idriss
JF-Expert Member
- Mar 11, 2014
- 720
- 366
Huyu Kikwete mnafiki tu, yeye ndiye kinara wa udini hapa Tanzania! Amalize muda wake aende zake.
Tupe ushahidi kama uko nao ndugu tafadhari si yuwafaham uzuri mkono mtupu haurambwiii.
Huyu Kikwete mnafiki tu, yeye ndiye kinara wa udini hapa Tanzania! Amalize muda wake aende zake.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa kuna ushahidi sasa unaothibitisha kuwa baadhi ya mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wamekuwa wanachaganya dini na siasa wakitumia dini kuunga mkono baadhi ya vyama vya siasa na shughuli za kisiasa nchini.
Aidha, Rais Kikwete amewaomba mabalozi hao kuiokoa Tanzania katika majanga makubwa yanayoweza kuipata kwa kutumia dini kuendeleza siasa, hatua ambayo ameielezea kama njia ya hatari kweli kweli.
Rais Kikwete alikuwa anazungumza usiku wa Jumatatu, Oktoba 6, 2014, wakati wa chakula cha usiku ambacho alikula na viongozi wa dini nchini ambao wanaendelea na mkutano wao wa mwaka kwenye Hoteli ya White Sands ya Dar es Salaam.
Mkutano huo wa siku nne ulioanza juzi unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders Initiative for Peace and Co-existence ni mwendelezo wa mikutano ya viongozi wa dini kubwa za Kikristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini. Mkutano wa mwisho ulifanyika mwaka juzi, 2012 kwenye Hoteli hiyo hiyo.
Aidha, Mkutano huo ambao moja ya wadhamini wake ni taasisi ya Programme for Christian-Muslim Relations in Africa (PROCMURA) yenye makao yake makuu mjini Nairobi, Kenya, unahudhuriwa na mabalozi 15 wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini na mashirika kadhaa ya kimataifa likiwemo lile la Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP).
Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao katika Mkutano huo ni wa Ujerumani, Iran, Marekani, Norway, Uturuki, Sweden, Canada, Denmark, Finland, Misri, Qatar, Uswisi, Palestina, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Saudi Arabia na Umoja wa Ulaya (EU). Viongozi wa dini wanaoshiriki katika Mkutano huo wanatoka Zanzibar, Dar es Salaam, Mwanza, Morogoro, Mtwara, Lindi, Arusha, Geita na Mbeya.
Akizungumza kwenye chakula hicho cha usiku, Rais Kikwete aliungana na Mshauri Mkuu wa PROCMURA ambaye alionya kuhusu hatari za kweli zinazoendelea kuikabili dunia kwa sababu ya kuingiza dini katika siasa (Politicisation of Religion) na kuingiza siasa katika dini (Religinasation of Politics).
Rais Kikwete amewaambia viongozi hao: Mwakilishi wa PROCMURA ametoa ujumbe mzito sana. Ametoa fumbo ambako amewaasa mabalozi wasiingize dini katika siasa na wasiingize siasa katika dini. Na mimi nataka kuungana naye na kuwaomba mabalozi waiokoe nchi yetu katika majanga makubwa yanayoweza kutokana na kutumia dini kuendeleza siasa. Ni njia ya hatari kweli kweli.
Ameongeza Rais Kikwete: Kuna ushahidi sasa kuwa baadhi yetu, baada ya kushindwa kutumia ukabila katika kuendeleza siasa, sasa mmegeukia dini. Mnatumia dini katika kuunga mkono baadhi ya shughuli za kisiasa na baadhi ya vyama vya siasa.
Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu Dar es Salaam.
7 Oktoba, 2014.
Kikwete atoe ushahidi wa watu wanaochanganya dini na siasa ! Rais naye si mhathirika wa hili ?
Safi sana, akina GWAJIMA na genge lake wakome.
Haina shida kama haukuwa usanii wa kutangaza kitu hewa ambacho hakikukusanywa ili kuonyesha ulimwengu kuwa kimekusanywa! Au isiwe watu walipewa kabla toka kwa Gwajima Mwenyewe wafanye kutoa alichotoa ili filamu ya kisanii ionekane!
Anyway sina tatizo.Tatizo langu kama hizo hela zilizokusanywa ziliingia akaunti binafsi ya Gwajima badala ya akaunti ya kanisa hapo pana maneno.Lakini kama zilikusanywa ni mali ya kanisa basi najua v milioni mia saba si haba zinatosha kuwapa mitaji waumini wengi wa Kwa GWAJIMA ambao ni malofa wa kutupwa kuweza kuondokana na umaskini.
Lakini kama amepewa Gwajima BINAFSI AKANUNULIE Flora Mbasha GARI la kifahari hapo sikubali.
....si kweli,Rais amesahau kuwa kuna padre aliuwawa kule zanzibar kwa sb tu ya dini yake?,lakini pia kuna mwingine alipigwa risasi ya kidevuni.Hapa nia ilikuwa risasi ya kichwani lakini target tu ndio ilikataa.Lakini pia tumeona pale mbagala ambako makanisa ya SDA,CATHOLIC na LUTHERANI yaliaharibiwa na waumini wa dini ya kislam eti kwa sb tu kuna taarifa kuwa katoto fulani alikojolea quaran ya katoto fulani.Sasa reaction hapa umeisoma?.Hapa kuna kitu.Lakini kama haotoshi kule kagera walokole waliokuwa kwenye mkesha waliuwawa wote kanisani kwao.....hapa kuna kitu.