Rais Magufuli avuruga wengi

Rais Magufuli avuruga wengi

Hata hivyo namna ya kumsimamisha haikuwa nzuri. Mh raisi anapaswa kuwaheshimu walio chini yake. JPJM amemhukumu Kabwe mbele ya hadhira na katika namna dhalili isiyofaa kwa binadamu yeyote.

Anyway, tulimtaka wenyewe sasa tumvumilie!
Alianza mwenyewe kujidhalilisha kwa kuiba mali za umma. Wenje alishawahi kulia sana bungeni lkn iyo iyo sheria haikufutilia wala kuchunguza tuhuma zinazomkabili leo sheria inaonekana sana kwa kuwa amemkuta. She ria inalinda sana wezi.big up Mr prezidaa
 
Nilazima watanzania tujiandae kisaikolojia ktk swala lakutumbuliwa, utumbuaji nikazi kidogo sana mh Rais anafanya. BADO TunaKWENDA kutaifishwa mali za walio hujumu uchi wetu na mahakamani nakama sheria ingeruhusu wangenyongwa.
Mtu anaye tetea mafisadi nakusema eti wanatumbuliwa vibaya sijuwi haki nasheria nilazima wajiulize kwanza watu wangapi wamekufa kwakukosa uduma bora kisa ni hao mafisadi.
Tumefika hapa kwasababu yakukaa kimya nakuacha watu wachache kuhujumu uchumi nakugawa fadhila kwenye kila taasisi ili siku wakikutwa na majanga muwe wakwanza kuwatetea. Pesa zimegaiwa makanisan na misikitin ili kuficha ubaya wao.
LAKINI MIM NISEME SIO DK MAGUFULI WALA SERIKALI HII INATUMBUA MAJIPU. ILA MUNGU AMESHUKA MWENYEWE KULIJENGA TAIFA HILI KUPITIA CCM CHINI YA SERIKAL YA DK JOHN POMBE MAGUFULI. TULIPOKUWA TUMEFIKA TAIFA HILI MASIKINI ALIKUWA HANA CHAKE NA HUYU MAMA ANAKUWA SIO MKWELI BORA ANGEKAA KIMYA MAANA SIKU YA KIAMA ATAKUWA NAMASWAL MAGUMU YAKUMJIBU MUNGU. BORA WATU WATUMBULIWE WOTE WAISHE SHERIA ITAKUJA FUWATA MKONDO WAKE AS LONG AS WAKATI WOTE RAIS WETU GENIUS HUWA ANASEMA "AMEMSIMAMISHA KAZI", AMETENGUA UTEUZI. Sasa sijuwi mtampata wapi kwenye mashtaka. Au mlitaka asemeje?
JANA NILISEMA HATA TZ TWAFANYA KIDOGO SANA KWENYE KUTUMBUWA MAFISADI.CHINA UNATUMBULIWA, UNAPELEKWA MAHAKAMANI HAKI YAKUSHINDA KESI INAKUWA HAKUNA NA MWISHO HAKIM ANATANGAZA JAMUHUR INAKUNYONGA NAILI WENGINE WASIRUDIE UNATAKIWA KUOMBA RADHI KWA TAIFA KABLA YA KUNYONGWA NA WAKISHA KUNYONGA TV YATAIFA INATOA MZOGA WAKO UONEKANE WATU WOTE WAJUE YOUR NW DEAD. Nahakuna cha human right wala cha nini na china uchumi wake wapaa kama rocket.
UFISADI UMELETA LAANA KUBWA KTK TAIFA HILI YEYOTE ANAYE PINGA KAZI NZURI NA MOYO WA MH RAIS KUWATUMIKIA WATANZANIA YAMPASA KWENDA MAKABURINI NAKUYAULIZA WANGAPI WALIKUFA KWA UZEMBE NA UFISADI WATU WACHACHE KTK SERIKALI NAKAMA WANGETAKA HAKI IFUWATE MKONDO WAKE WANGETAKA NIN KIFANYIKE JUU YAO. YATOSHA YALIOKWISHA TOKEA YATOSHA UHAI WA MTANZANIA KUTOKUWA THAMAN MBELE YA MAFISADI. MTU ANAYE DHANI KUWA HUYU RAIS HATENDI HAKI KULIKOKUWA MPINZANI NDANI YA SERIKALI HII BORA ATOKE NAAKAFANYE KAZI NYINGINE KUPISHA WENGINE WENYE HARI NA NGUVU YAKUMSAIDIA RAIS WAPATE HYO NAFASI.

Mh Rais wewe piga kazi, nakwaushauri ongeza nguvu kwenye vyombo vya usalama. LAZIMA TAIFA HILI LITANYOOKA TU HAUPO PEKE YAKO ANGALIA, KULIA,KUSHOTO MBELE NA NYUMA UMEZUNGUKWA NA MAELFU YA WA TZ NA MALAIKA WAMUNGU KUKULINDA NAHAKUNA KITAKACHO KUGUSA.
NIMTU ASIE JUWA TULIPOTOKA ANAWEZA KEBEI KAZI YAKO ILA MUNGU NA MALAIKA NA WA TZ WOTE TWAUNGANA KUSEMA THANK YOU VERY MUCH MR PRESIDENT DR JOHN POMBE MAGUFULI.
Mungu ibariki Tanzania na watu wake. Amen
At least you are there brother thanks. Mie nilisema wapigwe risasi hadharani tu kusiwe kabisa na mafisadi.
 
Kwa bahati mbaya sana Mheshimiwa John Pombe Magufuli amekuja na kauli mbiu ya kutumbua majipu. Lakini binafsi naona hakuangalia mbali. Aliona mwisho wa pua yake tu. Hili ni kosa la kwa.nza kwa kiongozi mkubwa kama yeye, kutokuona mbali. Kosa la pili ni namna anavyotumbua jipu. Hatumbui kitaaluma namna majipu yanavyotakiwa utumbuliwa. Nitaeleza moja baada jingine.
Angalianza kujiuliza ni kwa nini majipu yapo. Majipu msingi wake ni upungufu wa kinga mwilini. Kinga ikipungua ukitumbua jipu hili huota jipu jingine mahala pengine. Mchezo hujirudia rudia hadi jipu linaota kwenye ini, mahala pabaya zaidi. Daktari makini hatibu dalili, hutibu kisababishi cha ugonjwa. Daktari makini hawezi kutibu kichwa kwa sababu kichwa ni kiashiria tu kuwa mwili unatatizo mahali. Atachunguza kitabibu. Akigundua kwa mgonjwa ana malaria atatibu malaria akiwa makini zaidi atamshauri mgonjwa kufyeka majani yote kuzunguka nyumba yake, kufukia vidimbwi vyote wanamozalia mbu na kutumia chandarua kwa kulala ndani ya chandarua mwaka mzima. Magufuli hafanyi hivyo anampa mgonjwa dawa ya kutuliza maumivu ya kichwa kwa kumpa panadol mbili mara tatu kutwa maumivu yakizidi anaongeza dozi tatu mara nne kutwa, lakini masikini DKT Magufuli mgonjwa wake Tanzania haponi na hakuna dalili kuwa atapona sababu anatibu dalili. Masikini Magufuli apate wa sikio ili asikie kuwa tatizo siyo majipu ni kinga imepungua ili ampe mgonjwa wake vyakula vinavyopandisha CD4? Shida ya Tanzania na watanzania ni maadili. Tatizo la maadili linaanzia kwa wanasiasa kujilimbizia mali kwa kutumia nafasi zao za kisiasa. Tanzama viongozi wa kisiasa wanavyojilimbizia mishahara mikubwa. Viongozi wa kisiasa kuanzia raisi, mkamu wa rais, waziri mkuu mawaziri manaibu mawaziri, wabunge nk nk mishahara yao na marupurupu yao yalivyo makubwa upita hata wanataaluma wa hali ya juu. Kansa hii ndiyo ndiyo iliyotufikisha hapa tulipo. Kiini cha jipu ni fikira kuw ukiwa na nafasi fulani ya kiutumishi sharti uitumie wewe mwenyewe kwanza kabla hujawagawia wengine. Jipu hili lipo katika kila ubongo wa Mtanzania kwa sasa. Hizo zingine ni dalili tu.
Nani aliyesema mtumishi aliyeko kwenye taasisi za fedha alipwe zaidi kuliko daktari aliyeko hospitali au mhandisi anayejenga barabara au daraja ati kwa sababu anatunza fedha? Nani aliyesema mtumishi aliyeko TRA ana umuhimu kuliko mtumishi aliyeko kilimo.
Tunajua hata wabunge Bungeni hupitisha miswada kwa kuangalia masilahi ama ya vikundi ama binafsi. Tatizo linaanzia katika akili za watanzania wote kwa pamoja wala siyo mmoja mmoja.
Kosa la pili ni kutumbua jipu bila hata kufuata kanuni za utumbuaji. Jipu linapaswa kwanza lionyeshe mdomo wake, pili lisubiriwe hadi liive ndipo litumbuliwe. Unapokamua jibu sharti usaha wote utoke pamoja na kiini chake. Ukitumua jipu bila kumalizia kutoa kiini, jipu linarudia tena palepale. Magufuli anachanja juujuu nakutoa amu kidogo huku akiacha kiini cha jipu. You are sorry my dear man hujatumbua jipu bado.
Fuata taratibu za kuwaondoa watu kazini. Usikurupuke wewe ni Rais, una haraka gani?
STAILI ya Rais John Magufuli kutimua watumishi wa umma kwa ‘munkari’ inawavuruga watu wengi ambapo Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimeonya, anaandika Regina Mkonde.

Kabla ya LHRC kuonya, Edward Lowassa, aliyekuwa mgombea uraas kupitia Chadema na kuungwa mkono na Ukawa pia Sheikh Ponda Issa Ponda, Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam nchini walionya staili hiyo na kushauri taratibu za kisheria za utumishi wa umma zifuatwe.

Helen Kijo Bisimba, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC ameikumbusha serikali kufuata sheria za utumishi wa umma katika kuwawajibisha watumishi wanaotuhumiwa kufanya makosa.

Bisimba ametoa kauli hiyo leo wakati wa uzinduzi wa ripoti ya haki za binadamu ya mwaka 2015 uliofanyika jijini Dar es Salaam, MwanaHALISI Online lilishuhudia.

“Inafahamika kwamba, Rais John Pombe Magufuli ameikuta nchi sehemu mbaya na anahitaji kuirekebisha.

“Ila ni vema akafuata taratibu za kisheria wakati anapotaka kumtumbua mfanyakazi aliyeajiriwa na serikali ambayo ndiyo anayoiongoza,” amesema Bisimba.

Anaeleza kuwa, Rais hakuchukua uamuzi wa busara kwa kumsimamisha kazi Wilson Kabwe, aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam mbele ya hadhara na kwamba, alitakiwa kufanya uamuzi huo kwa kufuata sheria.

“Makonda (Paul Makonda) hakuwa na sababu za kumsema Kabwe mbele ya hadhara, alitakiwa afuate utaratibu, si maanishi kuwa namtetea Kabwe, bali kutokana na agizo la rais alilotoa la kusimamishwa na kufanyiwa uchunguzi, je atakapobainika kuwa ni msafi ataweza kumsafisha?” anahoji.

Bisimba amewataka Watanzania waache unafiki kwamba, wapo baadhi ya wanasheria wanaojua taratibu za kumsimaisha kazi mtumishi wa umma lakini walishindwa kumshauri badala yake waliacha aendelee na uamuzi wake.

“Mfano jana alikuwa anauliza wananchi, nimtumbue nisimtumbue, mbele ya hadhara, huyo aliyekuwa anamfanyia hivyo ni mtumishi aliyeajiriwa na serikali, isitoshe Kabwe ninavyomjua ni mgonjwa, je angepata matatizo ingekuaje?” anauliza.

Bisimba pia ametolea mfano wa hatua iliyochukuliwa wakati wa kufukuzwa kazi Anne Kilango Malecela, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kwamba, aliju akwamba amefukuzwa kazi baada ya kupigiwa simu akiwa ofisini.

“Kilango alitumbuliwa wakati alipokuwa ofisini, alipigiwa simu ili kujibu baadhi ya maswali juu ya kufukuzwa kwake, cha kustajaabisha hakuwa na taarifa kama alifukuzwa kazi na rais,” amesema.

Amesema kuwa, mfumo wa utumishi mbaya ulianzishwa na serikali baada ya kuuondoa mfumo wa ujamaa na kuuweka mfumo wa ubepari.

Kwa upande wa sheria anasema, zipo nzuri ila nyingi kati ya hizo zinahitaji maboresho na kwamba, inahitajika Katiba Mpya ili ifanyike marekebisho ya sheria zilizoachwa na mkoloni.

Aidha, ripoti iliyotolewa leo inaonesha kuwa, uchaguzi uliofanyika tarehe 25 Oktoba 2015 ulikuwa huru japo kulikuwa na wasiwasi wa kutokuwa na haki kutokana na madai ya kuibiwa kura.

Ripoti hiyo inabainisha kuwa, kwa mujibu wa uangalizi uliofanywa na LHRC umebaini kuwa, elimu ya uraia haikutolewa vizuri, watu wenye ulemavu walipata shida kufika maeneo ya kampeni na kutumika kwa vifaa vya serikali wakati wa kampeni hasa magari pamoja na uchelewashaji wa kutangaza matokeo katika vituo mbalimbali.
 
Hivi kati ya JPM/Makonda na TAKUKURU/Police, ni nani mwenye uwezo na pengine mamlaka na weledi wa kumtuhumu mtu kuhusika na rushwa? Nashindwa kuelewa inawezekanaje Makonda anamtuhumu mtu kula rushwa wakati mtu huyo hajatuhumiwa na TAKUKURU? Matarajio yangu ni kwamba Makonda akihisi kuna vitendo vya rushwa mahali, anapaswa kuitaarifu TAKUKURU ambao kwa kufuata taratibu zao wanaweza kumtuhumu mtu kuhusika na rushwa au la. Makonda anaweza kumtuhumu/kumwajibisha mtu kwa underperformance na mambo kama hayo. Lakini kumtuhumu mtu kuhusika na rushwa, awaashirikishe TAKUKURU.

Magufuli kumsimamisha mtu kwa kuhisiwa kula rushwa, halafu kuvitaka vyombo husika, ikiwa ni pamoja na TAKUKURU, ni kuingilia uhuru wa vyombo hivyo kufanya kazi zake (It's like putting the cart before the horse). Ni kama vile anaviambia hivyo vyombo viandae ripoti kuhalalisha maamuzi yake na si ripoti ya kueleza ukweli/reality. Unatarajia TAKUKURU itakuja na ripoti ikisema mfanyakazi aliyesimamishwa ni clean na Rais alikurupuka kumsimamisha? Niungane na wale wanaopendekeza TAKUKURU kuongezewa mamlaka ikiwa ni pamoja na kuweka utaratibu ambao utazuia viongozi wa serikali na kisiasa ku-influence maamuzi yao.
POLE KWA KUTOJUA, UMECHELEWA NDEGE. Ni jambazi la CK nyingi tangu Arusha, Mbeya ,Mwanza na sasa Dar es salaam pengine hilo la Dar ni sababu tu. Yupo kwenye ripoti ya CAG KTK ujenzi wa clinic mwanza na sunset hotel kule LECHELELE MWANZA.
 
Na bado kuna watu wanatatumbuliwa tu na utumbuaji majipu hauhitaj ganzi so mvumilie tu yakiwa yanawauma
Tufanye kazi kwa bidii
Tuache kuabudu pesa
Tufikirie zaid ya tunavyoona
Tujenge Tanzania yenye nguvu umoja na mshikamano
Tupunguze lawama za kila siku tuache kuish kimazoea
 
STAILI ya Rais John Magufuli kutimua watumishi wa umma kwa ‘munkari’ inawavuruga watu wengi ambapo Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimeonya, anaandika Regina Mkonde.

Kabla ya LHRC kuonya, Edward Lowassa, aliyekuwa mgombea uraas kupitia Chadema na kuungwa mkono na Ukawa pia Sheikh Ponda Issa Ponda, Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam nchini walionya staili hiyo na kushauri taratibu za kisheria za utumishi wa umma zifuatwe.

Helen Kijo Bisimba, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC ameikumbusha serikali kufuata sheria za utumishi wa umma katika kuwawajibisha watumishi wanaotuhumiwa kufanya makosa.

Bisimba ametoa kauli hiyo leo wakati wa uzinduzi wa ripoti ya haki za binadamu ya mwaka 2015 uliofanyika jijini Dar es Salaam, MwanaHALISI Online lilishuhudia.

“Inafahamika kwamba, Rais John Pombe Magufuli ameikuta nchi sehemu mbaya na anahitaji kuirekebisha.

“Ila ni vema akafuata taratibu za kisheria wakati anapotaka kumtumbua mfanyakazi aliyeajiriwa na serikali ambayo ndiyo anayoiongoza,” amesema Bisimba.

Anaeleza kuwa, Rais hakuchukua uamuzi wa busara kwa kumsimamisha kazi Wilson Kabwe, aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam mbele ya hadhara na kwamba, alitakiwa kufanya uamuzi huo kwa kufuata sheria.

“Makonda (Paul Makonda) hakuwa na sababu za kumsema Kabwe mbele ya hadhara, alitakiwa afuate utaratibu, si maanishi kuwa namtetea Kabwe, bali kutokana na agizo la rais alilotoa la kusimamishwa na kufanyiwa uchunguzi, je atakapobainika kuwa ni msafi ataweza kumsafisha?” anahoji.

Bisimba amewataka Watanzania waache unafiki kwamba, wapo baadhi ya wanasheria wanaojua taratibu za kumsimaisha kazi mtumishi wa umma lakini walishindwa kumshauri badala yake waliacha aendelee na uamuzi wake.

“Mfano jana alikuwa anauliza wananchi, nimtumbue nisimtumbue, mbele ya hadhara, huyo aliyekuwa anamfanyia hivyo ni mtumishi aliyeajiriwa na serikali, isitoshe Kabwe ninavyomjua ni mgonjwa, je angepata matatizo ingekuaje?” anauliza.

Bisimba pia ametolea mfano wa hatua iliyochukuliwa wakati wa kufukuzwa kazi Anne Kilango Malecela, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kwamba, aliju akwamba amefukuzwa kazi baada ya kupigiwa simu akiwa ofisini.

“Kilango alitumbuliwa wakati alipokuwa ofisini, alipigiwa simu ili kujibu baadhi ya maswali juu ya kufukuzwa kwake, cha kustajaabisha hakuwa na taarifa kama alifukuzwa kazi na rais,” amesema.

Amesema kuwa, mfumo wa utumishi mbaya ulianzishwa na serikali baada ya kuuondoa mfumo wa ujamaa na kuuweka mfumo wa ubepari.

Kwa upande wa sheria anasema, zipo nzuri ila nyingi kati ya hizo zinahitaji maboresho na kwamba, inahitajika Katiba Mpya ili ifanyike marekebisho ya sheria zilizoachwa na mkoloni.

Aidha, ripoti iliyotolewa leo inaonesha kuwa, uchaguzi uliofanyika tarehe 25 Oktoba 2015 ulikuwa huru japo kulikuwa na wasiwasi wa kutokuwa na haki kutokana na madai ya kuibiwa kura.

Ripoti hiyo inabainisha kuwa, kwa mujibu wa uangalizi uliofanywa na LHRC umebaini kuwa, elimu ya uraia haikutolewa vizuri, watu wenye ulemavu walipata shida kufika maeneo ya kampeni na kutumika kwa vifaa vya serikali wakati wa kampeni hasa magari pamoja na uchelewashaji wa kutangaza matokeo katika vituo mbalimbali.
Naunga mkono hoja
 
Fisadi ni mtu mdaya sana hatumtetei tunachosema sheria zifuatwe unakumbuka yale ya Samaki tulilipa bei gani?
Hii michakato tuliilalamikia sana..kwenye serikali ya awamu ya nne..hahahah mbona kwenye mambo mengine hatutaki sheria zifuatwe.
 
Yaan bado watu mnatetea sheria kwenye ukweli acheni ujinga sheria nyingi ziliundwa kutetea wachache tuzipuuze ndio maana tunadai katiba ndio maana magu anapuuza kutetea wengi tumuunge mkono
tatizo la kila viporo limehasiri sana ubongo wako! hakuna unachofikiri zaidi ya kutapika tu.
 
Pole muhangaikaji tafuta njia mbadala wa kuendesha maisha ambazo ulizoea ndan ya miaka 30 ya utawala wa kidhalimu
 
POLE KWA KUTOJUA, UMECHELEWA NDEGE. Ni jambazi la CK nyingi tangu Arusha, Mbeya ,Mwanza na sasa Dar es salaam pengine hilo la Dar ni sababu tu. Yupo kwenye ripoti ya CAG KTK ujenzi wa clinic mwanza na sunset hotel kule LECHELELE MWANZA.

Hoja yangu umeilewa lakini? Hoja yangu haina uhusiano wowote na ulichoandika hapa. "Jambazi la CK [sic] la siku nyingi" ni nani? Na hilo jambazi au mtu kuwa kwenye ripoti ya CAG kuna uhusiano gani na hoja yangu kuhusu umuhimu wa kuzifanya taasisi kama TAKUKURU kuwa na more autonomy? Vijana wa siku hizi hapa JF hamtaki kabisa kusoma hoja na kuzielewa. Kwa nini?
 
Aidha, ripoti iliyotolewa leo inaonesha kuwa, uchaguzi uliofanyika tarehe 25 Oktoba 2015 ulikuwa huru japo kulikuwa na wasiwasi wa kutokuwa na haki kutokana na madai ya kuibiwa kura.

Hii kali!
Hili hapo chini kulikuwa na uongo?

Polisi wavamia Kituo cha Haki za Binadamu, wabeba ...
www.jamiiforums.com/2015/.../polisi-wavamia-kituo-...
Translate this page
Oct 30, 2015 - Polisi wanaodaiwa kuwa na silaha za moto wamevamia na kuzingira ofisi ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), ... ni uwezekano wa kituo hicho kuwa na matokeo ya uchaguzi ambayo ... Breaking news: Wabunge wa CUF wamejiondoa katika Bunge la Tanzania katika kipindi cha 2015-2020.
 
Acheni ushabiki nyie kwani yeye Kabwe alipokabidhiwa ofisi hayo hakuyaona. Kwanza anashutumiwa tokea alipokuwa Mwanza. Wengi wape sisi wananchi tumeridhika labda nyie na kituo chenu.
 
Mkuu ukitaka kushindwa kufanya kazi, wasikilize watanzania, ukitumbua watasema, usipotumbua watasema!! Ndio maana namkubali Mkapa alipoita baadhi ya watz ambao ndio wengi kwa maoni yangu kuwa ni wapumbavu na malofa
Unamkubali eeh? Ila yule kijana wa Arusha hukubali mawazoyake!
 
Back
Top Bottom