Rais, kama umetoka kwenye kampeni, fuatilia haya mahojiano ya Maxence Melo na The Chanzo

Rais, kama umetoka kwenye kampeni, fuatilia haya mahojiano ya Maxence Melo na The Chanzo

Sifi Leo

Platinum Member
Joined
Mar 30, 2012
Posts
5,937
Reaction score
10,815
Wapo wajinga wanaodhania yakuwa kila mtu wanaemuona anatokea MLANGO wa IKULU ni usalama wa taifa na ndio maana wanaogopa kumbe wengine ni "majwakwama"

Niyaache haya,

Mh Rais Mimi ni raia wako, mwema ninae ipenda nchi yangu kwa moyo wangu wa dhati, nimefatilia mahojiano yaliyofanyika MASAA matano yaliyopita KUHUSIANA na jinsi mtandao wa JamiiForums ulivvyofungwa
Na sababu za kufungiwa kwa mtandao HUO.

Mkurugenzi huyo hakuficha sababu ameweka sawa ikiwemo
1. TAARIFA ya yule bwana gabachori yaani Rostamu kununua Mgodi wa makaa ya mawe kwa SHILINGI bilioni 5.

Mkurugenzi WA JamiiForums anasema Ile habari wao hawakuwa na makosa maana Ile habari aliyeiweka aliitoa kwenye vyanzo vingine akaiweka pale JamiiForums Ili sisi wananchi tuweze changia mjadala na kweli tulichangia mimi nilichangia kwa kusema kabachori kama ni kweli basi ni jizi la rasilimali za kitaifa.

Lengo LILIKUWA ni kumtia hasira ili akai
fungue kesi Ili ukweli ujulikane Ili Hali kuwa Badala yake Rostam aliishia kumwita yule Mzee sijui siku hizi anaandikia CHOMBO Gani na kuelezea porojo porojo. TU.

Mh Rais SUALA la Rostam kwa kweli linaumiza nchi ebu CCM litafutieni majibu mwafaka.

SUALA la pili ni kuhusu picha ULIZOPIGA wewe na lile lijibaba la kizimbambwe wewe mwenyewe mama,

Mama hapa sitokulaumu ila naomba unielewe Kuna pahala protocol za IKULU zinachezewa vibaya mno.

Mh Rais mkurugenzi wa JamiiForums anadai miezi kadhaa iliyopita alikuwa Zimbabwe kwenye masuala yake na ni Moja ya vitu alivyokutana navyo.

TENA HATARI NI KUTAADHALISHWA DHIDI YA MTU WAKIWAJUZA YAKUWA JITU LILE NI JITU HATARI.

Mh Rais picha ZAKO na za yule bwana alizipost yule bwana kwenye mitandao yake yeye mwenyewe, kama ilivyo kawaida mtanzania Mmoja akazibeba akaziweka JamiiForums Ili nasi tuchangie au tutoe MAONI yetu.

Mh Rais baada ya picha hizo kuwekwa, hata Mimi nilichangia maoni kwa kulisema vibaya jitu lile kwani picha zake hazikuwa na maadili ya utanzania.

Swali ni Moja jamaaa ni linani?

Kama jamaa aliweza post picha hizo Instagram na mwana JF akazileta hapa tuzione, tatizo LILIKUWA wapi? Zikifutwa JamiiForums zitakuwa zimefutwa Instagram?

Jibu ni hapana Sasa swali kwanini ifungiwe JamiiForums au Kuna chuki?
 
Nimefatilia mahojiano ya Maxence Melo na kila uchwao namfatilia pole pole, nafatilia huu upuuzi wa kuzima mitandao wakiwa wanaongea au kuifungia jamiii forumu hakika naiona hatari kubwa mno kwa taifa ENDAPO watu HAWA wataamua kusema yakuwa Sasa WATATUMIA MJIA NYINGINE KUWAFIKIA WATANZANIA HASA VIJANA, KUWAPA TAARIFA WANAZO DHANIA NI MHM KWAO.

NAIONA HATARI KUBWA MNO KWA SABABU WAPO WATU WACHACHE KATIKA TAIFA WANAO JIPENDEKEZA KWA UTAWALA BAADAE WANAWEZA TUMIKA KAMA KONDOMU NA WAKAKOSA LA KUFANYA.


NAIONA HATARI KUBWA MNO
 
Huwa tunajifunza kwa makosa tunayoyafanya na wengine pia huwa hawataki kujifunza wala kujua makosa waliyoyafanya
 
IMG-20250916-WA0003.jpg
 
Wapo wajinga wanao dhania yakuwa kila mtu wanae mwona anatokea MLANGO wa IKULU ni usalama wa taifa na ndio maana mawaogopa kumbe wengine ni "majwakwama"
Mkuu 'Sifi', nimeisoma mada yako kwa uangalifu; kwa kujuwa wewe husimamia wapi katika maswala ya taifa letu.

Baada ya kuusoma nimebaki najiuliza, hasa maudhui ya mada hii ni nini hasa?

Kuwalaumu na kuwakashifu kabisa Rostam Azziz na hilo jamaa la Zimbabwe? Hili ndilo ulikuwa msukumo wa kuleta mada hii hapa?

Picha niliyo nayo kichwani baada ya kusoma mada yako, ni kama unamwondolea lawama zote huyu"Mheshimiwa Rais", asiyejuwa maana ya kuitwa kwa heshima hiyo kubwa unayompa wewe!
Mh Rais picha ZAKO na za yule bwana alizipost yule bwana kwenye mitandao yake yeye mwenyewe, kama ilivyokawaida mtanzania Mmoja akazibeba akaziweka JamiiForums Ili nasi tuchangie au tutoe MAONI yetu.

Mh Rais baada ya picha hizo kuweka hata Mimi nilichangia kwa kulisema vibaya jitu lire kwani picha zake hazikuwa na maadili ya utanzania
Akina Rostam na hayo majamaa mengine; muhusika wa yote hayo anajulikana.

Hakuna sababu yoyote ya kulaumu kwingine zaidi ya mtu mwenyewe asiyejuwa maana ya nafasi aliyo nayo.
 
Kwa hiyo hili Bonge nyanya pamoja na wahuni wenzake ndiyo wamechangia mtandao wetu pendwa kufungiwa! Basi hii nchi ni ya hovyo sana.
Tanganyika itakombolewa na kurudisha hadhi yake kwa watanganyika hawa washenzi wasifikiri wataendelea na wanayoyafanya.
 
Dah! Mungu tusaidie watanzania tupate haki tuishi kwa uhuru na amani nchini kwetu
 
Back
Top Bottom