Uchaguzi 2020 Rais Magufuli lipa Mafao ya Wastaafu kabla ya Uchaguzi Oktoba 2020

Mzalendo2015

JF-Expert Member
Aug 14, 2012
6,697
9,048
Kulingana na report ya Ukaguzi ya CAG 2019/20 Serikali inadaiwa na Mifuko ya Jamii PSSSF kiasi cha zaidi ya Tshs. 700 Bilioni ambazo Serikali imekopa toka PSSSF na haijarudisha/kulipa fedha hizo.

Kuna Habari za kuaminika kwamba fedha hiyo imekopwa kwenda kujengea miradi mikubwa ya Serikali kama SGR na Stieglers Gorge(Bwawa la Nyerere).

Tunajua Bunge linamaliza muda wake na kuvunjwa June hii,2020. Kwa uhakika Wabunge na Mawaziri wote watalipwa mamia ya mamilioni ya Shilingi baada ya kulitumikia Bunge kwa miaka 5 tu!

Kinachosikitisha kuna wazee Wastaafu wamelitumikia Taifa hili kwa uaminifu na kwa miaka mingi kati ya 25~40 lakini mpaka sasa wengi wao hawajalipwa mafao yao tangu Wastaafu.

Wengine wana miaka 3,2,1 na wengine wana miezi kadhaa. Wazee hawa wanapofika PSSSF hupewa Majibu yaliyojaa visingizio vya uchelewesho wa malipo ya michango toka kwa Waajiriwa au makosa ya ujazaji wa fomu, majina au tarehe za kuzaliwa ilhali Ukweli ni kwamba Mifuko haina Fedha ya kuwalipa wazee hao.

Kama Hali itaendelea kuwa hivo Rais Magufuli ajue kuwa hatopata kura hata moja toka kwa hao wazee Wastaafu pamoja na familia zinazowategemea.

Wazee hao wamepigika sana hasa kipindi hiki cha Covic-19 maana hawana kipato chochote, hawana mishahara, hawana malipo ya pensheni na hawawezi kukopesheka popote.

Chondechonde Rais Magufuli toa maelekezo kwa Hazina ilipe Deni Hilo la PSSSF ili mfuko uwalipe Wastaafu hao wanyonge.
 
Kwanini hawaogopi kutumia pesa za watu kwenye mambo yao bila ridhaa ya wenye nazo, huu ni wizi, wanatumia hizo pesa halafu wanatudanganya sisi ni donor country!.

Hivi siku watanzania wakigoma kuweka fedha zao kwenye hiyo mifuko nani atawalaumu?

Halafu hili jambo la kionevu sasa limegeuka tabia, huwa linajirudia rudia kila awamu, CCM na serikali yake ni yakuifuta kabisa nchi hii.
 
Wapo pia wazee ambao kwa mujibu wa maamuzi ya wizara ya fedha wanastahili kulipwa kima cha chini pensheni si pungufu ya laki 1 tokea july, 2015. Hadi sasa wastaafu hawa wanalipwa pensheni chini ya tsh. 100,000! Wamedai mpk wamekata tamaa. Uhakiki umefanyika tokea mwaka jana lakini malipo hayatekelezwi na wanaendelea kuteseka. Very sad!
 
Wapo pia wazee ambao kwa mujibu wa maamuzi ya wizara ya fedha wanastahili kulipwa kima cha chini pensheni si pungufu ya laki 1 tokea july, 2015. Hadi sasa wastaafu hawa wanalipwa pensheni chini ya tsh. 100,000! Wamedai mpk wamekata tamaa. Uhakiki umefanyika tokea mwaka jana lakini malipo hayatekelezwi na wanaendelea kuteseka. Very sad!

Halafu Rais Magufuli huyu huyu anajiita RAIS WA WANYONGE!

Fedha za kujenga SGR, FLY OVERS na GORGE zipo lakini za kuwalipa wazee hazipo...huyu Rais ni tatizo!
 
Masikini Wazee wetu Wastaafu wanaishi kwa dhiki kubwa huku Mafao yao wakizungushwa wakati waliitumikia Nchi hii kwa Uaminifu mkubwa mpaka Wakastaafu.Enyi Viongozi waoneeni huruma Wazee hawa.

Huyu ni Rais wa VITU na siyo WATU!

Vipaumbele vyake ni kuona barabara, flyovers, ndege(Dreamliner,Bombardier, etc) na Kujenga Ikulu za Chamwino na Chato !! Lakini mafao ya wastaafu, kuboresha mishahara na marupurupu ya Wafanyikazi Hana Fedha na wakti huohuo anasema hii nji ni Tajiri sana! Ni shidaaaa!
 
Nini Magufuli hili ni tatizo la kundi la MACCM wote

Kuna waastafu wa URAFIKI na TZR wanadai mafao kwa miaka kumi na Saba sasa, Yani wanakufa

Binafsi nini mzee wangu katika hilo kundi nikipita maeneo hayo natamani kuchoma moto hayo majengo.

CCM ni msiba kwa Taifa.
 
Nini Magufuli hili ni tatizo la kundi la MACCM wote

Kuna waastafu wa URAFIKI na TZR wanadai mafao kwa miaka kumi na Saba sasa, Yani wanakufa

Binafsi nini mzee wangu katika hilo kundi nikipita maeneo hayo natamani kuchoma moto hayo majengo.

CCM ni msiba kwa Taifa.

Pole Sana Mkuu.
Watz wanatakiwa kwene Uchaguzi Mkuu wa 2020 kuchukua MAAMUZI MAGUMU NA SAHIHI!!
Byebye CCM!
 
Wapo pia wazee ambao kwa mujibu wa maamuzi ya wizara ya fedha wanastahili kulipwa kima cha chini pensheni si pungufu ya laki 1 tokea july, 2015. Hadi sasa wastaafu hawa wanalipwa pensheni chini ya tsh. 100,000! Wamedai mpk wamekata tamaa. Uhakiki umefanyika tokea mwaka jana lakini malipo hayatekelezwi na wanaendelea kuteseka. Very sad!
Ndiyo serikali ya wanyonge anayoiongoza mhe rais jpm.
Mnyonge anyongwe ila apewe haki yake.
 
Ungechoma ndio ukajua maana ya ccm inanguvu
Nini Magufuli hili ni tatizo la kundi la MACCM wote

Kuna waastafu wa URAFIKI na TZR wanadai mafao kwa miaka kumi na Saba sasa, Yani wanakufa

Binafsi nini mzee wangu katika hilo kundi nikipita maeneo hayo natamani kuchoma moto hayo majengo.

CCM ni msiba kwa Taifa.
 
Hawakutunza ziada .serkali inawathamini wastafu
Masikini Wazee wetu Wastaafu wanaishi kwa dhiki kubwa huku Mafao yao wakizungushwa wakati waliitumikia Nchi hii kwa Uaminifu mkubwa mpaka Wakastaafu.Enyi Viongozi waoneeni huruma Wazee hawa.
 
Back
Top Bottom