Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi NIMR Dr. Mwele Malecela

Naunga mkono kabisa kutumbuliwa kwa Huyu Mama, Issue ya ZIKA ni kubwa mno kwake yeye kutangaza kuwa ipo Tanzania au haipo,

Kama ipo ilitakiwa amuone Waziri wa Afya kwanza ili Waziri wa Afya akashauriane na Rais kuhusu kuwepo kwa dalili za ugonjwa huo nchini, then sampuli zichukuliwe zipelekwe maabara Nje ya nchi ikibidi hata WHO wangetakiwa kuhusishwa kupima hizo sampuli, kama ingegundulika hiyo ZIKA ipo nchini, basi Rais au Waziri wa Afya ndio wangetutangazia rasmi na kutueleza nini cha kufanya, sasa Tangazo la Dr. Mwele lilizua taharuki sana kwa wananchi na hata nchi za jirani zimepatwa na taharuki sana na hili swala linaweza kusababisha uchumi wetu kuporomoka kwa sababu watalii wanaweza wasije kabisa na hata nchi zingine Raia wanaotoka Tanzania wanaweza kuzuiwa kuingia huko, hivyo, hili swala si dogo kama tunavyoweza kufikiri
 
Nilimuona akijiumauma na maneno baada ya waziri kutangaza hakuna zika Mara ooh tuliona sampuli Mara ooh hiyo haithibitishi kuwa kuna zika, ameshusha sana hadhi ya utafiti, wao kutest chombo kama kinaweza kutoa sampuli ya zika! Wao wanakuja na matokeo tayari na kutangaza duniani kuwa Tanzania kuna zika.
 
Serikali inaficha nini ina maana kituo cha NIMR Tanzania chini ya Dr. Mwele Malecela PhD Mwele Malecela, PhD | IANPHI wataalamu hatuna na wala hatuamini busara zao mpaka WHO World Health Organization Geneva Switzerland na CDC Centre for Disease Control USA waseme kuwa gonjwa la Zika virus lipo Tanzania Tanzania dismisses reported Zika virus outbreak - Xinhua | English.news.cn

Nini dhana ya kuwa na wasomi Tanzania wanaojiamini na kusimamia ktk taaluma zao maana bora kuzuia maradhi kusambaa zaidi kuliko kusubiri ugonjwa wa Zika Virus usambae na kukumba mamia ya watu wakati serikali haina pesa.

Juzi juzi Waziri Ummy Mwalimu alishutumu "waganga" wa hospitali kuficha ukweli wa kipindupindu ktk maeneo yao kwa kuogopa kutumbuliwa ! Msimamo wa serikali ni upi sasa?
 
Na kweli,ni kama walikuwa wanamsubiria tu,na lazima alishaambiwa amuonye Mange,naona kaliwa kichwa,mimi nataka kujua ni kweli Zika ipo ama?
Ninadhani Zika ni because tu, mkuu lakini yule mama aliachana na Mange long time kitambo, tangia ule wakati wa matusi kwa kina Nafue ilionekana kama habari za ndani anazitoa kwa mkurugenzi. Pia kinyang'anyiro nafasi aliyoshika hakutegemia, inasemekana impact ya mange ilichangia.
 
ITV wametangaza sasa hivi. Dr Mwele Malecela ametenguliwa uteuzi baada ya kutangaza kuwa Tanzania kuna ugonjwa wa Zika. Waziri wa afya amekanusha hakuna zika, na ikafuata habari kuwa uteuzi umetenguliwa.
Huyo anaitwa sijui waziri wa afya sitaki hata kumsikia, mwanamke muongo hakuna mfano.
Ni huyo huyo alitangazia taifa kuwa tunadawa za kutosha kauli iliyokuja kutenguliwa na rais msaidizi, leo siwezi kumshangaa akibishana na utafiti mpaka tuanze kufa ndio wakubali kwamba zika IPO.
 
Mdoma uliponza kichwa

ab250bcbdc31edcf9b1b52c579b21d98.jpg

Ninavyojua kumpiga teke Chura ni kumuongezea mwendo. Hata cv tu ya aliyetumbuliwa ghafla inaizidi by far cv ya mtumbuaji hivyo sijaona kipya hapo sana sana tu anazidi tu kutudhihirishia na kutuonyesha mapungufu yake. Na labda ningemshauri tu kwakuwa tayari imeshaonekana kuwa hawapendi Wataalam na mawazo yao ya Kitaalam basi angeamuru tu kwamba ufanyike ukaguzi wa Wataalam wote waliopo katika Sekta na Idara mbalimbali za Kimamlaka kisha awafute Kazi na awaajiri wale anaowaona wataweza kumlamba miguu hadi unyayo ili aridhike kuwa hana mpinzani na kwamba yeye pekee tu ndiyo Mfalme Njozi hapa Tanzania.
 
Kuna mambo yalikuwa yanasemwa kuhusu JPM nilikuwa siamini sasa naanza kuyaamini
Yapi hayo Mkuu, hebu tudokezee?

Au unaogopa kusema kwa kuwa waweza funguliwa mashitaka ya uchochezi na kutaka kumjaribu Mkulu?
 
Ninadhani Zika ni because tu, mkuu lakini yule mama aliachana na Mange long time kitambo, tangia ule wakati wa matusi kwa kina Nafue ilionekana kama habari za ndani anazitoa kwa mkurugenzi. Pia kinyang'anyiro nafasi aliyoshika hakutegemia, inasemekana impact ya mange ilichangia.
Itakuwa makosa ya kiufundi,ila Mwele ilikuwaje atangaze kuna Zika?Zika ipo TZ AMA HAIPO?
 
Naunga mkono kabisa kutumbuliwa kwa Huyu Mama, Issue ya ZIKA ni kubwa mno kwake yeye kutangaza kuwa ipo Tanzania au haipo,

Kama ipo ilitakiwa amuone Waziri wa Afya kwanza ili Waziri wa Afya akashauriane na Rais kuhusu kuwepo kwa dalili za ugonjwa huo nchini, then sampuli zichukuliwe zipelekwe maabara Nje ya nchi ikibidi hata WHO wangetakiwa kuhusishwa kupima hizo sampuli, kama ingegundulika hiyo ZIKA ipo nchini, basi Rais au Waziri wa Afya ndio wangetutangazia rasmi na kutueleza nini cha kufanya, sasa Tangazo la Dr. Mwele lilizua taharuki sana kwa wananchi na hata nchi za jirani zimepatwa na taharuki sana na hili swala linaweza kusababisha uchumi wetu kuporomoka kwa sababu watalii wanaweza wasije kabisa na hata nchi zingine Raia wanaotoka Tanzania wanaweza kuzuiwa kuingia huko, hivyo, hili swala si dogo kama tunavyoweza kufikiri
Cna uhakika sana km unaelewa research kwa mapana. Nilidhani ungejikita ktk kujua ni aina gani ya research iliyofanywa. Hapo ndipo ungejua who was responsible.
 
Back
Top Bottom