figganigga
Platinum Member
- Oct 17, 2010
- 26,996
- 60,090
Mkoa wa Mbeya ni kati ya mikoa 30 ya Tanzania ikipakana na Zambia na Malawi, halafu na mikoa ya Rukwa, Tabora, Singida na Iringa.Umesahau na mchele wao ule wa Kyela!! duh! hiv Kyela nayo ipo Mbeya? au nimekosea
Kuna wilaya 9 zifuatazo: Mbeya Mjini, Mbeya Vijijini, Rungwe, Kyela, Ileje, Mbozi, Chunya, Momba na Mbarali.
Mbeya ni kati ya maeneo yanayopendeza kabisa ndani ya Tanzania ikiwa na sehemu za Ziwa la Nyasa, Ziwa Rukwa, milima ya Mbeya, milima ya Rungwe, Uwanja wa juu wa Uporoto, Uwanja wa Usangu ingawa haukufikiwa bado na utalii.
Wenyeji wa wilaya ya Chunya ni Wabungu na waishio huko zaidi ni Wanyiha.
Wilaya ya Rungwe ni eneo penye mvua nyingi katika Tanzania. Mkoa wa ujumla ni mojawapo kati ya mikoa yenye kilimo kizuri inayotoa mazao ya kulisha taifa. Lakini maeneo makubwa ya Wilaya ya Chunya ni makavu.
Wilaya ya Chunya ina madini mbalimbali hasa dhahabu. Mbeya na Mbozi kahawa hupandwa. Rungwe pana chai nyingi, pamoja na Rungwe na Chimala hulimwa mpunga. Nyanda za juu kuna nafaka na viazi.
Kijiolojia mkoa wa Mbeya ni eneo la kukutana kwa mikono miwili ya Bonde la Ufa la Afrika ya Mashariki inayoendelaea hapa katika ziwa Nyasa.
[h=2]Kyela Location Map (Mbeya, Tanzania)[/h]