Rais Kikwete amteua Bibi Mwanahamisi Omari Kitogo kuwa msaidizi wa Rais katika Huduma za Jamii

Ofisi ya Rais ina mawaziri na manaibu kibao, kuna makamu wa Rais ambaye na ofisi yake ina mawaziri na manaibu na wakurugenzi. Kuna Ofisi ya waziri mkuu ambayo pia ina mawaziri na manaibu na wakurugenzi kibao, kuna wizara za kisekta ambazo pia zina mawaziri manaibu wakurugenzi, maafisa wakuu, maafisa waandamizi, maafisa daraja la I na la II kibao. Wote hao wako kwa ajili ya kumsaidia Rais. Kuna vikao vya mawaziri na vikao vya makatibu wakuu ambayo humshauri Rais na kutekeleza mambo mbalimbali. Duuu kweli utumishi wa umma umevamiwa.
 
Hivi JK na hawa wasaidizi kutoka katika taasisi binafsi na siyo utumishi wa umma yeye anawajuaje ufanisi wao na integrity yao kama siyo kutembea majina ya maswahiba na marafiki kwenye briefcase.
Katika utawala wake ndio hii dhana ya uteuzi wa kutoka katika private firms imejijenga sana tofauti na awamu nyingine zilizopita na kwa kiasi kikubwa na ushikaji wa wanamtandao.Tazama punde baada ya kuchukua uraisi kitengo cha habari na mawasiliano alichukua wanahabari wanamtandao wote wakapewa nafasi ofisi ya Raisi yupo Salva Rweyemamu-mzee wa Kagera,Bi Mwingira aliyekuwepo wakati wa Mzee Mkapa akarudishwa mambo ya nje,wapo pia akina Premi Kibanga alikuwa BBC.Ofisi ya Waziri Mkuu yupo Ireni Bwire huyu alikuwa Mtanzania enzi hizo na Said Nkuba huyu alikuwa Uhuru akaenda Mwananchi kukaanga sumu ya kwamba DR.Salimu ndiye alihusika na mauji ya Mzee Karume na Ofisi ya Makamu wa Raisi yupo Kijana wa fujo UDSM Boniface Makene huyo alikuwa mwananchi na baadae Rai ya Rostam Aziz . Kwenye Ubalozi na Ujaji ndio kabisa wapo wazee wa IMMA Advocates-Mujulizi amepewa ujaji,Mwanaidi amepewa ubalozi na wengine ni jaji Dr Fauz alikuwa wakili wa kujitegemea na jaji mwingine ni Jungu alikuwa wakili wa kujitegemea kwenye ukuu wa Wilaya ndio usiseme.
Kwa mifano hii na wasiwasi na uteuzi wake kama unakidhi hasa vigezo vya utumishi wa umma na kama siyo mapenzi binafsi kama raisi kutunuku watu vyeo.
Naamini katika uteuzi vyombo muhimu husika kama tume ya utumishi wa umma,mahakama,bunge nk.Hivyo katika kupitia majina hao hawawezi kupitikana kwenye orodha ya utumishi wa umma hivyo ni wazi rais ndio anawafanyia kazi vyombo vilivyoundwa kwa mujibu wa sheria kutafuta jina badala ya vyombo kupendekeza majina kwake na yeye kufanya uteuzi kwa.
 
Nachopata shida na wasiwasi CDM watakapochukua nchi 2015 watachukua mazuri yapi kutoka kwa mtangulizi wao Baba Riz...
Msaada tutani wadau.
 
wa jf msisahau mpango wa ujenzi wa ukumbi wa mikutano pale ikulu labda dada ndo ameletwa kwa ajili ya kusimamia na kuendesha ukumbi huo.
 
Inabidi tuweke record zetu vizuri ili mwisho wa siku tutengue teuzi zote hizi zisizo na kichwa wala miguu
 
Embu tuwe wa kweli, hapa sio wivu, Katika watu millioni arobaini, hakuna aliyeonekana kasomea kwenye taaluma ya jamii mpaka tumchukue mkadiriaji majengo. Kwa nini asingempeleka huyo dada kule Takukuru aende kuangalia jinsi pesa zetu zinaliwa kwa kupandisha gharama za ujenzi kwenye majengo ya serikali. Namwonea huyo dada huruma maana ndiyo mwisho wa utaalamu wake. Atakapokuja raisi mwingine atapangua na atajikuta hana kazi. Raisi wetu tumia hekima Mungu aliyokupa japo kidogo. Mungu ibariki Tanzania.
 
Nilifikiri mngeomba CV ya huyo bibie badala yake jina limekuwa ishu!



CV gani mkubwa unayotaka tuombe wakati tume-google wee hatujapata contribution yake yoyote ambayo kizazi hiki cha dot.com kitafaidika? Hebu google Zidane uone moto wake
 
Kila rafiki wa rais lazima alambe cheo kwa katiba hii

Mkuu heshima juu, una maono. Huyu quantinty surveyor na habari za huduma za jamii namuona kama ni mbadala wa Mar-hum Sheikh Hussein Yahya zaid kuliko mtaalamu wa Community Development. Ni dhahiri kuwa hakuwa katika mfumo rasmi wa serikali lakini anafahamiana na JK kibinafsi kufikia kuaminiwa hata kupewa kazi hii. Mambo ya ulaji tupu. Katiba ijayo lazima iweke ukomo wa vitu vya namna hii.

Sasa nahitaji kumjua mshauri wa JK katika maswala ya "kuzurura duniani". Nimhoji JK anatafuta nn huko!!
 
Kuna Wizara za Mambo ya Ndani (usalama wa raia), Afya (matibabu na magonjwa), Maji (Inajieleza), Elimu (Inajieleza), Ujenzi (barabara), Uchukuzi (Usafirishaji). Zote hizo zina mawaziri, manaibu, makatibu wakuu, wakurugenzi wa Idara mpaka kufikia mtu wa chini kabisaaaa!!

Huyu Mshauri wa Rais katika maswala hayo, anafanya nini kilichoshindwa kujulikana kwa Rais. Hivi ni kweli kufahamu matatizo ya kijamii kunahitaji mshauri, tena surveyor???

Ahh, JK!!
 
Hivi hiyo kazi aliyokuwa anaifanya (ukadiriaji majengo) na hiyo mpya ya huduma za jamii mbona naona kama hazifanani? Au ndo kusema atajifunzia huko huko ofisini? Labda mimi ndo nitakuwa sielewi hapo!

Kwani majukumu yake haya mapya ni yapi?
 
...pengine alikuwa anajenga majengo mengi ya kuishi binadamu,which means kwa mtazamo wa mteuzi ni experience tosha ya masuala ya kijamii,sabu naamini alikuwa lazima anakutana na jamii katika kukubaliana jinsi gani majengo yao wanapenda yajengwe,hii ndo Tz ya JK,''THE MORE U TRY2MAKE URSELF MORE QUALIFIED IN WHAT U DO BEST ACORDING2UR FIELD,ZE MOST U GET THROWN FAR-FAR AWAY FROM RIGHFUL PLACES OF URZ..''
 
Back
Top Bottom