Raha ya ndoa upendwe na upendeke

Raha ya ndoa upendwe na upendeke

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
58,636
Reaction score
220,353
Ukipendwa kwenye ndoa ni kama unaishi pepo ya dunia. Hata uwe unakoroma usingizini mwenza ataichukulia poa tu. tena ukisafiri ana miss ule mkoromo wako.

Hata uwe unakojoa kitandani, ataongeza budget ya omo na kubadilisha shuka alfajiri huku kimya kimya akimtafuta daktari wa kukutibu.

Makosa tunayofanya ni kumtafuta msichana wa kuvutia na unawaacha wale wanaokupenda kwa upendo huu wa agape.

Wadada wanatafuta handsome, aliyesoma, mwenye kuendesha gari nzuri. Yule Hamis next door ambae angeweza kukinga matapishi yako kwa mkono ukiugua unamuona zobwe.

Dunia ni majanga.
 
Aisee mimi miaka miwili nimeona ndoa HELL,
Mama mkwe,
Mchana kutwa,usiku,simu tu mama mkwe.
 
Basi tunalijuaga hilo ke anampenda me kuzidi lakini akiangalia mmm sio type yangu anatafuta wapaka carorite
nakumuacha mwenye mapenzi ya kweli

Pia kadhalika me anampenda ke vizuri sana ila ke naye akitizama chogo daa huku anataka wanyoa kiduku na wapaka poda sasa mwisho wake ni majanga tupu na vilio visivyoisha
 
Back
Top Bottom