Rais kikwete atembelea wagonjwa muhimbili

Rais kikwete atembelea wagonjwa muhimbili

Mkuu huyu ni msanii wa hali ya juu ndio maana hata utendaji dhaifu wa Mawaziri wake haushtukii kabisa. Mara mbili sasa imebidi Wabunge waje juu na kumshinikiza ili afukuze watendaji wabovu ndani ya Baraza lake la Mawaziri na hao waliofukuzwa ni asilimia ndogo sana. Baraza lote la Mawaziri limejaa mizigo mitupu ndio maana kila sekta nchini ni hovyo hovyo.

Najuta kuwa na rais wa nchi ana akili nyembamba hivi....hivi hata huwa anafikiriaga huyu haya mambo au anakurupuka tu
 
baada ya kutoka kutibiwa kwenye hospitali za maana akaona awapitie mazezeta kidogo awakejeli kabla ya kwenda kula bata magogoni! kwani kuwaona kwake ndipo watapona hata kama hawajapata tiba yoyote? ama kweli kenyata hakukosea aliposema kwamba nyerere anaongoza maiti. hawa watanzania wa sasa ni zaidi ya maiti.
 
QUOTE=tpaul;8215044]baada ya kutoka kutibiwa kwenye hospitali za maana akaona awapitie mazezeta kidogo awakejeli kabla ya kwenda kula bata magogoni! kwani kuwaona kwake ndipo watapona hata kama hawajapata tiba yoyote? ama kweli kenyata hakukosea aliposema kwamba nyerere anaongoza maiti. hawa watanzania wa sasa ni zaidi ya maiti.[/QUOTE]

Mkuu najuta kuwa na rais bogus kama huyu!sasa yeye katoka kutibiwa nje then ana kuja anawaangalia wagonjwa walivyo banana na kulala chini huku wakikosa dawa!kweli ina ingia akilini hii???O.M.G!!!hili ni furushi kabisa!
 
Sishangai kabisa rais wa nchi kwenda matibabu US, bongo hospitali za ovyo sana, sijui zitarekebishwa lini, Hospitali kama muhimbili ina jina kubwa ila ukilinganisha facilities na hospitali za nje, ile ni kama hospitali inayokua owned na chuo kimoja tu, tena ya chuo inakua na facilities kali zaidi.. Nawaheshimu sana madaktari wetu ila nchi yetu imewaangusha kutumia potential zao to the fullest...
 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali mtoto Andrew Simba(15) aliyelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili wakati Rais alipowatembelea na kuwafariji baadhi ya wagonjwa katika wodi ya Mwaisela leo.
View attachment 129013

Angefanya la maana kama angechekiwa afya yake hapo badala ya kwenda US
 
Kama kawaida wagonjwa waliolazwa chini kutokana na kukosa vitanda walihamishwa ili Mheshimiwa asiwakanyage.

By the way hiyo ziara imeachieve nini, hicho kitu alichoachieve kingeshindwa kuwa achieved bila yeye kwenda physically huko?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Yaani muhimbili nikwenda tu kuona wagonjwa, yeye kutibiwa hata kwa winchi hamumpeleki muhimbili.
 
Kazi kubwa alifanya rostam ya kutoa rushwa ktk kamati za maccm yamchague zezeta kuongoza ili avune superprofit na wananchi mazezeta yakesema eti chaguo la rostam ni chaguo la mungu.si unaona mikataba mingi holela inamuhusu yeye.
Ebu tusubiri 2015 rostam atatuchagulia zezeta gani jingine
 
Acheni wivu yy ameguswa kama kiongozi kwenda kuwatembelea wagonjwa inahusu akikaa maneno akisema maneno na nyie ni mizigo tu huyo si malaika bwana.
 
Angefika Muhimbili na kuagiza vitanda viwekwe haraka sana kwa gharama sawa na safari yake!angetoa Mil 500 magodoro,mashuka,blankets na vitanda vingejaa pale....pia angeagiza CT Scan na Xray hospitali zote nchini ziwepo!hapo ingeleta maana!
 
kama mtu inakuuma sana 2015 siyo mbali unachukua fomu katiba ipo wazi ila tahadhari usiwe na kichaa. watanzania tupunguze kulalamika
 
Lipi jema kwenu nyie mahafidhina?

jema ni rais kikwete aboreshe huduma za hospitali ili wote tutibiwe hapahapa badala ya kuteketeza mamilioni ya pesa za walipakodi kwenda kucheck afya nje ya nchi. wewe hulioni hilo mburula mkubwa?
 
kama mtu inakuuma sana 2015 siyo mbali unachukua fomu katiba ipo wazi ila tahadhari usiwe na kichaa. watanzania tupunguze kulalamika

wewe umeona hilo ndio suluhisho? kichaa chako kimesababishwa na nini? huduma za hospitali hazifai halafu unataka watu tukae kimya? kichwa chako kimejaa konokono!
 
Acheni wivu yy ameguswa kama kiongozi kwenda kuwatembelea wagonjwa inahusu akikaa maneno akisema maneno na nyie ni mizigo tu huyo si malaika bwana.

amemgusa mamako? kawapelekea dawa na vitanda au ameenda kushuhudia jinsi wanavyolala chini na kufa kwa kukosa dawa? usijitoe akili.
 
Akitoka hapo atajipumzisha Ruaha, Serengeti au Kilimanjaro kwaajili ya mwisho wa mwaka, then atafanya ziara ya ndani kwenye mikoa 2 au 3. Halafu huyo ndani ya pipa kuelekea Ulaya. Tusisahau hawezi kosa kwenda Brazil kwenye lile Kombe.
 
Back
Top Bottom