Mfiaukweli
JF-Expert Member
- Aug 30, 2018
- 5,636
- 8,779
Kwanza unatakiwa kujua kuwa wizara ambayo inashughulikia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa iko kwenye ofisi ya Rais. Kwa maana nyingine, Boss wa Serikali za Mitaa ni Rais.
Pili, Mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa iko mikononi mwa Ofisi ya Rais.
Rais alichofanya ni kutimiza majukumu ya Ofisi kama ambavyo kanuni za utumishi zinavyomtaka.
Kwa upande wa kisiasa, Rais Magufuli na CCM hawana hasara yoyote kama watu wengi hawatajitokeza kwenda kupiga kura kwa sababu haiwaathiri katika majukumu yao ya kitaifa kwa sababu tatizo la political legitimacy lipo tokea mwaka 1995.
Kutojitokeza watu wengi kwenda kujiandikisha ni pigo kwa upinzani ambao unategemea nguvu ya madaraka kupitia sanduku la kura!
Haina mjadala kuwa watawala wa nchi za kiafrika huhofia sana wanapoona wananchi wengi wanakuwa na mwamko wa kutaka kupiga kura kwa sababu hii inayonyesha wanataka mabadiliko.
Jaribu kuangalia utagundua kuwa CCM walipata msukosuko katika chaguzi mbali mbali kutokana na wananchi wengi kujitokeza kupiga kura.
Nihitimishe kwa kusema, Watu wengi kutojitokeza kwenda kujiandikisha ni sherehe kwa serikali iliyoko madarakani (CCM) na kilio kwa wale wanataka kuingia madarakani (Wapinzani).
Umeandika sawa na mtu asiefikiria. Hata watu wote wangejiandikisha na wakapigia kura chama tofauti bado ccm watajitangaza kushinda. Unadai kuwa ccm wanachekelea watu kutojiandikisha sasa kwa nini Magufuli anatishia kuwaadhibu viongozi wa mikoa itakayokuwa na idadi ndogo ya waliojiandikisha? Ni aibu kwa ccm watu kususia uchaguzi maana inadhihirisha kutokukubalika kwao.