Elisante Yona
Senior Member
- Oct 6, 2009
- 130
- 24
MAWAZIRI wote wamezuiwa kusafiri kikazi nje ya Jiji la Dar es Salaam kutokana na kile kinachoelezwa ni maandalizi ya kukabidhi ofisi kwa mawaziri wapya ambao wanatarajiwa kutangazwa wakati wowote kuanzia sasa.
Taarifa hizo zimekuja siku moja tu tangu Ikulu kupitia kwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Salvatory Rweyemamu, kuwataka Watanzania kuwa na subira kwa kuwa Rais Jakaya Kikwete wakati wowote kuanzia sasa atatoa uamuzi dhidi ya tuhuma zinazomkabili Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
Profesa Muhongo na baadhi ya viongozi wengine wa Serikali, wanahusishwa na sakata la uchotwaji wa zaidi ya Sh bilioni 306 kwenye akaunti ya Tegeta Escrow
Endelea kufuatilia,
Taarifa hizo zimekuja siku moja tu tangu Ikulu kupitia kwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Salvatory Rweyemamu, kuwataka Watanzania kuwa na subira kwa kuwa Rais Jakaya Kikwete wakati wowote kuanzia sasa atatoa uamuzi dhidi ya tuhuma zinazomkabili Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
Profesa Muhongo na baadhi ya viongozi wengine wa Serikali, wanahusishwa na sakata la uchotwaji wa zaidi ya Sh bilioni 306 kwenye akaunti ya Tegeta Escrow
Endelea kufuatilia,