tang'ana
JF-Expert Member
- Apr 3, 2015
- 11,810
- 15,070
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.John Pombe Magufuli leo tarehe 29 Novemba, 2020 amefanya uteuzi wa Wabunge 2 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwanza, Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. Humphrey Polepole kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Bw. Humphrey Polepole ni Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Pili, Mhe. Rais Magufuli amemteua Bi. Riziki Said Lulida kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Wabunge Wateule hao wataapishwa kwa mujibu wa sheria na taratibu za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
====
REJEA:
Mbunge wa Viti Maalum (CUF), Riziki Lulida aomba kurejea CCM. Asema Rais Magufuli ni msikivu alifuturu naye na kuongea naye kama ndugu
Amesema amerudi CCM kwasababu nyingi na ya kwanza ni kuwa Rais Magufuli ni msikivu na atakaposikiliza hoja yake atakuwa msikivu. Amesema “Mwaka 2015, Rais alinikuta nje akaniuliza nafanya nini. Nilijibu nataka kwenda nyumbani kufuturu. Akaniambia mimi ndio baba watoto twende, nami nikamuambia...
www.jamiiforums.com