Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,898
- Thread starter
- #21
wewe si unamuona obama yuko mtaani anasukuma toroli lenye bidhaa alizotoka kununua sokoni,...tena kwa usafiri wa miguu kabisa
Ningetazamia ungesoma maelezo niliyotoa ziada ya kichwa cha habari. Obama unayemzungumzia alipofika pale farmers market kununua maboga kwa ajili ya kumbukumbu ya hallowen na thanksgiving gari alilokuja nalo alikaa seat ya kati kama kawaida. Na hapo alipo ukiangalia sana hiyo avator unaona kwa mbali wanausalama wakivinjari kulinda eneo hilo huku idadi ya watu eneo hilo limethibitiwa, ni wachache sana.
Hoja yako kutetea Rais Kikwete kukaa seat ya mbele na kufanya ulinganisho wa Obama kusukuma tolori lililosheheni maboga pale farmers market hali mshiko kwa maana ya mazingira ya kununua sokoni na kusafiri barabarani ni mambo mawili tofauti na yanayohitaji mfumo wa ulinzi tofauti. Utetezi wako naona umekosa nguvu kwa hoja ya kusukuma tolori. Ni sawa na kushika shovel (sepetu) anapotia utongo kuzika wafu ni nafasi tofauti na hii ya kusafiri barabarani.
Anaposafiri barabarani usalama si kutoka kwa maadui au kwa tafsiri nyingine watu wenye malengo mabaya naye, la hasha, ila ni usalama pia wa vyombo vya usalama kwa mategemeo kwamba seat ya kati itokeapo ajali ina unafuu wa kusalimika kuliko seat ya mbele.