Corticopontine
JF-Expert Member
- Sep 20, 2019
- 664
- 1,272
Raia mmoja wa China mwenye umri wa miaka 41 amethibitishwa kuwa na kisa cha kwanza cha maambukizi ya homa ya ndege isio ya kawaida.
Maafisa hawakutoa maelezo kuhusu jinsi mtu huyo alivyoambukizwa virusi hivyo vya H10N3 ambavyo vinadaiwa kusambaa kwa urahisi miongoni mwa wanadamu.
Mkaazi huyo wa mkoa wa Jiansu, ambaye alipatikana na maradhi hayo wiki iliopita kwa sasa amepona na yuko tayari kutoka hospitalini.
Kuna homa nyingi za ndege na haijasikika kwamba watu wanofanya kazi ya kuku huambukizwa maradhi hayo.
Ufuatiliaji wa waliokaribiana na mwathiriwa haukupata wagonjwa wengine.
Tume ya afya mjini Bejing NHC imesema siku ya Jumanne kwamba mkaazi huyo wa mji wa Zhenjiang alilazwa hospitali tarehe 28 mwezi Aprili na kupatikana na virusi vya H10N3 miezi mitatu baadaye.
"Hakuna hata kisa kimoja cha ugonjwa huo kilichoripotiwa duniani. Kisa hiki ni cha maambukizi kutoka kwa ndege hadi kwa binadamu , na hatari ya kusambaa kwake ipo chini sana '', ilisema tume hiyo, kulingana na ripoti ya gazeti la Global Times.
Tume hiyo pia ilisema kwamba virusi hivyo haviwezi kuhatarisha maisha ya ndege na kwamba pia haviwezi kusambaa kwa haraka.
Shirika la Afya duniani WHO liliambia Reuters kwamba wakati huu hakuna ishara ya maambukizi ya kutoka binadamu mmoja hadi mwengine.
''Mradi homa ya ndege husambaa katika kuku omaambukizi ya hma hiyo miongoni mwa wanadamu hayatashangaza, hatua inayotuonesha kwamba tisho la mlipuko wa homa ya ndege ni endelevu'', imeelezea WHO.
Kwa sasa kuna mlipuko kati ya ndege wa homa ya H5N8 ambayo imesababisha mamia ya maelfu ya kuku kukatwa midomo katika nchi kadhaa za Ulaya
Mnamo mwezi Februari, Urusi iliripoti kisa cha kwanza cha homa hiyo miongoni mwa wanadamu.
Maambukizi ya binadamu sio mengi tangu mlipuko mkubwa wa virusi vya vya H7N9 kuwaua takriban watu 300 mwaka 2016 na 2017.
Maafisa hawakutoa maelezo kuhusu jinsi mtu huyo alivyoambukizwa virusi hivyo vya H10N3 ambavyo vinadaiwa kusambaa kwa urahisi miongoni mwa wanadamu.
Mkaazi huyo wa mkoa wa Jiansu, ambaye alipatikana na maradhi hayo wiki iliopita kwa sasa amepona na yuko tayari kutoka hospitalini.
Kuna homa nyingi za ndege na haijasikika kwamba watu wanofanya kazi ya kuku huambukizwa maradhi hayo.
Ufuatiliaji wa waliokaribiana na mwathiriwa haukupata wagonjwa wengine.
Tume ya afya mjini Bejing NHC imesema siku ya Jumanne kwamba mkaazi huyo wa mji wa Zhenjiang alilazwa hospitali tarehe 28 mwezi Aprili na kupatikana na virusi vya H10N3 miezi mitatu baadaye.
"Hakuna hata kisa kimoja cha ugonjwa huo kilichoripotiwa duniani. Kisa hiki ni cha maambukizi kutoka kwa ndege hadi kwa binadamu , na hatari ya kusambaa kwake ipo chini sana '', ilisema tume hiyo, kulingana na ripoti ya gazeti la Global Times.
Tume hiyo pia ilisema kwamba virusi hivyo haviwezi kuhatarisha maisha ya ndege na kwamba pia haviwezi kusambaa kwa haraka.
Shirika la Afya duniani WHO liliambia Reuters kwamba wakati huu hakuna ishara ya maambukizi ya kutoka binadamu mmoja hadi mwengine.
''Mradi homa ya ndege husambaa katika kuku omaambukizi ya hma hiyo miongoni mwa wanadamu hayatashangaza, hatua inayotuonesha kwamba tisho la mlipuko wa homa ya ndege ni endelevu'', imeelezea WHO.
Kwa sasa kuna mlipuko kati ya ndege wa homa ya H5N8 ambayo imesababisha mamia ya maelfu ya kuku kukatwa midomo katika nchi kadhaa za Ulaya
Mnamo mwezi Februari, Urusi iliripoti kisa cha kwanza cha homa hiyo miongoni mwa wanadamu.
Maambukizi ya binadamu sio mengi tangu mlipuko mkubwa wa virusi vya vya H7N9 kuwaua takriban watu 300 mwaka 2016 na 2017.