Matajiri wa nchi hii walifikia wakati ambapo wakageuka Miungu watu, wakashindwa kukumbuka ukweli kwamba kila mtu anapaswa kuwa mtenda haki kwa nafasi yake kwenye jamii. Rais JPM hajawadharau bali anawakumbusha tu kuhusiana na kujinyenyekeza na kujishusha maishani.
Unakumbuka issue ya yule mke wa waziri ambaye alijibizana hovyo na traffic police?. Hakuna anayepaswa kujiona yupo juu ya sheria, na kujiona anao ushawishi mkubwa kiasi cha sheria na matakwa yake kuwa sio kitu mbele yake.
Sio kweli Matajiri wengi ni wastarabu sana.
Baharessa, Mengi, Dewj, Abood, Moil, Manji, na wengine wengi ni watu wa watu na wanajichanganya sana na watu wa chini.
Hii tabia ya kutafuta umaarufu wa kisiasa kwa kuwaponda na kuwasingizia matajiri sio nzuri.
Watu wenye hulka ya kujifanya miungu watu ni wale wanaopata mapesa kupitia vyeo vyao na madaraka serikalini.
Hawa ndio hatari sana. Hawa ndio wanatishia watu maisha.
Na hata sheria nyingi zinazotungwa zinatungwa kuwalinda wao wasiguswe wala kunyoshewa kidole. Hawa ni zaidi ya miungu watu. Ni miungu kabisa wa dunia hii. Wanataka kuitwa waheshimiwa na wanataka kila mtu awaogope na kuwatii kwa sababu ya mamlaka waliyonayo. Hawa hata familia zao ni tatizo sana kwenye jamii. Watoto wao hawaguswi. Zaidi hawana mchango wowote kwenye majanga kama haya. Na hata wakitoa basi wanatoa kwa malengo ya kupata umaarufu.
Tusiwasingizie wafanyabiashara matajiri kuwa ni watu wabaya. Wabaya siku zote ni majizi yaliyoshika madaraka makubwa yenye vipato vikubwa na madili mengi. Hawa ndio wenye dharau mana wanapata pesa nyingi bila kufanya biashara yoyote zaidi ya kuwatumia wafanyabiashara kama vitega uchumi wao.
Labda wewe unitajie mfanyabiashara tajiri anayejifanya mungu mtu.