Rais Kikwete Matibabu Marekani: Story ya Jaribu Ujinga

Hussein Massanza

JF-Expert Member
Dec 26, 2012
918
1,994
10730794_10152559197966225_2573629083854848739_n.jpg




Ukiona elimu ni ghali jaribu ujinga! Ni msemo maarufu sana, kwamba ukiona elimu ni bei mbaya, basi baki upande wa pili ukutane na gharama za ujinga zilivyo kubwa. Hii ina maana pia kuwa ukiona kinga zinagharimu sana, jaribu maradhi uone.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, yupo nchini Marekani kwa matibabu. Amefanyiwa upasuaji wa tezi dume (prostate) katika Hospitali ya Johns Hopkins, iliyopo Baltimore, Jimbo la Maryland.

Kwa kitendo cha Mkuu wa Nchi kutibiwa Marekani, baadhi ya wana wa taifa la lawama (Tanzania), wanalalamika, eti kwa nini wakubwa wanatibiwa nje ilhali hali za hospitali hapa nchini ni mbaya. Hawa wanaona gharama za kumtibu rais wa nchi ni kubwa, wanahitaji kuona matokeo ya upande wa pili.

Wapo wanasiasa (sishangai, ni kawiada yao), kuna watu mbalimbali pia wanakosoa Rais Kikwete kutibiwa Marekani. Kichekesho; eti wanataka atibiwe Amana, Mwananyamala au Temeke kisha apewe rufaa kwenda Muhimbili. Anayejadiliwa hivi ni mkuu wa nchi!

Kabla ya kuwaza ubora wa matibabu, tufikirie tu mazingira halisi. Mathalan; Rais Kikwete angetibiwa Muhimbili, je, wakosoaji wanajua gharama ambazo wananchi watazipata kwa kitendo cha mkuu huyo wa nchi kulazwa hospitali hiyo ya taifa?

Hivi, wanadhani JK akilazwa Muhimbili, wananchi watakuwa wanaweza kuingia na kutoka pale hospitali kwa uhuru kama ilivyo sasa? Wakosoaji wanajua mfumo wa kumlinda Rais wa Nchi ulivyo? Hawa nao wanataka kujaribu ujinga.

Wakosoaji hawajui kuwa JK kulazwa muhimbili, ingeweza kusababisha vifo vya wananchi wasio na hatia kutokana na kucheleweshwa kuanzishiwa tiba. Muda ambao mgonjwa mahututi angeshughulikiwa matibabu Kitengo cha Dharura (Emergency Unit) kuokoa maisha yake, angekuwa anapitishwa kwenye mashine za ukaguzi wa kiusalama. Hawatakufa watu hapo?

Hata hivyo, najua kuwa JK angetibiwa Muhimbili bado malalamiko yasingekosekana. Kuna ambao wangelaumu kwa sababu upatikanaji wa matibabu ungekuwa wa shida kutokana na mfumo wa ulinzi ambao ungeboreshwa hospitalini hapo. Ulinzi kwa Mkuu wa Nchi haukwepeki. lazima alindwe sana.

Walalamikaji hao, si ajabu ndiyo haohao wakosoao JK kufanyiwa upasuaji Marekani, wangetamka: "Kwa nini hajapelekwa nje akatibiwe?" Wangesonya na kuzungumza kwa jazba kwamba anasababisha foleni kubwa ya kupata matibabu Muhimbili.

Wengine wangebeza; je, taifa limefikia hali ya kutojiweza kiuchumi kiasi cha kushindwa kumpatia Mkuu wa Nchi matibabu ya uhakika katika mataifa yaliyopiga hatua kubwa kwenye nyanja ya utoaji wa huduma za afya? Kila eneo litakosolewa!

Vilevile JK angetibiwa hapa nchini, wapo ambao wasingeacha kuibuka na hoja kuwa "anajikosha kwa wananchi", aonekane anaishi maisha ya kawaida wakati siyo kweli hata kidogo. Unaweza kumzuia mwana wa lawama? Anayekuwinda hakosi sababu ya kukusema!


SHANGAA WATANZANIA:


Mwaka jana, Rais Marekani, Barack Obama, aliwasili nchi kwa ziara ya siku mbili. Tulikuwa mashuhuda jinsi ambavyo Marekani ilivyotumia mamilioni ya dola (mabilioni ya shilingi), kuhakikisha kiongozi wao huyo hapatwi na janga lolote akiwa nchini.

Tena Watanzania tulishangilia kweli; "Dah, Marekani kiboko, rais wao analindwa si mchezo", magazeti ya Tanzania yakaandika "ulinzi wa Obama balaa", mengine "Obama anavyolindwa ni funga kazi", yaani tunakuwa mashabiki wa jinsi Marekani wanavyomlinda rais wao, sisi wa kwetu hatutaki apate huduma bora za afya! Sisi Watanzania ni watumwa?

Utumwa si mpaka uchukuliwe mateka au ununuliwe kwenda kufanya kazi za watu bila uhuru binafsi. Upo utumwa wa fikra ambao Watanzania tunaamua kuupokea na kuufanya ni utaratibu wetu. Swali; Kifo cha Obama au JK, kipi kina gharama kubwa kwa Watanzania?

Marekani wanatambua gharama ambayo wanaweza kuipata kwa kumpoteza kiongozi wao ndiyo maana wanamlinda hivyo. Nasi tunageuka mashabiki wa huo ulinzi ambao rais wa taifa hilo anapewa. Ila tunanung'unika rais wetu akipelekwa Marekani kutibiwa.

Yaliandikwa madege ya kijeshi ambayo yalitua Tanzania, likasifiwa lile manowari la kivita ambalo liliweka doria majini na rada zake kumulika anga lote. Walizungumziwa makomandoo wa FBI na utitiri wa majasusi CIA, yalizunguzwa magari bila kusahau lile Cadillac DTS Limousine (Cadillac One) linalombeba Obama.

Aliyekuwa Rais wa China, Hu Jintao, alitembelea Tanzania mwaka 2009. Japo ulinzi wake si wenye mbwembwe nyingi kama Marekani lakini tuliona jinsi ambavyo Wachina wanamlinda kiongozi wao. Ulinzi ni mkubwa sana kuhakikisha taifa lao haliingii hasara ya kumpoteza kiongozi wao.

Hata kiongozi wa China wa sasa, Rais Xi Jinping, mwaka jana baada tu ya kuchaguliwa na kabla hajaapishwa kulitumikia taifa hilo, alizuru Tanzania na tuliona ulinzi ambao Wachina waliutoa kwake. Yaani sisi tunapenda watoto wa nyumba jirani wanavyomlinda baba yao, ila sisi kumlinda baba yetu inakuwa nongwa.

Ilishatolewa taarifa rasmi kuwa inakuja zamu ya Urusi, lile taifa namba mbili kwa mbwembwe za Kijeshi duniani baada ya Barekani. Rais wao, Vladimir Putin atawasili nchini Februari mwakani. Kwa mara nyingine tutashangilia ulinzi ambao Warusi wanautoa kwa rais wao.

Sababu ya mataifa hayo kutumia gharama kubwa kulinda viongozi wao hata wanapokuwa nje ya mipaka ya nchi zao, si kwamba hawana imani na vyombo vya ulinzi na usalama katika mataifa ambayo wakuu wao wanatembelea, isipokuwa wanajua kuwa jukumu la kuwalinda wakuu wao ni lao wenyewe.

Yaani Marekani wampandishe Obama ndege halafu wampigie simu JK kumtaarifu kuwa yupo njiani na wanategemea ulinzi wa uhakika uliopo Tanzania, thubutu! Tena hiyo siyo Tanzania tu, hata anapokwenda Uingereza ambalo ni taifa swahiba damu na Marekani, bado ulinzi ni uleule. Anapokwenda Israel ni vilevile. Kwa kifupi ni kwamba dunia nzima, ulinzi ni huohuo.

Hata Obama anapozunguka ndani ya Marekani yenyewe, ulinzi unaboreshwa kwa kiwango cha juu sana. Tukumbuke pia Rais wa 43 wa nchi hiyo, George Bush alipotembelea Tanzania mwaka 2008, tuliona ulinzi wake. Vilevile Rais wa 42, Bill Clinton alipofika Arusha kwa mwaliko wa marehemu Mzee Nelson Mandela wakati wa kutia sahihi makubaliano ya kumaliza mgogoro wa kivita Burundi.

Kwa kifupi ni kwamba Marekani hutumia wastani wa dola milioni 50 (zaidi ya shilingi bilioni 80) katika ziara moja ya rais wao nje ya nchi. Ziara ya Rais Obama barani Afrika mwaka jana, iliigharimu Marekani dola milioni 100 (zaidi ya shilingi bilioni 160). Pesa zote hizo zinateketezwa kwa sababu moja kuu, lazima kiongozi wao alindwe.

Uingereza siyo tu kwamba inamlinda kwa nguvu zote Waziri Mkuu wao (sasa hivi David Cameron), bali inatumia fedha nyingi kumhudumia Malkia Elizabeth II pamoja na ukoo wote wa Kifalme, wao huo ni utamaduni wao na haulalamikiwi.

Kila mwaka Serikali ya Uingereza inatumia wastani wa pauni milioni 40, sawa na shilingi za Kitanzania bilioni 109 kuhudumia ukoo wa Kifalme (The Civil List). Vilevile Malkia Elizabeth II anapewa pauni milioni 8 (shilingi bilioni 22) kila mwaka, kwa ajili ya matumizi yake tu. Fedha hizo zinaidhinishwa pia na Bunge la Uingereza (House of Commons).

Hapa ni kuweka hoja sawa kwamba suala la kumhudumia Rais wa Nchi ni utamaduni wa mataifa yote ulimwenguni. Hata Wamarekani au Waingereza wakisikia Watanzania wanalalamika rais wao kutibiwa Marekani watashangaa!

Jambo baya ni matumizi mabaya ya fedha za umma, ila kama imeonekana JK akitibiwa Marekani ndiyo anapata huduma bora kabisa kwa nini asipelekwe? Kwa hali ambayo tayari nimeshaieleza, angetibiwa Tanzania gharama zake ni kubwa kuliko alipo Marekani.


ILA NYUMA YAKE KUNA HOJA YA MSINGI

Kwa upande wa pili, kuna hoja kuhusu hospitali zetu. Hali ni mbaya. Hili ndilo la kuwekewa mkazo. Kwa nini wagonjwa waendelee kulala chini mpaka leo tukielekea miaka 53 baada ya uhuru?

Ni kweli kwamba serikali imekuwa ikitenga bajeti kila mwaka kwa ajili ya kuboresha sekta ya afya. Hata hivyo, kasi yake ni ndogo na haiendani na mahitaji halisi ya wagonjwa ambao wamekuwa wakikabiliana na mazingira magumu ya huduma.

Tanzania haina uhaba wa madaktari, hilo halina ubishi. Tatizo kubwa ni vifaa vya utoaji huduma za afya. Matokeo yake kuna madaktari wapo nchini na hawana kazi kwa sababu aina ya magonjwa ambayo wamebobea kuyatibu, vifaa vyake vya ugunduzi na tiba havipo nchini. (Hii ni mada ambayo siku yake ikifika nitaichambua na kutaja majina ya madaktari ambao imebidi watibu magonjwa mengine na kuacha yale waliyobobea.)

Kutokana na ukosefu wa vifaa, serikali kupitia wizara ya afya na hata Mfuko wa Bima ya Afya ya Tifa, imekuwa ikilazimika kutumia fedha nyingi kuwadhamini wagonjwa kwenda kutibiwa India na nchi nyinginezo, ikiwemo Afrika Kusini.

Kadhalika, serikali imekuwa ikilazimika kupeleka viongozi mbalimbali kutibiwa nje, hata katika magonjwa ambayo ingewezekana kabisa kuwatibu nchini. Hii yote ni kwa sababu ya mazingira ya utoaji wa huduma za afya nchini bado ni duni.

Serikali iboreshe huduma. Hata hivyo, kilio hicho hakipaswi kufikia hatua ya kutaka na Rais Kikwete naye atibiwe hapahapa. Hapo tunazungumzia habari nyingine. Hata kama vifaa na wataalamu wa kutosha wangekuwepo Muhimbili, ukweli ni kwamba angelazwa pale ingekuwa shida juu ya shida kwa wagonjwa wengine. Ulinzi wa rais ni kero kwa wananchi wa kawaida.

Mazingira ya Muhimbili kwa sasa na muundo wake kwa jumla, hautoshi kumlaza Rais wa Nchi pasipo kusababisha bughudha kwa wananchi wengine watakaokuwa wanakwenda kupata tiba, wagonjwa waliolazwa na ndugu zao wanaowahudumia au wanaokwenda kuwatembelea.

Tusiwe na ndoto kama za yule mbunge (nimemsahau jina), aliyetoa hoja bungeni Dodoma miaka 1990, kwamba Tanzania imefikia hatua iwe na treni ya umeme! Yaani umeme wetu wenyewe shida, tunawaza treni ya umeme. Ndiyo haya ya kutaka JK atibiwe Muhimbili. Je, tunataka kujaribu ujinga? Maana elimu tunaona ni ghali sana.

Luqman Maloto

 
Marais wote waliopita walienda matibabun nje ya nchi,hivi kwa Rais kikwete kimezidi nn kwenda matibabu nje ya nchi...? Tumeshuhudia wabunge wengi wanakwenda matibabu india, vp hao hawatumii kodi yetu vibaya.
 
Mtoa mada hoja yako dhaifu. Hivi Rais wetu ana maadui gani ambao wangepelekea Muhimbili isifikike kwa sababu za kiusalama? Gharama ya ulinzi ndani ya nchi na gharama ya safari kwenda marekani plus matibabu kipi kinazidi chenzake?

Kwa nini serikali isiboreshe mifumo ya hospitali zetu ili pia kwa kigezo chako dhaifu ziweze kutoa hizo executive services kwa viongozi kama Rais?
Nashangaa elimu unayojivunia ina tofauti gani na ujinga?

Watanzania nchi nzima hali zao ni mbaya kwa huduma duni,mbovu,na pia ukosefu wa vifaa tiba na madawa lakini rais anafanya anasa nje ya nchi,kwako wewe ni sawa tu!

Kinacholalamikiwa si ujinga maana rais angeenda nje ya nchi kwa maradhi ambayo kiutaalamu na kiuwezo wa hospitali zetu hayatibiki isingekua hoja. Lakin prostate gland inaweza kushughulikiwa na hospitali zetu bila shida. Kama si anasa ni nini?

Ifikie kipindi huo ujinga ulionao unaouchukulia werevu ukutoke ili nchi hii ithubutu kusema ina wasomi !

SI SAHIHI HATA KIDOGO RAIS KUWAACHA WATANZANIA WAKIFARIKI NA KUTESEKA KWA MAELFU KWA HUDUMA MBOVU ZA AFYA NA UKOSEFU WA MADAWA,NA YEYE KUKIMBILIA MAREKANI KWA MATIBABU"
 
Duh! Binadamu ikiwa mvua atalalamika likija jua atapiga kelele kwa kuwa haridhiki na hali moja. hongera kwa mleta uzi umenigusa.
 
Mtoa mada hoja yako dhaifu.Hivi Rais wetu ana maadui gani ambao wangepelekea Muhimbili isifikike kwa sababu za kiusalama?
Gharama ya ulinzi ndani ya nchi na gharama ya safari kwenda marekani plus matibabu kipi kinazidi chenzake?
Kwa nini serikali isiboreshe mifumo ya hospitali zetu ili pia kwa kigezo chako dhaifu ziweze kutoa hizo executive services kwa viongozi kama Rais?
Nashangaa elimu unayojivunia ina tofauti gani na ujinga?
Watanzania nchi nzima hali zao ni mbaya kwa huduma duni,mbovu,na pia ukosefu wa vifaa tiba na madawa lakini rais anafanya anasa nje ya nchi,kwako wewe ni sawa tu!
Kinacholalamikiwa si ujinga maana rais angeenda nje ya nchi kwa maradhi ambayo kiutaalamu na kiuwezo wa hospitali zetu hayatibiki isingekua hoja.Lakin prostate gland inaweza kushughulikiwa na hospitali zetu bila shida.Kama si anasa ni nini?
Ifikie kipindi huo ujinga ulionao unaouchukulia werevu ukutoke ili nchi hii ithubutu kusema ina wasomi!
SI SAHIHI HATA KIDOGO RAIS KUWAACHA WATANZANIA WAKIFARIKI NA KUTESEKA KWA MAELFU KWA HUDUMA MBOVU ZA AFYA NA UKOSEFU WA MADAWA,NA YEYE KUKIMBILIA MAREKANI KWA MATIBABU"

Ni Rais yupi wa Tanzania ambae hajawahi kutibiwa nje ya nchi?

Kila mwenye uwezo wake Tanzania anakwenda kutibwa nje, wala si ajabu, na hata wengi wasikuwa na uwezo wanapelekwa na serikali kila mara kwa mara.

Nyerere alifia Hospital nje ya Tanzania, au ulikuwa bado hujazaliwa?
 
Ni Rais yupi wa Tanzania ambae hajawahi kutibiwa nje ya nchi?

Kila mwenye uwezo wake Tanzania anakwenda kutibwa nje, wala si ajabu, na hata wengi wasikuwa na uwezo wanapelekwa na serikali kila mara kwa mara.

Nyerere alifia Hospital nje ya Tanzania, au ulikuwa bado hujazaliwa?

Nyerere alikua anaumwa cancer ya damu kwa uwezo wa hospitali zetu haitibiki. Prostate cancer inatibika hata hospitali ya wilaya.Na hili jambo nimeshalifafanua hapo juu. Kweli Ujinga una una gharama kubwa sana.Naanza kuipata hiyo picha ya mada husika.
 
Tatizo sio kumlinda mkuu wa kaya,tatizo ni ufisadi na wizi anaoufanya wa kuzidi kuliweka hili taifa katika hali masikini zaidi.Moyo wa kumlinda mwizi unatoka wapi?
 
Ni kweli umeujaribu ujinga na umevaa kama koti!. Wataka kutuaminisha hakuna ma-surgeons wanaoweza kumfanyia upasuaji hapa nchini? Huku ni kuwadhalilisha madaktari wetu na kuwadharau wananchi kwa kitendo chake cha kudharau vya kwetu na kutukuza vya wageni. Kwangu mimi, hili halivumiliki wala kusameheka.

Wajua gharama anazotumia kule kwa siku kuwa zingetosha kujenga maabara za shule nchi nzima na vifaa vya kutosha kwa miaka mitano?. Pia zingetosha kuwapa vijana wetu mikopo ya kusomea? Itoshe kusema kwa hili la kuwaacha ndugu zetu wakitaabika mahospitalini bila dawa, amevuruga mno. Jiulize, ungekuwa wodini kisha ukaandikiwa dawa na zikakosekana, ungemsifu?. Acha ujinga na sera zako za lumumba. Ushachukua buku 7?.
 
Kama swala ni ulinzi na usalama wa raids wakati akitibiwa, basi angeenda kutibiwa hospital ya rufaa ya lugalo kwani VIP section imejitenga na jeshi lingesaidia ulinzi
 
Katika rule of law kunakitu kinaitwa equality before the law.
kamsemo hako kinawapoteza wasomi wengi hasa wa kisiasa pamoja na wale wote waliokimbia umande. kwamaana hujifanya na wao wako equal na watu wote kitu ambacho sio kweli.

EQUALITY BEFORE THE LAW = Equal should treated equal and unequal should treated unequal.

Mimi sio mwanasiasa wala si mwanachama wa CCM! But Sometimes nashujudia wapinzani wakipotosha kwa hoja za kipu.uzi sana.

Natoa pole kwa waji.nga wote.
 
Hivi hizi shule huwa mnaenda kujifundisha ujinga?

Nenda karekebishe na uandike neno sahihi "prostate".

Kawarekebishe kwanza wale ndugu zako wa kurugenzi ya matamko na mipasho ikulu manake MR. CONFIDENT kaichomoa kwenye tamko lao kama ilivyo
 
Last edited by a moderator:
mwacheni presidah atibiwe nje yeye si kaamua na yeye si kaona huko atapata huduma nzuri kuliko huku nyumbani.
ila akistaafu muulizeni kwanini aliamua kwenda kutibiwa nje kuitoa hiyo tezi lake badala ya kwenda hospital hapa tanzania.....?
 
Mimi nilichojifunza ni kuwa kumbe hata rais akiwa hayupo maisha yanaendelea tu kama kawaida!
Tofauti ni moja tu kuwa shillingi inazidi kushuka kwa kasi na huenda week hii ikaishia na rekodi ya $1 = 1,800/-!
 
mleta uzi..mimi swali langu moja tu.. Kwa huduma zetu je kulikuwa na uwezekano wa rais kutibiwa na madaktar wetu akapona au hakuna uwezekano huo...?
 
Very interesting thread kwakwel,kama Mzee Mkapa alienda nje basi na shemeji yetu nae aende???hiyo si hoja jaman,hoja ni kwamba huyu aboreshe huduma tupunguze mzigo kwa watawala kwenda nje,sio rais sio mbunge yeyote yule,mara kadhaa husema serikal yake imeboresha sekta ya afya sasa kama imeboreshwa why he is in Maryland?
 
Akitokea mzalendo wa kweli akawa kiongozi wa taifa hili, cha kwanza atahakikisha huduma zote muhimu hapa nchini zinapatikana bila tatizo, atahakikisha sectors zote za kiuchumi zinaendeshwa vizuri na ukusanyaji wa kodi mzuri na miradi ya kimaendeleo ikibuniwa ili kuongeza kipato cha wananchi na taifa kwa ujumla ili sifa na hadhi ya nchi yake ikue.
hivi vyote vikifanyika hatutasikia kiongozi fulani kaenda nje ya nchi kufuata huduma fulani ziadi ya ziara za kitaifa kwa manufaa ya nchi yake. Hatutasikia malalamiko mengi kama yanayoelekezwa sasa kwa viongozi wetu kutoka kwa wananchi na taasisi mbalimbali. Watu wote wataipenda nchi hii na hata kuwa tayari kufichua aina yoyote ya uovu (mikubwa kwa midogo) katika taasisi husika za kiusalama.
Ili hili litokee huchukua muda na hata kuendelezwa na viongozi watakaofuata maana ni ngumu kwenda tofauti na utaratibu ulioukuta vinginevyo mpinzani ndiye awe amechekua madaraka. Kwa umri wa nchi yetu tangia tupate uhuru yote haya yangekuwa yameshawezekana kama viongozi wetu wangekuwa REAL PATRIOTS to their country( TANZANIA ).
tuendelee kumuomba Mungu ili tupate mtu ambaye yuko tayari kuifia nchi yake ( move the mountain or dying trying ).
Kwa Hali ilivyo sasa nchini sishangai viongozi kwenda kutibiwa nje maana hawana uhakika wa maisha yao kama watatibiwa nchini. Je Hali ikoje kwa wananchi wenye matumaini ya kupona katika hospitali zetu ndani ya nchi? Mbona viongozi wanakuwaga mstari wa mbele katika kuonesha mifano wakati wa upimaji na si katika kupata matibabu wakati wanaumwa?
TUREKEBISHE MAZINGIRA YETU NDANI Y A NCHI. LET'S ALL FORGET ABOUT THE PAST, LET'S ALL WORK TOGETHER FOR THE BETTERMENT OF OUR OUNTRY. TUGETHER WE CAN
 
Bongo bhana! Nimefanya utafiti wangu binafsi tena kwa makini na uweledi wa hali ya juu nikagundua umaamuma wetu uliokubuhu ni genetic. Hatutawahi kubadilika kamwe awe msomi au nani nå awe bongo ama popote pale dunian tabia yetu ni ile ile ya upopompo. Na nina uhakika hata kabinti ka chekechea kakipewa nchi katawale kanaweza tu na mambo yakaenda tena vizuri. Kitakachotusaidia tu ni kuhalalisha uvutaji wa bangi baaaas! Nyambaff zetu!!
 
Back
Top Bottom