmesema vyema sana.
Sasa maswali ya kujiuliza
1. Tanzania tunatoa Scholarship ?
2. Tanzania tunasaida Africa kulipia Matumizi ya Sattelite ?
3. Raia wa Tanzania tuna Maisha bora kuwazidi watu wengine wote barani Africa ?
Ukijbu haya Maswali utajua kuwa hatupaswi kujifananisha na Libya ya enzi za Gadafi,hatufanani nayo hata Chembe...
Nchi ili iweze kuendelea pasipo shaka lazima udikteta utumike ,,mfn Libya,U.S,Uk,Russia,Israel,Egypt,Cuba,Venezuela na nyingine nyingi tu,udikteta ulitumika.Hivyo basi JPM ana malengo mazuri na Nchi yake
Basi tafuteni mfano mwingineBado hatujafikia huko ila Magufuli ndiyo anataka tuelekee huko
Hahahahahhahha% alizopata Magufuli hadi tunafika 2020 atabakiza 20% tu !!
Pamoja Na dikteta .....!! Nasikia anapenda hadi sera za savimbiHahahahahhahha
Mkuu ACT Mzalendo kitambo sana sijakusikia.
Kwema Mazalendo ???
We Nyani acha uchocheziNi mara kadhaa sasa nimemsikia mtukufu rais Dkt.John Pombe Joseph Magufuli, akiwa anazungumzia suala la amani, akiitolea mfano nchi ya Libya kipindi cha Gadafi.
Kwamba mambo huko Libya yalikuwa safi tu. Vijana waliokuwa wanaoa walipewa hela, nyumba, na mengineyo.
Inawezekana kweli walikuwa wanapewa hivyo vitu lakini je, walikuwa wako huru kiasi gani?
Gadafi alikuwa dikteta. Tena dikteta mkubwa tu aliyeng'ang'ania madaraka kwa muda mrefu sana hadi walipomfurumsha.
Mtukufu rais Magufuli naye watu wengi wameshaanza kumwona kuwa ni dikteta. Hataki watu wafanye siasa kwenye maeneo yasiyo yao.
Tumeshaona na kusikia watu wakikamatwa na kufunguliwa mashitaka kwa makosa ya kumtukana/ kusema maneno mabaya dhidi yake.
Tumeona vyombo vya habari vikifungiwa kwa sababu zisizo na mashiko.
Sasa haya mambo ya yeye kuisifia Libya ya Gadafi mimi yananitatiza.
Nabaki najiuliza maswali tu. Ina maana yeye Magufuli alikuwa anamwona Gadafi kuwa ni kiongozi bora aliyeweza kutunza amani huko Libya hadi awe anaisifia sifia hivyo?
Kama Gadafi ndo mmoja wa viongozi ambao Magufuli anawaona kama mfano mzuri wa utunzaji wa amani, watu wakimwona na yeye dikteta watakuwa wanakosea kweli?
Ndo mambo ya ndege wafananao hayo au..?
Ndugu yangu kesi ya libya na tanzania ni tofauti....kule serikali ya familia ya gadafi na watu hawakuridhika ...nchi ni ya watu wote.Hao uliokaa nao wakakwambia hivyo leo hii kawaulize tena wanaonaje maisha kipindi cha Gadaffi na sasa?
Ni kawaida ya binadamu kuona alicho nacho sio bora akatamani asichokuwa nacho mpaka kile alichokuwa nacho kikimponyoka ndipo huona umuhimu wake.
JK si alitukanwa sana akaitwa dhaifu na wapinzani na watanzania wengi, lakini sasa wanamtamani.
Same applied to Gadaf na Magu muda wake ukiisha atasifiwa.
Hao wanaokaa miaka kumi kumi wanaleta maendeleo ya nchi na wanawajali wananchi wao? mimi nadhani tatizo si kukaa muda mrefu, muhimu ni maendeleo yapatikane na wananchi wasisote, japokuwa hao wanaotetea "demokrasia" hawalikubali hilo. Ila kama kiongozi anakaa miaka mingi halafu hakuna maendeleo, njaa tupu, elimu ni shida, mahospitali hakuna dawa nk. basi hafai na hata kama atakaa miaka kumi tu halafu hamna kitu (kama hapa kwetu wameshabadilisha maraisi mara ngapi?) basi pia huyo kiongozi hafai.tatizo la gadafi nikukaakatika cheokwamudamrefu miyaka 40 simchezo
Nakubaliana naweSawa mkuu vile inategemea uungwana wa viongozi!! wengine wanafikiri wakiwa maamiri jeshi ni kutawala tu kwa mkono wa chuma. Hawa wanaosema waombewe huku wakiwa na roho za visasi ni majanga tu hata ungeweka tume huru!! damu itamwagika kuliko waachie kwa sanduku la kura!!
Nimechukizwa mno na kauli zake huko pemba na ZNZ nina uhakika kuwa huyo muungwana Dr Shein analazimishwa tu dhambi lakini hayuko hivyo!!