Rais kumzawadia mtoto pipi alikuwa na maana gani?

5648d1250818172-rais-kumzawadia-mtoto-pipi-alikuwa-na-maana-gani-8d6u9682-2-.jpg


Kiukweli mimi binafsi, nimeshitushwa na nimeshangaa na kujiuliza maswali mengi mno baada ya kuona picha ya Rais akimzawadia mtoto Pipi. nimejiuliza maswali mengi kuwa kwa mfano huo anataka sisi tujifunze nini? au alikuwa na maana gani? na kwanini afanye hivyo.... na je alikuwa na uhakika kama huyo mtoto alikuwa amekwisha kula chakula ama anauhakika wa chakula baada ya hapo? Vp kuhusu afya yake namuona kama anamapunye kichwani kama nimeona vizuri, vp kuhusu uhakika wake wa elimu? mimi nahisi mtoto kama huyo anatakiwa kuzawadiwa uhakika wa elimu na sio pipi kama alivyo fanya rais. Na kwa mtizamo huu hivi kweli matabaka yatakwisha , hivi kweli jamani maisha bora kwa kila mtanzania yanaletwa kwa kugawa pipi?


Anagawa pipi ili apendwe.

Ni dhahiri hafikirii au kujiuliza maswali uliyoyaweka hapo juu. Yeye hayuko hivyo ambavyo ungemtegemea awe. This displays who he really is.
 
Huyo mtoto alitakiwa awepo darasani anasoma; na si kupokea pipi. Hiyo picha inaonesha INEQUALITIES ni tatizo linalokuwa kwa kasi sana ndani ya TZ. Rais yupo kwenye gari la kifahari + msafara wa wapambe; halafu huyo mtoto hata viatu hana. Sasa hivi kuna tofauti kubwa sana kati ya maskini (mlalahoi) na mtu wa middle class ndani ya TZ.
Kama ilikuwa jumamosi au jumapili huyo mtoto atakuwa darasa la nani?
 
Kufuatia hiyo picha kwenye post ya kwanza, can you tell what was the conversation like kwenye hii picha hapa chini?

attachment.php


Picha ilipigwa 2008
 

Attachments

  • Rais Kikwete.jpg
    Rais Kikwete.jpg
    14.1 KB · Views: 113
Mnyimeni JK sifa zote lakini hili la kujichanganya kirahisi kabisa na watu wa kawaida hana mfano. Iwe misiba, harusi, JK yupo.
 
5648d1250818172-rais-kumzawadia-mtoto-pipi-alikuwa-na-maana-gani-8d6u9682-2-.jpg


Kiukweli mimi binafsi, nimeshitushwa na nimeshangaa na kujiuliza maswali mengi mno baada ya kuona picha ya Rais akimzawadia mtoto Pipi. nimejiuliza maswali mengi kuwa kwa mfano huo anataka sisi tujifunze nini? au alikuwa na maana gani? na kwanini afanye hivyo.... na je alikuwa na uhakika kama huyo mtoto alikuwa amekwisha kula chakula ama anauhakika wa chakula baada ya hapo? Vp kuhusu afya yake namuona kama anamapunye kichwani kama nimeona vizuri, vp kuhusu uhakika wake wa elimu? mimi nahisi mtoto kama huyo anatakiwa kuzawadiwa uhakika wa elimu na sio pipi kama alivyo fanya rais. Na kwa mtizamo huu hivi kweli matabaka yatakwisha , hivi kweli jamani maisha bora kwa kila mtanzania yanaletwa kwa kugawa pipi?

Mkuu mbona hii kali sana... Rais kumzawadia(kumpa) mtoto pipi akiwa njiani sioni kama ni kitu cha kudiscuss kwa hisia hivyo. Hata kama angemzawadia chakula, maisha bora na elimu sidhani kama ndio yangeishia hapo maana Tanzania ina watoto wengi sana wanoishi katika mazingira magumu...
Ni wangapi wakienda kumtembelea ndg au rafiki na akakuta watoto huwapa zawadi za pipi/chocolate au ice cream? Mbona kwa Rais inakuwa nongwa? Rais ni binadamu kama wengine na kumpa mtoto zawadi ni kwa kupenda kuonyesha upendo wake kwa watoto....

Tujaribu kuwa na rational thinking sometimes.... coz above all we are still HUMANS!!
 
5648d1250818172-rais-kumzawadia-mtoto-pipi-alikuwa-na-maana-gani-8d6u9682-2-.jpg


Kiukweli mimi binafsi, nimeshitushwa na nimeshangaa na kujiuliza maswali mengi mno baada ya kuona picha ya Rais akimzawadia mtoto Pipi. nimejiuliza maswali mengi kuwa kwa mfano huo anataka sisi tujifunze nini? au alikuwa na maana gani? na kwanini afanye hivyo.... na je alikuwa na uhakika kama huyo mtoto alikuwa amekwisha kula chakula ama anauhakika wa chakula baada ya hapo? Vp kuhusu afya yake namuona kama anamapunye kichwani kama nimeona vizuri, vp kuhusu uhakika wake wa elimu? mimi nahisi mtoto kama huyo anatakiwa kuzawadiwa uhakika wa elimu na sio pipi kama alivyo fanya rais. Na kwa mtizamo huu hivi kweli matabaka yatakwisha , hivi kweli jamani maisha bora kwa kila mtanzania yanaletwa kwa kugawa pipi?

Naona huyu jamaa amewachosha kweli kweli, ndo maana kila anachofanya mnakiona kibaya. Kumpa mtoto pipi ni ishara ya upendo jamani, maana hatujui baada ya pipi labda kuna vitu vingine alivyompa ambavyo havikuonekana hapa kwenye picha. Na si kila baba anayetoa pipi kwa mtoto inamaanisha ni fataki. Mimi sioni ubaya wowote kwa rais kutoa zawadi ya pipi kwa mtoto. Kuhusu kulazimisha kupendwa c kweli, mbona huyu baba anapendeka tu. Na hakuna atakaye chukua kiti cha urais 2010 zaidi yake, eti wana jf nyie mmeshaona jamani!!
 
Mr.President hajakosea kitu pale...wewe unafikiri yule mtoto angepewa penseli au kalamu si angeipoteza tu lakini pipi ataila na ataiona tamu kishenzi..kwanza lile ni tukio la kihistoria kwake ..na suala la shule ni la mzazi wa yule mtoto la wala sio la Rais.

Katika yote hilo la bold ndio la msingi zaidi.
 
watanzania tunapena sana kuchonga kwa saaaanaa tu! kikwete ni mzazi kama wazazi wengine,ulitaka amwulize maswala ya kuulizwa na mjumbe wake au mzazi wake?au ampelekee lunch?atawapa wangapi?Ni upendo tu jamnai, asipoongea na watu mtasema oooh anajifungia kwenye gari hawathaimi wanyonge, akijichanganya nao ooh amempa pipi, sasa watz tunataka mtu aweje?afanye nini mumpende?nae analipwa km wewe na mimi so salary yake ni yeye na family yake so kugawia watu lunch au hela njiani,so alichoanya ni upendo wa kibaba,tena kwa mtoto maskini,katoto katasimulia maisha yake yote,na may katapata changamoto ya kusoma zaidi amfikie aliempa pipi!! asanteni
 
Ukiwa rahisi wa Nchi lazima uwe na code of conduct.....kwanini asingepunga mkono tu na kuishia zake.....! Nikiwa kijijini kwetu kule mji mwema mimi ni kama rahisi sigawi pipi wala kuuza sura, hapo si ajabu Mkwere anataka aingie kwenye Guiness book of records rahisi aliyegawa pipi....this is very low.....hajui kama mtoto amekula, anasafura, minyoo....afanye vitu tangible si kugawa pipi ebo.....
 
Sioni ubaya wowote kwa yeye kugawa peremende. Watu wengine mko criticism happy na mtakosoa chochote tu kile akifanyacho au akisemacho. Hoja ambayo ina maana kidogo labda ni kwenye suala la usalama ingawaje hata hilo mimi sioni kama kuwa ni tatizo. Kwanza picha yenyewe haitupi wide view ya kuweza kuona kama kulikuwa na mlinzi pembeni ya hilo gari.

Ukiangalia vizuri chini mkono wa kulia wa hiyo picha utaona kitu ambacho pengine ni mkono wa mtu aliyevaa Kaunda suti anayeweza kuwa mlinzi. Kwa ujumla sioni ubaya yeye kugawa hivyo viutamu. Kumkosoa kwa hilo ni petty!!!!
 
Sijaona tatizo katika hili, JK kama mzazi mwingine yeyote kampa alichokuwa nacho mkononi kwa wakati huo, ingekuwa ni mwaliko fulani hivi halafu akamuandalia mtoto zawadi ya pipi, hapo angalau tungejiuliza.
 
..hajui kama mtoto amekula, anasafura, minyoo....afanye vitu tangible si kugawa pipi ebo.....

Watu wengine mahepe ,sasa mtoto ana safura au minyoo ,yeye imemuhusu nini ? Maana kwa hivyo mnavyofikiria ,sijui mtoto hajashiba au ananjaa sioni hoja hiyo kunhusisha na Raisi mpita njia tu !!

Zipo hoja za kuhoji lakini si hali ya mtoto ambayo inahitaji daktari kujua yote hayo.

Tatizo WaTanganyika hamtosheki ,hivi mlitaka agawe gari moshi ,pipi ni kitu maarufu kwa watoto wote duniani na si kiongozi kumgaia mtoto lakini hata wapita njia wengine huwa wakipita kwenye kikundi cha watoto na akafurahi nao anaweza kuwagaia chochote ambacho kipo karibu yake na kinalingana.Hapahitajiki milioni katika kufanya ibada hiyo.

Yaani kama Raisi angekasilika kwa mtoto kuigusa gari yake hapo ningelalamika maana wapo watu hawataki gari zao ziguswe wala kuegemewa.

Mnachosha sana ,hivi mngeona anatoa fedha mngesemaje ? anatumia hela kifisadi ,najua msingekosa la kusema.

Ila naona amejua wa kumpa pipi kama angempa mtu mzima ela,basi mtu huyo angeenda kuponda na kuzarau huku hela ametia mfukoni akiipangia cha kununua.
 
Watu wengine mahepe ,sasa mtoto ana safura au minyoo ,yeye imemuhusu nini ? Maana kwa hivyo mnavyofikiria ,sijui mtoto hajashiba au ananjaa sioni hoja hiyo kunhusisha na Raisi mpita njia tu !!
Sasa pipi mtoto zinamsaidia nini? JK hujaza mapipi kwenye gari kugawia watoto.....!
 
Mie silaani wala simpongezi.

Ila ingelikuwa BUSARA kama Kikwete angelijenga kiwanda cha PIPI na chocolate ili WAZAZI wa hao watoto wapate kazi na watoto wawe na uwezekano wa kuzila hizo pipi na mabiskuti mara kwa mara. Sasa ukimpa siku moja na kutoweka kama vumbi la gari lako, utakuwa umetoa msaada gani?

Kama RAIS na awape watu NDOANO na si SAMAKI. Nafikiri watu wanaolaani, wanalaani kwa hilo. Kama angelikuwa kafika na kununua hizo pipi kwenye kiwanda hapo mjini na kuzigawa, tungeliona kafanya la maana kwani kiwanda kimeuza Pipi, wazazi watapata kazi zaidi ya kuzalisha nyingine na watoto siku hiyo wamepata pipi, na mwisho wa mwezi wazazi wakipata mshahara, wataweza kuwanunulia watoto Pipi nyingine.
 
Back
Top Bottom