Rais JP Magufuli, Mulika na Shirika la Bima la Taifa( NIC)

Tenderness

Member
Nov 28, 2015
29
18
Hiki ni kichaka kingine cha wezi wa pesa za Umma! Yaani mtu unazungushwa kama unafuatilia mali ya urithi vile, vocha nimesainishwa ila hundi hawatoi na wakati pesa ilishaletwa siku nyingi.. Toka mwezi wa saba mpaka leo tunaelekea mwezi december naishiwa kuambiwa sijui nenda TIRA mara sijui kwa msuluhishi wa migogoro ya bima.

Nataka nikwambie mh rais ni kwamba binafsi niliamua kukatia bima gari langu NIC kwa sababu ya uzalendo wangu tu kwa taifa langu, ila bahati mbaya matatizo ndo yakanikuta. Kilichotokea ni kama vile huyu meneja ametumia hiyo hela kufanya mambo yake hivyo ananizungusha ili yeye aendeleee kunufaika na pesa yake! Nimepoteza mpaka ajira yangu kwaajili ya kutumia muda mwingi kufuatilia madai yangu!

Naomba umulike shirika hilo kwani limekua kama kichaka cha kujipatia pesa wakati watanzania wa hali ya chini tunateseka,sio kama hatuoni kampuni binafsi, ni vile tu sisi wengine tunaipenda sana hii nchi kwahiyo hata tunafikiria kufanya lolote tunawaza kwanza nchi yangu inanufaikaje!

Mwisho kabisa nakutakia kila lililo jema katika safari yako ndefu ya kukamua majipu, ni kazi ngumu na yenye gharama kubwa lakini nataka nikukikishie kwamba MUNGU ANAEISHI yuko mbele yako atakushika mkono na kukupigania, na zaidi Watanzania wote tunasali sana kwaajili yako!

Ni mimi mzalendo, sijafunguka sana kwa sababu za kiusalama!
 
Atatumbua JIPU moja baada ya jingine tumpe muda Dkt.Pombe.

Kubwa zaidi tumuombee manake kila mahali wamejaa wajanja wajanja tu, watu wenye viburi na kujitutumua. Hii nchi ni ya kwetu sote. Inauma sana kunyanyaswa na Mtanzania mwenzio kisa tu anafanya kazI katika shirika la serikali.
 
NIC ina matatizo sanaaaa inabidi imulikwe sanaa

Wamejaa wazee wazee tu, wanaendesha shirika kama vile familia zao, ubabe na ukoloni.. kuna siku nilikuta jamaa wanafuatilia bima sijui ya afya ile dah, niliumia sana kwa jinsi walivyokua wakitendewa.
 
Duh kwa hali hii si itabidi amulike hadi SACCOS za kina mama mitaani

Mkuu kama hizo SACCOS ni za serikali amulike tu kwa kweli.. watumishi wa serikali ni wasumbufu sana,Nawapongeza sana Walimu wa serikalini, wanafanya kazi katika mazingira magumu ila bado hawana dharau, wanamoyo wa kufanya kazi na kuwalea watoto wetu kama vile ni watoto wao wa damu au ndugu zao.
 
NIC linahitaji mageuzi makubwa...ni sawa na ATCL na mashirika mengi ya umma ambayo yanahujumiwa na urasimu wa baadhi ya viongozi wa juu
 
Back
Top Bottom