domokaya
JF-Expert Member
- Apr 22, 2010
- 3,545
- 1,719
Huna haja ya kwenda laboratory kupima akili za watanzania, wewe angalia tu vitendo vyao. Rais wa nchi ya Tanzania na washirika wake wakitumia mamilioni ya pesa kumfanyia sherehe ya kuzaliwa marehemu. Kawaida mtu akizaliwa na kufa siku inayobaki kukumbukwa ni ile aliyokufa na si kuzaliwa. Mfano Nyerere anakumbukwa katika siku ya kifo chake, Karume nae hivyohivyo sasa leo TANU alishakufa miaka 30 na ushee halafu eti ikakumbukwa siku ya kuzaliwa. Yaani kama vile unachamba kabla ya kujisaidia wakati kopo lenyewe la maji lipo moja.