Rais Magufuli afanya uteuzi, Sophia Simba aula, awa mwenyekiti wa bodi ya Magavana

Status
Not open for further replies.

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,895
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wenyeviti wa bodi za taasisi 5 za Serikali baada ya wenyeviti waliokuwa wakiongoza bodi hizo kumaliza muda wao na wengine kuteuliwa katika nyadhifa nyingine.

  1. Mhe. Rais Magufuli amemteua Prof. Charles Anael Mkonyi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Mifupa (MOI). Prof. Mkonyi ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi (MUHAS).
  2. Mhe. Rais Magufuli amemteua Bi. Mwamini Juma Malemi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Sukari.
  3. Mhe. Rais Magufuli amemteua Bi. Sophia Simba kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Magavana wa Taasisi ya Ustawi wa Jamii.
  4. Mhe. Rais Magufuli amemteua Dkt. Mwanza Kamata kuwa Mwenyekiti wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE). Dkt. Kamata amechukua nafasi iliyoachwa wazi na Mhandisi Christopher Chiza ambaye amechaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Buyungu.
  5. Mhe. Rais Magufuli amemteua Dkt. Maria Mashingo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Maendeleo (TIB). Dkt. Mashingo amechukua nafasi iliyoachwa wazi na Prof. Palamagamba Kabudi ambaye aliteuliwa kuwa Mbunge na baadaye kuwa Waziri wa Katiba na Sheria.
Uteuzi wa wenyeviti hawa wa bodi umeanza leo tarehe 22 Oktoba, 2018.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

22 Oktoba, 2018


d4a3ad88463a93ca9fe879e834ab8500.jpeg
 
Wafanye kazi wakileta mchezo Magu anaweza kuwaweka kando akamchukua hata Wenje ,maana chama chake kimemtupa sana,sasa hivi anaendesha lori LA Asas.Nape una mambo mengi sana ya kujifunza kutoka kwa mama Sophia
 
Ufanisi wa hao maprof na madokta tangu wameanza kuteuliwa ukoje.....?

BAU..... Unless he mean it for 10-15yrs down the line... Otherwise nawaona kawaida Sana....
Sophia Simba, nadhani amesubiri Sana baada ya msamaha..
 
Katiba hii ya 1977 ni ya ajabu sana; Rais akisema wote tulale nje hakuna wa kubisha wala wa kukimbilia mahakamani
 
Eti "ameula"..

As if kuna cha maana cha maslahi kwenye kazi za serikali...

Sema ameenda kuhudumu...

"Kuula" kwenye kazi za serikalini ni hali na tabia fulani hivi ya njaa na umasikini....

"Kuula" ni kufanya biashara na kufanikiwa nothing else!
 
Ndugu nauliza swali, kati ya magufuli na Dr Dau na mdini? Na kati ya Magufuli na Kikwete nani Mkanda au Mkabila.
 
Hivi Msigwa huwa haufanyi uhakiki wa unachoandika? Mfano, huyo anaitwa Dkt Ng’wanza Kamata, wewe unaandika Dkt Mwanza. Anyway hongera kwa wateule. Dkt Ng’wanza ni miongoni mwa wafuasi watiifu wa falsafa za mwl, mchapa kazi, mwenye weledi na hana tamaa, ni simple na mtu wa watu, kwa hapo Dkt Magufuli kachagua mtu safi.
Anajua biashara?! Nchi hii ina watu wenye IQ ndogo sana! Mtu akisikia tu Doctor basi anadhani ni bingwa ktk kila kitu! Mo Dewji ana Masters ya Georgetown University au Alhaji Aliko Dangote ana elimu ya kawaida lakini uliza "Wealth" walio create! Unampa mtu kusimamia biashara za Kimataifa huku hajawahi hata kuendesha genge mtaani! Poor Tanzania!
 
Hivi Msigwa huwa haufanyi uhakiki wa unachoandika? Mfano, huyo anaitwa Dkt Ng’wanza Kamata, wewe unaandika Dkt Mwanza. Anyway hongera kwa wateule. Dkt Ng’wanza ni miongoni mwa wafuasi watiifu wa falsafa za mwl, mchapa kazi, mwenye weledi na hana tamaa, ni simple na mtu wa watu, kwa hapo Dkt Magufuli kachagua mtu safi.
Anajua biashara?! Nchi hii ina watu wenye IQ ndogo sana! Mtu akisikia tu Doctor basi anadhani ni bingwa ktk kila kitu! Mo Dewji ana Masters ya Georgetown University au Alhaji Aliko Dangote ana elimu ya kawaida lakini uliza "Wealth" walio create! Unampa mtu kusimamia biashara za Kimataifa huku hajawahi hata kuendesha genge mtaani! Poor Tanzania!
 
Anajua biashara?! Nchi hii ina watu wenye IQ ndogo sana! Mtu akisikia tu Doctor basi anadhani ni bingwa ktk kila kitu! Mo Dewji ana Masters ya Georgetown University au Alhaji Aliko Dangote ana elimu ya kawaida lakini uliza "Wealth" walio create! Unampa mtu kusimamia biashara za Kimataifa huku hajawahi hata kuendesha genge mtaani! Poor Tanzania!

Sijui kama kuna Lumumba affiliated atakaelewa ulichokiandika hapa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom