Rais Magufuli kuondoka kama Che Guevara

Rais Magufuli kuondoka kama Che Guevara

Che Guevara gani unaemuweka kundi moja na akina Jiwe na hayo matakataka mengine ya udikteta? Labda uliyemuumba wewe.
Tunaemjuwa ni yule aliyepinga ubeberu popote ulipo mpaka huku Afrika. Aliyetoa mpaka uhai wake kupigania wanaokandamizwa. Nenda kasome kwa umakini zaidi itakusaidia.
Katika hali isiyo ya kawaida, Madikteta wote duniani huondoka kwa staili moja ya fedhea sana.

1. Muamar Gaddafi.

2. Saddam Hussein.

3. Al Bashir,

4. Mohamed Mosri.

5. Mugabe

6 .Sankara na wenzao waliondoka kwa aibu kubwa , sasa leo huyu mtu anayedhani yeye ndiye kila kitu huenda akaondoka kwa staili hiyo.
Tumsome CHE GUEVERA alikuwa kama JIWE, kila tabia ilifanania, tofauti ni kwamba Che guevera ana shahada ya kusomea tofauti na huyu ya kupewa tu, kwakuwa alisoma akiwa .

View attachment 1257614

Jina kamili: Ernesto Guevara
Kazi: Daktari, mwanamapinduzi wa kijamaa (Marxist)
Uraia: Argentina
Kuzaliwa: June 14 1928
Kufariki: October 9, 1967 ,Bolivia milima ya La heguera
Chanzo cha kifo: kuuwawa kwa kupigwa risasi

Kama kijana msomi wa shahada ya udaktari, Che Guevara alisafiri nchi nyingi sana huko bara la Amerika ya kusini na rafiki yake, akawa ni mtu mwenye uchungu mkubwa kuona maisha ya dhiki,njaa, magonjwa nchi za America ya kusini, akawa na mwamko mkubwa kubadili hali ile kwa kuwa aliamini ya kuwa mfumo wa ubepari ndio chanzo kikubwa kilichokuwa kinaitafuna Latin America.

Miaka ya 50 akiwa anasoma udaktari huko Mexico Che Guevara alikutana na Fidel Castro na Raul Castro ambapo watatu hao walipanga mapinduzi ya kumg’oa raisi wa Cuba wakati huo Fulgencio batista ambaye alikuwa na huhusiano wa kimaslahi na America, Che akapata nguvu na uaminifu mkubwa kutoka kwa Fedel Castro na kupandishwa kuwa kiongozi wa wanamgambo (guerilla insurgents)

Punde tu baada ya Fulgencio batista kukimbia CUBA,Che alihusika kama mtu muhimu katika serikali ya Cuba iliyoongozwa na Fidel Castro, akiwa kama Gavana wa benki kuu ya Cuba ambapo saini yake ilianza kutumika katika noti za CUBA , baadae kama waziri wa kilimo wa Cuba.

Mwaka 1964 akiwa kama mmoja ya msafara wa watu wa serikali ya Cuba umoja wa Mataifa New York MArekani, aliweza kupata “sifa” ya “mwanamapinduzi halisi wa kukumbukwa” pale alipotoa hotuba ndefu katika ukumbi wa UN akilaumu wazi ukimya wa Umoja huo juu ya kilichokuwa kinaendelea Afrika ya kusini (ubaguzi wa Rangi) alinukuliwa akisema

“wale wanaoua watoto wao na kuwabagua kila siku kwa sababu ya rangi ya ngozi zao, wazungu wanawaua watu weusi na hawakamatwi, serikali ya kikaburu inawalinda wauaji, na mbaya Zaidi inawaadhibu watu weusi kwa kuwa tu wanatataka haki zao na utu wao, vipi watu hawa (makaburu) wakaitwa watetezi na walinzi wa Amani?”

MGOGORO WA CONGO – DRC
Miezi michache baada ya kutoa hotuba UN, Che alitoweka katika maisha ya kawaida “public life” na hakuna aliyejua alikwenda wapi mpaka baadae ilipokuja gundulika Che alikuwa akipigana sambamba na Laurent Kabila huko Congo dhidi ya wabeligiji na baadhi ya wapiganaji wa ki cuba waliokuwa Afrika, vita ambayo ilishindikana na akakimbilia Tanzania na kukaa maeneo ya karibu na ziwa Tanganyika na baadae Dar es salaam huku akiishi kwa kujificha

Baadae mwaka 1966 alirejea Cuba kumuaga kwa Fudel castro na kusafiri kwenda Bolivia kuendeleza harakati zake za kuzikomboa nchi za America ya kusini kutoka kwenye makucha ya Ubepari…aliingia Bolivia akiwa kama mfanyabiashara hasiyejulikana baada ya kunyoa upara, kuweka mvi bandia na kuyoa ndevu zake zote, akaweka kambi na baadhi ya wapiganaji wenzake aliowakuta Bolivia maeneo ya milima ya montane dry fores

KUKAMTWA NA KUUWAWA
Mwaka 1967, makachero wa Bolivia wakisaidiwa na CIA amabye alikuwa akiwakilsha ndugu Felix Rodriguez waligundua maficho ya ache na kundi lake huko milimani Bolivia, asubuhi ya October 8 mwaka 1967 wanajeshi takribani 1,800 walizingira maeneo yoote ya milima walikokuwa wamejificha akina Che na ikapiganwa vita ya masaa kadhaa na Che akipigwa Risasi za miguu na kukamatwa na wenzake,

Yasemekana baada ya kuzidiwa katika mapigano yale alisema
“Usifyatue risasi, mi ni Che Guevara nina thamani kubwa kuwa hai kuliko kunikamata nimekufa”

Alifungwa kama na wenzake akakamatwa na kupelekwa kijiji cha La higuera ambapo baada ya raisi wa Bolivia ndugu kusikia amekamtwa alitoa amri auwawe haraka sana, wakati huo huo CIA walimtaka apelekwe Panama akahojiwe kwa kina na salama yake ili hasiuwawe alikuwa apelekwe America japo haikutokea.

Siku moja kabal ya kuuwawa alichukuliwa na baadhi ya wanajeshi na kupiga picha ya kumbukumbu na kesho yake akauliwa na askari mmoja aliyejitolea na kumpiga risasi sita za kifua na kufa palepale

Kabla hajapigwa risasi na muuaji wake haya ndio yalikuwa maneno yake ya mwisho

“Najua umekuja kuniua, shoot mtu mwoga wewe!!! na ufahamu utakua umeua mwanaume kamili”
Aliacha wake wawili na watoto watano.

"Jiwe" kama tunavyomwita huku mitaani na MEKO kama ambavyo Nape a.k.a Kogogo2014 anavyomuita huenda akaondoka kama CHE GUEVARA .
Ameteka seriakali za mitaa, sasa atakuja serikali kuu na baadae atajiongezea muda kama KAGAME NA MUSEVENI.


*HOJA YAKO*
 
Museveni aliondoka kwa aibu? au Mimi pekee ndio sijui Museveni bado ni rais Wa Uganda?

Rais Magufuli hawezi kuondoka kwa aibu kama unavyopotosha kwa sababu:

1. Rais Magufuli ni muumini Wa katiba ambayo imeweka ukomo Wa miaka 10 na baada ya miaka 10 ataondoka zake kupisha wengine. kwa namna hii ataondokaje kwa aibu?

2. Rais Magufuli ndiye Rais bora Wa kizazi hiki na hata kama hamtalisema hili mawe yatasema kwa ajili ya wengi.

3. Rais Magufuli ndio yule katiba na sheria inamsema kuwa anafuata sheria ,kanuni na taratibu za uongozi.

4. Rais Magufuli ni sauti na kilio cha wengi waliokosa sauti katika matumizi yasiyo sahihi ya kodi zao, waliokuwa wanalia unyanyasaji na maonezi mbalimbali ndani ya ardhi yao.

huyu ndiye Rais Magufuli ambaye ni kithibitisho kuwa nabii hakubaliki kwao. Yesu aliwahi kusema " kama mti mbichi wanaufanyia hivyo ,je mkavu wataufanyia nini? Rais Magufuli ni nabii Wa Tanzania

Yaani wewe akili zako ziko kwa nyuma... Siku zikiwa kwa mbele utang'amua kuwa yote uloandika hapo ni uongo uliolishwa huku nyuma ya mapazia yanafanyika mazito!
 
Che Guevara alikua kiongozi wa taifa gani?!
Na mimi nashangaa. Che Ernesto Guevara alikuwa ni mwanamapinduzi na hakuwahi kushika nyadhifa ya kuiongoza nchi yoyote kama raisi. Japo alishawahi shika nafasi za juu kama uwaziri kwenye serikali ya Cuba ila kwa mapenzi yake mwenyewe aliacha nafasi hiyo na kuendelea toa support kwa wapigania uhuru kwingine duniani, hasa Amerika ya Kusini/Latin America
 
Kama mzalendo mbona anaogopa CAG.?
Museveni aliondoka kwa aibu? au Mimi pekee ndio sijui Museveni bado ni rais Wa Uganda?

Rais Magufuli hawezi kuondoka kwa aibu kama unavyopotosha kwa sababu:

1. Rais Magufuli ni muumini Wa katiba ambayo imeweka ukomo Wa miaka 10 na baada ya miaka 10 ataondoka zake kupisha wengine. kwa namna hii ataondokaje kwa aibu?

2. Rais Magufuli ndiye Rais bora Wa kizazi hiki na hata kama hamtalisema hili mawe yatasema kwa ajili ya wengi.

3. Rais Magufuli ndio yule katiba na sheria inamsema kuwa anafuata sheria ,kanuni na taratibu za uongozi.

4. Rais Magufuli ni sauti na kilio cha wengi waliokosa sauti katika matumizi yasiyo sahihi ya kodi zao, waliokuwa wanalia unyanyasaji na maonezi mbalimbali ndani ya ardhi yao.

huyu ndiye Rais Magufuli ambaye ni kithibitisho kuwa nabii hakubaliki kwao. Yesu aliwahi kusema " kama mti mbichi wanaufanyia hivyo ,je mkavu wataufanyia nini? Rais Magufuli ni nabii Wa Tanzania
 
Si muda mtaanza kukufuru mkisema alitabiriwa na mitume na manabii wapiga zumari na vinubi sijui huwa mna akili gani
 
Kama mzalendo mbona anaogopa CAG.?
Ukiona mtu analazimisha kutambulika kwa jambo fulani ujue ni dhaifu.
1. nyerere: hakuwahi kutaka kutambulika zaidi ya kuitwa ,\mwalimu.
Mwinyi na mkapa the same,

kikwete ndio kabisaa, ila JIWE anataka kila kitu iwe yeye, na bado hamna kitu
 
Thomas Sankara alikuwa Dikteta? 😂😂😂😂
 
Stop this nonsense. Stop degrading Che by even comparing Magufuli with him. People like you have no idea what Che stood for. Stop this nonsense. Praise your president all you like but stop with the delusions.

I see people wear Commandante Ernesto Che Guevara Tshits, caps and put his posters on their cars and I ask myself......Do they really know who this man was? His ideas...what he stood and die for...

That man first of all was a doctor from Argentine and could have lived a comfortable life as a doctor and fend for his family BUT he stood up and made motorcycle trip arround South America.

Seeing how poverty degrade human and how poor leadership failed to provide for it's citizen Che's ideas and life changed forever.....

He end up in Guatemala, met Fidel Castro .....then spend the whole night listening to what Fidel was fighting for and understood him.

They left Guatemala and set a camp in Mexico (mekiko)....After that sail to Cuba onboard Granma.....Che was initially the outfit doctor but having seeing his fellow Comrades fall in combat, he pick up the gun and the rest is history.......

Do people even realize at one point Che visit Dar es salaam....met with various freedom fighters as Dar was a headquarter for freedom Fighters from Southern Africa?????

He even met the late Kabila and made a Journey to Congo DRC to join Guerrillas there but later disqualified them as just drunkards and people who are after women with no clear political agenda.....

He then left for Bolivia where Gringos (America) or Yankees as South Americans like to call them formed a Special force purposely trained for killing Comrade Che and it did just that....

The man gave up his Country,his career as a Medical doctor and his life for others.......

How do even start to compare this man with some African politicians.......wachumia tumbo???????

Let Che be Che and His Excellency our President be himself......

Adios
 
Unamsema Guevara?

Wewe ni nani hara midomo yako itoshe kumzungumzia huyu meamba?
 
Hata Freeman Mbowe kuondoka hivyo hivyo.

Dikteta wa uenyekiti wa chama
 
Back
Top Bottom