Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,484
- 30,162
Nimestuka sana nilipoisikia kauli aliyotoa mkuu wetu wa mkoa wa Dar tena kanisani, kuwa tarehe 24, "anawaagiza" askari Polisi 5,000 na askari wa JWTZ 8,000 wajitokeze mitaani Dar, ili wafanye usafi!
Kustuka kwangu ni kuona Mkuu wa Mkoa, asivyoelewa majukumu ya Hawa walinxi wetu, Kwa kuwa Jeshi la Polisi nchini, wajibu wake namba moja ni kuwalinda Rais na Mali zao na JWTZ wajibu wao namna moja ni kulinda mipaka ya nchi yetu.
Nimuulize Mkuu wa Mkoa, Chalamila, hivi Kwa kuwataka hao Polisi wetu na askari wa JWTZ wafanye usafi wa Jiji, siyo kukiuka Katiba ya nchi?
Huyu aliyetoa kauli hii ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama wa mkoa wa Dar na pia ameitoa kauli hiyo akiwa kanisani na ametoa kauli hiyo, baada ya kumsikia Mwenyekiti wa Chama kikuu Cha siasa nchini Cha Chadema, kutoa kauli kuwa hiyo tarehe 24 watafanya maandamano ya amani, ambayo ni haki yao kikatiba kwa kuitaka serikali kuiondoa bungeni miswada 3 ya Sheria, Kwa kuwa hiyo miswada ni kiini macho!
Huyo Chalamila ndiye anayejaribu kuivunja Katiba ya nchi waziwazi Kwa kutaka kuleta taharuki nchini, Kwa kuwa siku hiyo aliyoyaagiza majeshi ya ulinzi nchini yaingie mitaani na kufanya usafi, ndiyo siku hiyohiyo ambayo Mwenyekiti wa Chadema ametangaza kuwa wanategemea kufanya maandamano ya amani.
Najua kuwa Chalamila, ametoa kauli hiyo ili kuwatisha wafuasi wa Chadema, wanaotarajia kuandamana siku hiyo, waingie hofu ya kuandamana.
Yeye Chalamila anajua fika kuwa taarifa aliyotoa Mwenyekiti wa Chadema, ni halali kabisa, Kwa kuwa ndani ya Katiba yetu ya nchi, inaruhusu kufanyika maandamano ya amani.
Hivi tukisema kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar, ndiye anayetaka kuleta uvunjifu wa amani ya nchi hii, nitakawa nakosea kweli?
Nimalizie Kwa kusema kuwa, kama amani ya nchi hii itapotea, basi Mkuu wa Mkoa wa Dar, awajibike Kwa kuitumbukiza nchi hii kwenye umwagaji wa damu.
Tunamwomba Mungu aendelee kuilinda nchi hii, kutokana na hao viongozi wa Chama tawala na serikali yao, kutokana na hila zao za wakati wote za kutaka kuendelea kuitawala nchi hii bila kutaka kuondoka madarakani Kwa amani
Kustuka kwangu ni kuona Mkuu wa Mkoa, asivyoelewa majukumu ya Hawa walinxi wetu, Kwa kuwa Jeshi la Polisi nchini, wajibu wake namba moja ni kuwalinda Rais na Mali zao na JWTZ wajibu wao namna moja ni kulinda mipaka ya nchi yetu.
Nimuulize Mkuu wa Mkoa, Chalamila, hivi Kwa kuwataka hao Polisi wetu na askari wa JWTZ wafanye usafi wa Jiji, siyo kukiuka Katiba ya nchi?
Huyu aliyetoa kauli hii ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama wa mkoa wa Dar na pia ameitoa kauli hiyo akiwa kanisani na ametoa kauli hiyo, baada ya kumsikia Mwenyekiti wa Chama kikuu Cha siasa nchini Cha Chadema, kutoa kauli kuwa hiyo tarehe 24 watafanya maandamano ya amani, ambayo ni haki yao kikatiba kwa kuitaka serikali kuiondoa bungeni miswada 3 ya Sheria, Kwa kuwa hiyo miswada ni kiini macho!
Huyo Chalamila ndiye anayejaribu kuivunja Katiba ya nchi waziwazi Kwa kutaka kuleta taharuki nchini, Kwa kuwa siku hiyo aliyoyaagiza majeshi ya ulinzi nchini yaingie mitaani na kufanya usafi, ndiyo siku hiyohiyo ambayo Mwenyekiti wa Chadema ametangaza kuwa wanategemea kufanya maandamano ya amani.
Najua kuwa Chalamila, ametoa kauli hiyo ili kuwatisha wafuasi wa Chadema, wanaotarajia kuandamana siku hiyo, waingie hofu ya kuandamana.
Yeye Chalamila anajua fika kuwa taarifa aliyotoa Mwenyekiti wa Chadema, ni halali kabisa, Kwa kuwa ndani ya Katiba yetu ya nchi, inaruhusu kufanyika maandamano ya amani.
Hivi tukisema kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar, ndiye anayetaka kuleta uvunjifu wa amani ya nchi hii, nitakawa nakosea kweli?
Nimalizie Kwa kusema kuwa, kama amani ya nchi hii itapotea, basi Mkuu wa Mkoa wa Dar, awajibike Kwa kuitumbukiza nchi hii kwenye umwagaji wa damu.
Tunamwomba Mungu aendelee kuilinda nchi hii, kutokana na hao viongozi wa Chama tawala na serikali yao, kutokana na hila zao za wakati wote za kutaka kuendelea kuitawala nchi hii bila kutaka kuondoka madarakani Kwa amani