dikteta2020
JF-Expert Member
- Aug 14, 2018
- 595
- 3,990
"Niliposikia wenzetu eti watagawanya nchi hii vipande vipande nilishangaa sana, tulipopata uhuru Baba wa Taifa alituweka pamoja kwa maana ya kwamba umoja ni nguvu, unapomsikia mtu anasema akipata madaraka atagawanya vipande, jua wanapotaka kutupeleke siko" Dkt. Magufuli
"Kusema kila jimbo lijitegemee ni kuirudisha nyuma Tanzania na kukuza ukabila, madhara yake majimbo yaliyo masikini yatakuwa masikini zaidi. Kataeni masuala ya majimbo, wakoloni walipotaka kuitawala duniani waligawanya majimbo" Dkt. Mgombea wa Urais kupitia CCM
"Kwenye ilani yao ukurasa wa 84 inasema kuwa, wakipata madaraka madini yetu watayaweka rehani, kwa neno walilolitumia kuwa ni dhamana. Yaani watachukua madini yetu kuwapa watu, wachimbe na kuuza" Dkt. Magufuli
"Leo wenzetu wanasema wataweka dhamana ya madini yetu, kesho watasema wanaweka dhamana mbuga zetu hata na wake zetu. Tunarudi kwenye utumwa, ni mambo ya ajabu sana" Dkt. Magufuli akiwa Itigi