GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,550
- 108,882
Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzia na Usalama nchini Dkt. John Pombe Joseph Magufuli leo nakuletea Kilio changu Kikubwa Kwako na ambacho naamini pia ni cha Watanzania wengi ambacho TCRA ndiyo wanatusababishia haya maumivu bila kuchukua hatua zozote stahiki.
Mheshimiwa Rais mwaka jana kulitokea matangazo mara mbili kwamba Ving'amuzi vyote vinatakiwa kutowalipisha Watanzania zile Local Channels ambazo ni ITV, Channel Ten, Clouds tv, East Africa tv na Star tv bila kuisahau na TBC1 lakini Mheshimiwa Rais Sisi Wananchi wako tunasikitika sana kwamba hadi hivi Mimi GENTAMYCINE naandika huu uzi bado Sisi Wananchi wako tunaendelea Kulipishwa kila mwezi Shilingi Elfu Sita ( 6,000/= ) kama Tozo ya mwezi ili tuweze kuona hizo local channels tajwa hapo juu.
Mheshimiwa Rais ni mwezi uliopita tu December 2017 kuna Tangazo la TCRA lilikuwa likizunguka mitandaoni na nadhani hata wafuatiliaji wengi wa haya masuala ya Mitandao waliliona ambapo TCRA ilikuwa ikiwataka Wamiliki wote wa Makampuni ya Ving'amuzi nchini Tanzania kuanzia tarehe 1 January mwaka huu wa 2018 waache kuwatoza Wananchi Pesa ili waweze kuona hizo Local Channels tajwa hapo juu ila kwa masikitiko makubwa Mheshimiwa Rais hadi hivi leo hali ni ile ile na hakuna lolote lililotendeka na bado Sisi Wananchi wako tunaendelea tu Kunyanyaswa na TCRA kwa haki yetu tunayoistahili.
Mheshimiwa Rais haiingii akilini leo hii Sisi Wananchi wako unaotutetea kila uchao tunalazimishwa na hayo Makampuni ya Ving'amuzi kulipia hata Channel ambayo bado ipo katika majaribio ya TVE na nyinginezo ambazo hazina umuhimu wowote Kwetu. Na kinachotuuma zaidi Mheshimiwa Rais ni kwamba hata Waziri husika pamoja na Naibu wake wamenyamaza tu hali ambayo inazidi kutuumiza Sisi Wananchi wako wa hali ya chini.
Na hapa nisifiche wala kuzunguka Mheshimiwa Rais Kampuni ninayoiongelea na kuipigia makelele kwa huu Uonevu kama siyo Unyanyasaji ni hii ya StarTimes japo najua yawezekana kuna Watu wengine labda na Wao wana lawama zao kwa Ving'amuzi wanavyovitumia ila tunaomba sana msaada wako Mheshimiwa Rais katika hili na ikiwezekana utoe rasmi AMRI yako ya Kiutalawa kama siyo Kiuongozi ili hizo Local Channels zote Tano tuwe tunaziangalia bure kama ambavyo ilikubaliwa awali lakini pia uwawajibishe vilivyo Viongozi wa TCRA na wale wa Wizarani kwani wametusababishia mno usumbufu na mateso Sisi wapiga Kura wako.
Naomba kwa yoyote yule ambaye ana mawasiliano ya karibu na Msemaji wa Ikulu Gerson Msigwa anisaidie Kumfowadia haraka huu uzi wangu ili na Yeye asubuhi hii hii amfikishie Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli kusudi ajue TCRA na Wizara husika wanavyotutesa kutokana na hili suala zima la Local Channels kuonyeshwa bure pasipo malipo. Inauma mno na inakera sana na mpaka unaona GENTAMYCINE nimeandika hivi jua nimechoka na nimekereka Kunakotukuka.
Nawasilisha.
Mheshimiwa Rais mwaka jana kulitokea matangazo mara mbili kwamba Ving'amuzi vyote vinatakiwa kutowalipisha Watanzania zile Local Channels ambazo ni ITV, Channel Ten, Clouds tv, East Africa tv na Star tv bila kuisahau na TBC1 lakini Mheshimiwa Rais Sisi Wananchi wako tunasikitika sana kwamba hadi hivi Mimi GENTAMYCINE naandika huu uzi bado Sisi Wananchi wako tunaendelea Kulipishwa kila mwezi Shilingi Elfu Sita ( 6,000/= ) kama Tozo ya mwezi ili tuweze kuona hizo local channels tajwa hapo juu.
Mheshimiwa Rais ni mwezi uliopita tu December 2017 kuna Tangazo la TCRA lilikuwa likizunguka mitandaoni na nadhani hata wafuatiliaji wengi wa haya masuala ya Mitandao waliliona ambapo TCRA ilikuwa ikiwataka Wamiliki wote wa Makampuni ya Ving'amuzi nchini Tanzania kuanzia tarehe 1 January mwaka huu wa 2018 waache kuwatoza Wananchi Pesa ili waweze kuona hizo Local Channels tajwa hapo juu ila kwa masikitiko makubwa Mheshimiwa Rais hadi hivi leo hali ni ile ile na hakuna lolote lililotendeka na bado Sisi Wananchi wako tunaendelea tu Kunyanyaswa na TCRA kwa haki yetu tunayoistahili.
Mheshimiwa Rais haiingii akilini leo hii Sisi Wananchi wako unaotutetea kila uchao tunalazimishwa na hayo Makampuni ya Ving'amuzi kulipia hata Channel ambayo bado ipo katika majaribio ya TVE na nyinginezo ambazo hazina umuhimu wowote Kwetu. Na kinachotuuma zaidi Mheshimiwa Rais ni kwamba hata Waziri husika pamoja na Naibu wake wamenyamaza tu hali ambayo inazidi kutuumiza Sisi Wananchi wako wa hali ya chini.
Na hapa nisifiche wala kuzunguka Mheshimiwa Rais Kampuni ninayoiongelea na kuipigia makelele kwa huu Uonevu kama siyo Unyanyasaji ni hii ya StarTimes japo najua yawezekana kuna Watu wengine labda na Wao wana lawama zao kwa Ving'amuzi wanavyovitumia ila tunaomba sana msaada wako Mheshimiwa Rais katika hili na ikiwezekana utoe rasmi AMRI yako ya Kiutalawa kama siyo Kiuongozi ili hizo Local Channels zote Tano tuwe tunaziangalia bure kama ambavyo ilikubaliwa awali lakini pia uwawajibishe vilivyo Viongozi wa TCRA na wale wa Wizarani kwani wametusababishia mno usumbufu na mateso Sisi wapiga Kura wako.
Naomba kwa yoyote yule ambaye ana mawasiliano ya karibu na Msemaji wa Ikulu Gerson Msigwa anisaidie Kumfowadia haraka huu uzi wangu ili na Yeye asubuhi hii hii amfikishie Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli kusudi ajue TCRA na Wizara husika wanavyotutesa kutokana na hili suala zima la Local Channels kuonyeshwa bure pasipo malipo. Inauma mno na inakera sana na mpaka unaona GENTAMYCINE nimeandika hivi jua nimechoka na nimekereka Kunakotukuka.
Nawasilisha.