Rais Magufuli asamehe wafungwa 5,678 kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 55 ya Uhuru

Queen V

JF-Expert Member
Jan 19, 2012
776
1,330
Rais John Magufuli ametoa msamaha kwa wafungwa 5,678 ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania Bara.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira, wafungwa 1,340 wataachiwa huru na 4,338 watatumikia kifungo kilichobaki baada ya kupunguziwa moja kwa sita ya vifungo vyao.

Rais ametoa msamaha huo kwa kutumia madaraka aliyopewa chini ya Ibara ya 45 (1) (d) ya Katiba.

Rwegasira imeeleza kuwa wafungwa wote wamepunguziwa vifungo vyao zaidi ya punguzo la kawaida linalotolewa chini ya kifungu 49(1) cha sheria ya Magereza sura ya 58.

Amesema wafungwa waliopewa msamaha huo ni pamoja na wagonjwa wa Ukimwi, Kifua Kikuu (TB) na saratani na ambao wamethibitishwa na Jopo la Waganga chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa au wa Wilaya.
 
Rais John Magufuli ametoa msamaha kwa wafungwa 5,678 ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania Bara.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira, wafungwa 1,340 wataachiwa huru na 4,338 watatumikia kifungo kilichobaki baada ya kupunguziwa moja kwa sita ya vifungo vyao.

Rais ametoa msamaha huo kwa kutumia madaraka aliyopewa chini ya Ibara ya 45 (1) (d) ya Katiba.

Rwegasira imeeleza kuwa wafungwa wote wamepunguziwa vifungo vyao zaidi ya punguzo la kawaida linalotolewa chini ya kifungu 49(1) cha sheria ya Magereza sura ya 58.

Amesema wafungwa waliopewa msamaha huo ni pamoja na wagonjwa wa Ukimwi, Kifua Kikuu (TB) na saratani na ambao wamethibitishwa na Jopo la Waganga chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa au wa Wilaya.


Yule Mfungwa namba moja tapeli Lema(chadema) naye ameachiwa?
 
Kweni mfungwa mwenye kifungo cha maisha gerezani e.g Babu Seya akiwa na TB, Saratani au Ukimwi basi ugonjwa huo unajustify kusamehewa?
 
Kweni mfungwa mwenye kifungo cha maisha gerezani e.g Babu Seya akiwa na TB, Saratani au Ukimwi basi ugonjwa huo unajustify kusamehewa?
Huyo hawezi kupata msamaha maana kosa alilotenda halina msamaha wa rais
 
Back
Top Bottom