Rais Magufuli ateua Wakurugenzi Wakuu wa NSSF, TBC na Shirika hodhi la reli (RAHCO)

Dr Rioba ni mpiganaji ,Ilboru boy #HAPA KAZI TU
Ni kweli mkuu..ila aliye juu yake si unamjua? hapo ndipo mtihani kwa dr unaponzia...pili tunamjua rioba kwa muda wake wote amekuwa ni "mtu wa harakati" vp sasa na mofump yetu tunayoifahamu huyu bwana ataachwa aonyenye utaalamu ili kuleta tija au ndo yaleyale yaliyonpata mzee wetu "Doti"..
 
Najua wengi mnampongeza Ryoba kwa kuwa mnamjua kutokana na kuonekana kwake mara nyingi kwenye vyombo vya habari, ila hata hao wawili ni waziri pia. Huyo wa NSSF anajichanganya sana na raiawa kawaida, mara nyingi utamkuta kwenye magazeti ameanzisha ubishi wa CCM na UKAWA kama sio wa Simba na Yanga
 
Yule mama wa NSSF alikaa masaa 5. Dr. RYOBA atakaa siku tano...natabiri Mh. Fulani kwa wadhifa wake atataka kumkalia kichwani lakini Daktari atagoma....hapo itakuwa kusuka au kunyowa....pia inawezakuwa mwisho wa Mh.Fulani


Inaelekea wewe unafahamu mambo...tumuombe Dk. Rioba afanye vizuri, Dk. Rioba ana msimamo, na huyo Fulani huwa hataki watu wenye msimamo...Tuone mambo yatakuwaje, ila namuombea Dk. Rioba afanye vizuri.
 
Hawa wote ni wahadhiri wa UDSM lakini tumeshalizwa na hawa maprofesa kuanzia kwa prof Mbilinyi prof Mahalu prof Tibaijuka, labda hawa watakuwa tofauti na watangulizi wao. Vinginevyo hongera kwa uteuzi.
 
mkatoliki ameteua watu wake?! ye acha awajaze cc hatuna elimu, elimu yetu madrasa
 
Kuna mteule Fulani anafahamika kwa uanaharakati wa Uhuru wa vyombo vya habari, si mwingine Bali ni Dr. Rioba!
Wasiwasi wangu ni kuwa boss wake mheshimiwa Fulani atamwambia " Uanaharakati mwisho chalinze" mjini ni chama tawala tu! Tusubiri tuone!
Rioba
Pita taraaaatibu pale Azam tv muone Tido umuulize masahibu yake TBC,kabla hujaanza kazi. u
Kuna kitu utajifunza
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa watendaji wakuu wa Taasisi tatu za serikali kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo.

KWANZA, Rais Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Profesa Godius Kahyarara kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Uteuzi huu umefanyika kwa mujibu wa Sheria ya NSSF namba 28 ya Mwaka 1997, Kifungu cha 42, kinachoeleza kuwa Rais ndiye mwenye mamlaka ya kuteua Mkurugenzi Mkuu wa NSSF.

Prof. Kahyarara anachukuwa nafasi iliyoachwa wazi na Dkt. Ramadhan Dau, ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.

PILI, Rais Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Ayub Rioba Chacha kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Dkt. Rioba anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Clement Mshana ambaye amestaafu.

TATU, Rais Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Mussa Iddi Mgwatu kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hodhi ya rasilimali za reli Tanzania (RAHCO).

Dkt. Mgwatu anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Mhandisi Benhadard Tito, ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.

Uteuzi wa watendaji wote watatu umeanza mara moja


Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU.
Dar es salaam.
19 Machi, 2016.
Ingekuwa jambo la msingi kama hizi nafasi zingetangazwa watu wakaomba na usaili ukafanyika tungepata watu makini zaidi kuliko marafiki kuvutana, naona prof Godius kama vile kuna mtu kamshika mkono, hainyeshi kama anayo taaluma au uzoefu katika investment au social security.
 
Lizaboni, ulikuwako kwe
Riona hajateuliwa kwa saabu ya uanaharakati wake bali kutokana na utendaji wake
Lizaboni, ulikuwako kwenye bodi ya kumsaidia rais kuteua, especially kumteua huyo Dr. Ryoba?? Unachekesha saana mkuu!!
Uteuzi una mazingatio mengi. Sio utendaji tu wa MTU.
Unaweza Ukawa na utendaji superb lkn ni mwoga maamuzi, na malaya , mlevi ukaachwa na huo utendaji wako pia.
Rais anajua kwa nini kamteua, full stop.
 
hivi inawezekana kwa mteule kukataa uteuzi ama labda kuomba marekebisho yafanyike wizarani ndio akubali ? maana kiukweli si haki duniani hadi ahera kwa Ryoba kuwa chini ya Nape , tuwe wakweli jamani .
kama mwenyewe ameridhia kwa moyo mweupe basi hakuna shida.
 
Dr. Ryioba mchambuzi muruwa wa siasa za ki marx, nakutakia kila la heri. Tuboreshee shirika letu, hakikisha Nape haingilii kazi zako, jitahidi tulipende.

Iwapo utalazimishwa kufanya kinyume na ilivyo sahihi, jiuzulu, rudi chuoni
 
Back
Top Bottom