Rais kushindwa kutumia gari la wazi leo Dodoma ni ishara kuwa hatuko salama au ametishwa?

Raisi Magufuli hata akiamua kutembea kwa miguu saa sita ya usiku hakuna mtu atakaye mdhuru, kwa sababu ni raisi anayependwa sana na wanyonge.
mwambie ajaribu leo,atembee kuanzia magogoni mpaka posta ya zamani tuone,
 
Katika maisha yangu ndani ya siasa hasa wakati nikiwa mtumishi wa makao makuu ya Chadema tena niliyeaminika kuwa simuungi mkono Mwenyekiti bali ni kijana wa Zitto, nilijifunza kuwa hakuna watu wanaokuza mambo kama Walinzi wa viongozi wakati huo (Redbrigade)

Walinzi wanapenda kumuweka kiongozi mkuu katika hali ya hofu kubwa ili wapate kazi ya kufanya. Kipindi kile utasikia "mwenyekiti CCM wameandaa kama vijana mia tatu hivi so tunahitaji fungu la kazi maalum kuwafuatilia n.k ". Ukija kwenye vikao utasikia "Mwenyekiti mambo ya ulinzi ni very sensitive hatuwezi kuyaongea hapa hata bajeti yetu hatuwezi kuiwasilisha hapa tutakufuata tukupe details ila hali ni mbaya sana tunawindwa sana na hata humu ndani hatuko salama kuna watu humu sio wenzetu". Ukishasikia hivyo ujue wakienda kumuona huko faragha wewe unayeonekana kuwahoji na kuwapinga wanakubebesha usaliti kwa Mwenyekiti na kwasababu ya hofu wanayompa na wanavyomlinda asikutane na mtu mwingine ujue atawaamini tu na kuwaidhinishia fedha wanazotaka.

Sisemi vyombo vyetu vya ulinzi na usalama havina uadilifu kama hawa niliowaona hapana ila reporting ya walinzi huwa inatia hofu sana viongozi labda ni kwasababu ya uzito wanaoutoa kila wanapoona dalili za tishio.

Tangu Rais Magufuli aingie madarakani nimekuwa nikishuhudia ulinzi wa hali ya juu sana kiasi kwamba hadi unanikera mimi binafsi kama mshabiki wake. Sioni kwanini wamzongezonge Rais kiasi hicho wakati anawapenzi na mashabiki wengi sana huenda kuliko watangulizi wake kwa mtazamo wangu. Ndipo huwa napata mashaka kuwa wanataka kumtia hofu bure hasa ikizingatiwa amechukua hatua ngumu kwenye baadhi ya mambo.

Hili la leo ndio limenikwaza zaidi kiasi kwamba nahisi kuna siku Rais hatahudhuria matukio muhimu kwasababu tutakazoambiwa ni za kiusalama. Na je mbona Rais na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama kila siku wanasema tuko SALAMA ila linapokuja swala la Rais tunaona vinginevyo?

Mwenyekiti wangu Mbowe aligombanishwa na kila mtu mzuri kwake na hawa hawa walinzi kwa kumjengea hofu na vitisho vingi mpaka mwisho wa siku amebaki amezungukwa na WANAFIKI na Wasaka FURSA. Rais wangu nae napata wasiwasi nae anaweza kufikishwa huko kwa kisingizio tu kuwa ana MAADUI wengi.

Mimi kama mwananchi sipendi Rais anavyozongwazongwa na tukio la leo ndio sijalipenda kabisa naomba Rais nae asikubali kubanwa kiasi hiki wananchi tunakerekwa. Na siamini kama ana maadui wengi kiasi hicho. Mtaani anapendwa sana. Ajiachie tu afanye kazi zake kwa Uhuru.

Mtamfuatilia JPM mpaka mtachoka. Hiyo ilikuwa ni security arrangement ya siku hiyo. Zinabadilika kila kukicha. Hata walinzi wanabadilika. Mambo mengi yanabadilika. Leo akiamua aendeshe bila motorcade mtakuja humu tena kutusumbua na maswali. Yeye ni Mkuu wa nchi walinzi wake wanafanya kazi yao. Wape hongera yao.
 
hii yote ni hofu ya maandamano maskin rais wetu...[HASHTAG]#mange[/HASHTAG] alikuwa anataka kuharibu ugal wa msukuma wa watu
 
Ukiona mtu ni muoga sana tambua hajiamini katika kila afanyalo, mimi ningekuwa Rais hata walinzi ningewaweka kando Mungu anatosha, ukiwa mtenda haki utapendwa tu na utaishi kwa amani kuu
 
Au kuna mpango uliokua unaufahamu hivyo umeshangaa kuona hajatumia gari la uwazi kama mlivyotegemea??
 
yaani unataka wasimlinde raisi kwann??
ww hujui huyu ndiye raisi anayechukiwa sana na RAIA waliomchagua kuliko maraisi wote walowahi kupita???!


Asilimia kubwa y watanzania wanampenda sana Rais na wako tayari kufa kwa ajili yake.....wanaolia n kulalamika ni kwa sababu wamebanwa na hawajuwi watapumulia wapi. Wache wafe tu.
 
Katika maisha yangu ndani ya siasa hasa wakati nikiwa mtumishi wa makao makuu ya Chadema tena niliyeaminika kuwa simuungi mkono Mwenyekiti bali ni kijana wa Zitto, nilijifunza kuwa hakuna watu wanaokuza mambo kama Walinzi wa viongozi wakati huo (Redbrigade)

Walinzi wanapenda kumuweka kiongozi mkuu katika hali ya hofu kubwa ili wapate kazi ya kufanya. Kipindi kile utasikia "mwenyekiti CCM wameandaa kama vijana mia tatu hivi so tunahitaji fungu la kazi maalum kuwafuatilia n.k ". Ukija kwenye vikao utasikia "Mwenyekiti mambo ya ulinzi ni very sensitive hatuwezi kuyaongea hapa hata bajeti yetu hatuwezi kuiwasilisha hapa tutakufuata tukupe details ila hali ni mbaya sana tunawindwa sana na hata humu ndani hatuko salama kuna watu humu sio wenzetu". Ukishasikia hivyo ujue wakienda kumuona huko faragha wewe unayeonekana kuwahoji na kuwapinga wanakubebesha usaliti kwa Mwenyekiti na kwasababu ya hofu wanayompa na wanavyomlinda asikutane na mtu mwingine ujue atawaamini tu na kuwaidhinishia fedha wanazotaka.

Sisemi vyombo vyetu vya ulinzi na usalama havina uadilifu kama hawa niliowaona hapana ila reporting ya walinzi huwa inatia hofu sana viongozi labda ni kwasababu ya uzito wanaoutoa kila wanapoona dalili za tishio.

Tangu Rais Magufuli aingie madarakani nimekuwa nikishuhudia ulinzi wa hali ya juu sana kiasi kwamba hadi unanikera mimi binafsi kama mshabiki wake. Sioni kwanini wamzongezonge Rais kiasi hicho wakati anawapenzi na mashabiki wengi sana huenda kuliko watangulizi wake kwa mtazamo wangu. Ndipo huwa napata mashaka kuwa wanataka kumtia hofu bure hasa ikizingatiwa amechukua hatua ngumu kwenye baadhi ya mambo.

Hili la leo ndio limenikwaza zaidi kiasi kwamba nahisi kuna siku Rais hatahudhuria matukio muhimu kwasababu tutakazoambiwa ni za kiusalama. Na je mbona Rais na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama kila siku wanasema tuko SALAMA ila linapokuja swala la Rais tunaona vinginevyo?

Mwenyekiti wangu Mbowe aligombanishwa na kila mtu mzuri kwake na hawa hawa walinzi kwa kumjengea hofu na vitisho vingi mpaka mwisho wa siku amebaki amezungukwa na WANAFIKI na Wasaka FURSA. Rais wangu nae napata wasiwasi nae anaweza kufikishwa huko kwa kisingizio tu kuwa ana MAADUI wengi.

Mimi kama mwananchi sipendi Rais anavyozongwazongwa na tukio la leo ndio sijalipenda kabisa naomba Rais nae asikubali kubanwa kiasi hiki wananchi tunakerekwa. Na siamini kama ana maadui wengi kiasi hicho. Mtaani anapendwa sana. Ajiachie tu afanye kazi zake kwa Uhuru.
Hivi umeandika ukiwa na akili timamu kabisa au umetoka milembe?
Eti anapendwa sana ,nahisi ulihusika kumuua Ben Saanane sasa damu yake inakutesa.
magufuli ndo rais wa mwisho kuitawala Tanzania chini ya ccm,kama huamini omba uzima utaona.
 
Hivi umeandika ukiwa na akili timamu kabisa au umetoka milembe?
Eti anapendwa sana ,nahisi ulihusika kumuua Ben Saanane sasa damu yake inakutesa.
magufuli ndo rais wa mwisho kuitawala Tanzania chini ya ccm,kama huamini omba uzima utaona.
Binafsi siamini kama magufuli ndio pekee anaweza kuhusika na swala la Ben Saanane. Its 50/50 maana nimefanya kazi na Ben Saanane namuelewa vizuri na hata mahusiano yake na aliokuwa anafanya nao kazi nayajua. Nitaandika maoni yangu kuhusu hili siku moja.
 
Huu ni utahira kudhani rais ameogopa.
Kwanza gari hilo la wazi hupandia pale uwanja.
Sasa kwanini ahofie maisha yake kwenye gari la wazi, wakati amekagua gwaride!?
Au alikagua pia akiwa ndani ya gari bullet proof!?
 
Kwa wingi huo unaousema stil mkashindwa kuingia barabarani leo kumuondoa? what a joke


Hukumuelewa Mange?maandamano yamefanikiwa kwa upande wake,we unadhani yeye ni mgeni na watanzania?kwamba hakujua kuwa watu hawatasndamana?!!!!

Lengo lake halikuwa kuwaona watu barabaran bali alitaka kuona serikali ina react VIP??umegundua serikali imereact VIP

Angalia Malaika mkuu alivokuwa na ulinz
mkali Jana pale Dodoma

Angalia police force Tanzania walivoandamanishwa barabaran karibia miji yote Tanzania na I guess walilipwa posho zao

Ona nguvu waloitumia wabunge na hata Mr jiwwe kukemea na kutisha wananchi watakaoandamana

haya yote yanaonesha Kuwa SHUJAA KIMAMBI anawajua vizur watanzania na maandamano yaliandaliwa ili kumsumbua
MR JIWWE!
 
Nia ya andiko naona si ulinzi wa rais bali kueleza yaliokukuta ulipokuwa CDM. Pole tu we pambana na hali yako, CDM iache iendelee na mambo yake.
 
Back
Top Bottom