Rais Karume Ajipanga Kujiongezea Muda Madarakani

Junius

JF-Expert Member
Mar 11, 2009
3,181
139
VIONGOZI wa chama cha National League for Democracy (NLD) Zanzibar, wamependekeza utawala wa Rais Amani Abeid Karume uendelee kwa miaka miwili zaidi, ili kutoa nafasi ya kumaliza matatizo yaliyojitokeza katika uandikishaji wapiga kura.

Wakizungumza na waandishi wa habari jana katika Idara ya Habari (Maelezo) Zanzibar, Naibu katibu Mkuu wa NLD, Rashid Ahmed Rashid na Mkurugenzi wa Haki za Binadamu wa Chama hicho, Nassor Khamis, walisema mazingira ya sasa hayatoi nafasi kwa uchaguzi mkuu uliokuwa huru na wa haki.

Walisema hoja zao za kutaka uchaguzi mkuu wa 2010 ucheleweshwe hadi mwaka 2013, zinatokana na kuwa watu wengi bado hawana vitambulisho vya ukazi au vyeti vya kuzaliwa, ili kuwawezesha kupata vitambulisho hivyo.

Walisema wananchi hawapaswi kulaumiwa moja kwa moja kwa kukosa vitambulisho, “lawama ni kwa ofisi ya vitambulisho, Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) na Chama cha Wananchi (CUF).

“Tulikuwa Pemba hivi karibuni na utafiti mdogo tulioufanya unaonesha kuwa watu wengi watakosa kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, kwa sababu ya kutokuwa na vitambulisho. “Mfano katika baadhi ya shehia zaidi ya watu 300 wenye umri wa kati ya miaka 18 na 70 wamekosa kujiandikisha kwa sababu ya kutokuwa na vitambulisho au vyeti vya kuzaliwa.

"Tunataka serikali isaidie kuhakikisha kwamba kila Mzanzibari anatendewa haki kwa kupata fursa ya kuchagua rais. Bora tuchelewe ili haki itendeke,” Rashid alisema. Alielekeza lawama dhidi ya ofisi ya Msajili wa Mzanzibari na kutoa vitambulisho na kusema watendaji hawakujiandaa na wamekuwa wakitoa taarifa za uongo kwa Rais Karume.

Alisema hakuna taarifa iliyotolewa mapema na serikali, ZEC wala ofisi ya vitambulisho, kuwa vingetumika katika uandikishaji Zanzibar katika uchaguzi wa mwakani.

“ZEC na ofisi ya vitambulisho wangekataa suala la vitambulisho kuwa lazima katika uchaguzi wa mwakani kwa sababu wananchi hawakuandaliwa na taarifa haikutolewa. Kwa hivi sasa haiwezekani kuwatenga watu wote kwa sababu ya uzembe, ni lazima watu wapewe fursa,” alisema Rashid.

Pia alitoa lawama kwa ofisi ya vitambulisho kuwa, “imekuwa ikitoa vitambulisho kwa watu wasio Wazanzibari. Wazungu na watu kutoka Tanzania tayari wana vitambulisho hivi, kwa hiyo Rais wa Zanzibar atachaguliwa na wageni.” Khamis aliungana na Rashid katika kulalamikia utendaji wa ofisi ya vitambulisho na ZEC na kusema CUF imekuwa inasababisha vurugu.

“Tayari tumemwandikia barua Rais Karume barua na nakala tumempelekea Rais Jakaya Kikwete kuhusu kasoro zote katika demokrasia nchini ikiwamo udhaifu wa ofisi ya vitambulisho, Uhamiaji na Idara ya Mambo ya Nje kwa kuwapa wageni vitambulisho na haki za kuishi nchini bila ridhaa ya wananchi,” Khamis alisema.

Katika mkutano huo, pia wanasiasa hao walikanusha taarifa zilizotolewa na ubalozi wa Marekani kuhusu tahadhari ya usafiri wa kuja Zanzibar na kusema Zanzibar na hasa Pemba ambako mvutano wa uandikishaji ulianzia, hali ni shwari.

“Taarifa ya Marekani kuwataka raia wake kuchukua tahadhari wanapokuja Zanzibar, imetolewa bila utafiti wa kina. Pemba ni shwari. "Marekani wamezoea kuingilia mambo ya ndani ya Zanzibar na kwa taarifa yao, uchumi wa Zanzibar unaweza kuathirika,” walisema na kuongeza kuwa wamewaandikia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon kulalamikia hatua hiyo ya Marekani.


SOURCE: HABARI LEO.
 
Ndiyo maana wanachafua hali makusudi kumbe wanamipango yao.
 
hakuna kitu hapo kwani wakiamua kuwaandikisha wapiga kura kwa umakini na uaminifu siwatamaliza mapema na kutoathiri tarehe ya uchaguzi? Hii inaweza kuwa janja ya CCM kujiongezea muda wa utawala baada ya kubaini kuwa hawawezi kuishinda CUF.

Endapo itashindikana kufanya uchaguzi, basi iundwe interim government siyo Karume aendelee
 
Karume anaomba leo amalize maana yu maji na keshachoka wala hana hamu tena ya uraisi ,hivi akimaliza tu anaenda zake kupumzika kwenye nyumba zao Amerika na sizani kama ataendelea kuishi tena hapa Tz ,na hili kwa viongozi wengi tu ambao tayari wameshajenga nchi za nje na wameshajitayarisha kuishi huko,kuna kundi au genge litaondoka hapa Tz ,hili ni la viongozi wa bara na Zanzibar kila mmoja ataelekea upande wake na kuanza maisha huko akiwa hana shida kubwa sana.
 
VIONGOZI wa chama cha National League for Democracy (NLD) Zanzibar, wamependekeza utawala wa Rais Amani Abeid Karume uendelee kwa miaka miwili zaidi, ili kutoa nafasi ya kumaliza matatizo yaliyojitokeza katika uandikishaji wapiga kura.

Wakizungumza na waandishi wa habari jana katika Idara ya Habari (Maelezo) Zanzibar, Naibu katibu Mkuu wa NLD, Rashid Ahmed Rashid na Mkurugenzi wa Haki za Binadamu wa Chama hicho, Nassor Khamis, walisema mazingira ya sasa hayatoi nafasi kwa uchaguzi mkuu uliokuwa huru na wa haki.

Walisema hoja zao za kutaka uchaguzi mkuu wa 2010 ucheleweshwe hadi mwaka 2013, zinatokana na kuwa watu wengi bado hawana vitambulisho vya ukazi au vyeti vya kuzaliwa, ili kuwawezesha kupata vitambulisho hivyo.
Kuandikisha watu (wa umri wa miaka 18+) ambao hawafikii hata laki 6, unahitaji miaka 2/3. Ama kweli huu ni ukichaa kama sio ulimbukeni. Wanaosema hivyo ni chama cha siasa chenye mategemeo ya kushika utawala wa nchi? Kudadeki, kweli hapa ni kubonyenyeza Kizenji, mdebwedo!
 
Kuandikisha watu (wa umri wa miaka 18+) ambao hawafikii hata laki 6, unahitaji miaka 2/3. Ama kweli huu ni ukichaa kama sio ulimbukeni. Wanaosema hivyo ni chama cha siasa chenye mategemeo ya kushika utawala wa nchi? Kudadeki, kweli hapa ni kubonyenyeza Kizenji, mdebwedo!
Hii wala si hoja ya karume, hawa wana lao jambo
 
Karume yu maji hana hamu tena ya kuendelea kutawala zanzibar. Ila CCM inataka kutawala zaidi na zaidi Znz
 
Kuandikisha watu (wa umri wa miaka 18+) ambao hawafikii hata laki 6, unahitaji miaka 2/3. Ama kweli huu ni ukichaa kama sio ulimbukeni. Wanaosema hivyo ni chama cha siasa chenye mategemeo ya kushika utawala wa nchi? Kudadeki, kweli hapa ni kubonyenyeza Kizenji, mdebwedo!


Kwa kweli inashangaza sana!
Haiwezekani wau wachache namna hiyo wasajiliwe kwa muda wa miaka miwili ilhali inawezekana kuwasajili ndani ya miezi isiyozidi miwili. Kwani kuwapa vyeti vya kuzaliwa hao waliokosa vitambulisho inachukua muda gani kama watatumia taratibu sahihi za uandikishaji?
Kweli Zenji kuna mambo!
 
Kuandikisha watu (wa umri wa miaka 18+) ambao hawafikii hata laki 6, unahitaji miaka 2/3. Ama kweli huu ni ukichaa kama sio ulimbukeni. Wanaosema hivyo ni chama cha siasa chenye mategemeo ya kushika utawala wa nchi? Kudadeki, kweli hapa ni kubonyenyeza Kizenji, mdebwedo!

Mimi nakuunga mkono serikali yoyote makini haitashindwa kuwapa wananchi wake vyeti vya kuzalia kwa wakati.Hii ikilinganishwa na idadi ya watu wenyewe ambao hawazidi 800,000 huitaji miaka miwili na zaidi kuifanya kazi hii.Hapa inaonyesha kuwa kuna hila zinatembea ili kuwanyima wananchi husika haki yao ya kikatiba ya kupiga kura.
 
Kibunango,duniani humu kuna mwanasiasa asiye na uchu wa madaraka? Hebu ntajie mmoja Mkuu?


Kwi kwi kwi!
Bishanga, ulitaka Kibunango amponde Karume ilhali yeye mwenyewe na Karume wanatoka chama kimoja? Angalia avatar yake kwanza! Kumbuka yaliyotokea mwaka 2000 wakati na wa/ na baada ya uchaguzi, utagundua kwamba jamaa ana uchu ama la!
Ukiachilia mbali chama, Kibz na Karume wanatokea kisiwa kimoja.
Teh teh teh!
 
hakuna haja ya karume kujichafua kwa kutaka kubadili katiba[kwakuwa atashindwa]aje tu huku bara agombee urais mwakani au abadilishane nafasi na shein
 
Kasema nani mbona hakumwachia GB asimame naye 2005?
1995 mbona alikubali kumwachia Komandoo! GB atulize game kwani 2000-10 ni zamu ya watu wa mjini...

Karume yu maji hana hamu tena ya kuendelea kutawala zanzibar. Ila CCM inataka kutawala zaidi na zaidi Znz
Ndivyo wanavyosema jamaa wa Daraja bovu na ile radio yao?

Kibunango,duniani humu kuna mwanasiasa asiye na uchu wa madaraka? Hebu ntajie mmoja Mkuu?
Ni Karume, Aman Karume!
 
Kwi kwi kwi!
Kumbuka yaliyotokea mwaka 2000 wakati na wa/ na baada ya uchaguzi, utagundua kwamba jamaa ana uchu ama la!
Hebu fafanua hapo! Nimjuavyo Karume hana uchu wa madaraka... muda wake ukifika ataweka manyanga chini na kumpisha Prez mpya pale uwanja wa Amani.
 
......Hebu fafanua hapo! ....

1. Kwa mtu ambaye hana uchu wa madaraka, asingeweza kuwavumilia watu waliokimbia na masanduku ya kura wakati ule wa uchaguzi na kwenda kubadili kura porini ili ashinde kwa kishindo, lazima angewashikisha adabu, kwa sababu walikuwa wanachafua amani ya nchi na kumchafua yeye binafsi, ambaye ndiye mteuzi wa watumishi wa tume ya uchaguzi ya huko.

2. Kwa mtu ambaye hana uchu wa madaraka, asingeweza kutaka kumjua mtu aliyemnyima kura mwaka juzi wwakati wa kura sa uongozi wa sisiemu, hii ina maana alitaka apate 100% ya kura zote. Ktk dunia ya leo, hakuna mahali unaweza kupata 100 % ya kura zote, unless umeiba.

3. Kuhusu kujiongezea muda wa kuwa madarakani, suala hili siwezi kumtuhumu Karume, najua hawezi kuthubutu kamwe!

Kibz, tuendelee na mjadala!
 
Re: Rais Karume Ajipanga Kujiongezea Muda Madarakani

Quote:


Kasema nani mbona hakumwachia GB asimame naye 2005?



1995 mbona alikubali kumwachia Komandoo! GB atulize game kwani 2000-10 ni zamu ya watu wa mjini...


Quote:


Karume yu maji hana hamu tena ya kuendelea kutawala zanzibar. Ila CCM inataka kutawala zaidi na zaidi Znz



Ndivyo wanavyosema jamaa wa Daraja bovu na ile radio yao?


Quote:


Kibunango,duniani humu kuna mwanasiasa asiye na uchu wa madaraka? Hebu ntajie mmoja Mkuu?



Ni Karume, Aman Karume!

Malafyale unajipanga kuteuliwa kuwakilisha Jimbo la Ikulu?.

Kila la kheir
 
Re: Rais Karume Ajipanga Kujiongezea Muda Madarakani

Quote:​



Kasema nani mbona hakumwachia GB asimame naye 2005?




1995 mbona alikubali kumwachia Komandoo! GB atulize game kwani 2000-10 ni zamu ya watu wa mjini...


Quote:​



Karume yu maji hana hamu tena ya kuendelea kutawala zanzibar. Ila CCM inataka kutawala zaidi na zaidi Znz




Ndivyo wanavyosema jamaa wa Daraja bovu na ile radio yao?


Quote:​



Kibunango,duniani humu kuna mwanasiasa asiye na uchu wa madaraka? Hebu ntajie mmoja Mkuu?




Ni Karume, Aman Karume!

Malafyale unajipanga kuteuliwa kuwakilisha Jimbo la Ikulu?.

Kila la kheir
 
Back
Top Bottom